Saturday, December 1, 2007

Mchimba madini afanya uchafu hadharani

IPATE KAMILI HAPA: WWW.GLOBALPUBLISHERSTZ.COM

Aisha Madinda kukamua Desemba 7 Diamond


Mnenguaji mahiri wa Bendi ya African Stars ‘Twanga Pepeta International’ Aisha Madinda ameibuka na kuzima uvumi uliokuwa ukisambaa kwa kasi ya ajabu kuwa ameitema Twanga Pepeta.

Akizungumza na mwandishi wetu mapema wiki hii Kinondoni jijini Dar es Salaam, Aisha alisema kuwa ameshangazwa na uvumi huo kuwa aliamua kuachana na Twanaga Pepeta ikiwa imebaki siku chache tu bendi hiyo izindue albamu yake katika Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

“Watu wanazusha kuwa mimi nimeimwaga Twanga, lakini ninachotaka kusema ni kuwa mimi bado nipo Twanga ila nasumbuliwa na afya kidogo nawaomba wapenzi wangu wasiwe na hofu kwani naendelea vizuri, naamini Desemba 7 nitakuwepo Diamond Jubilee kwenye uzinduzi wa albamu yetu ya Mtaa wa Kwanza,” alisema Aisha.

Aisha Madinda ni miongoni mwa wanenguaji wachache wenye uwezo wa kuteka hisia za wapenzi wa muziki wa dansi nchini mara tu apandapo jukwaani na kuanza kupinda mugongo!

UDAKU ZAIDI: WWW.GLOBALPUBLISHERSTZ.COM

Thursday, November 29, 2007

HARAMBEE!


Waziri Mkuu, Edward Lowassa akimshukuru Mkurugenzi wa Mamlaka ya Elimu nchini, Mercy Silla na Mwenyekiti wa Mamlaka , Patrick Rutabanzibwa ambeye pia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji (kulia) baada ya Mamlaka hiyo hiyokutoa ahadi ya kujenga shule yenye thamani y ash. Milioni 1000 katika harambee ya kuchangia maendeleo ya elimu mkoani Kagera ilyofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam juzi. Wapili kushoto ni mshereheshaji , Peter Mavunde kutoka Dodoma Shilingi bilioni 1.4 zilichangwa katika harambee hiyo..(Picha na Ofisi ya Waziei Mkuu)

MACHO HAYANA PAZIA

Tuesday, November 27, 2007

HII NDO STAILI YA KUDOZI KAZINI!

11 reasons !

11 reasons why ladies today are still SINGLE:

1. The nice men are ugly.
2. The handsome men are not nice.
3. The handsome and nice men are Gay.
4. The handsome, nice and heterosexual men are married.
5. The men who are not so handsome, but are nice men, have no money.
6. The men who are not so handsome, but are nice men with money think ladies are only after their money.
7. The handsome men without money are after ladies money.
8. The handsome men, who are not so nice and somewhat heterosexual, don't think ladies are beautiful enough.
9. The men who think ladies are beautiful, that are heterosexual, somewhat nice and have money, are cowards.
10. The men who are somewhat handsome, somewhat nice and have some money and thank God are heterosexual, are shy and NEVER MAKE THE FIRST MOVE to ladies!!!!
11. The men who never make the first move, automatically lose interest in us when we take the initiative.
NOW WHO THE HELL UNDERSTAND MAN?
" Men are like a fine wine.
They all start out like grapes, and it's the ladies job to stomp on them and keep them in the dark until they mature into something you'd like to have dinner with."

Why breast cancer is usually found near the armpit

I was informed by the Moderator of Women's workcom that one of her rep. had been diagnosed with breast cancer and she is concerned that we should

inform our friends about this.

Ladies - some awareness!!! Gentleman - pass on to the ladies in your life, to all the women you know.

Some time ago, I attended a Breast Cancer Awareness seminar put on by Terry & A period.

I asked why the most common area for Breast Cancer was near the armpit. My question could not be answered at that time. This e-mail was just sent to me, and I find it interesting that my question has been answered. I challenge you all to rethink your every day use of a product that could ultimately lead to a terminal illness. As of today, I will change my use. A friend forwarded this to me.

I showed it to a friend going through chemotherapy and she said she learned this fact in a support group recently. I just got information from a health seminar that I would like to share. The leading cause of breast cancer is the use of anti-perspirant.

What? A concentration of toxins and leads to cell mutations,a. k.a.CANCER. Yes, ANTI-PERSPIRANT. Most of the products out there are an anti-perspirant /deodorant combination, so go home and check. Deodorant is fine, anti-perspirant is not.

Here's why: - The human body has a few areas that it uses to purge toxins; behind the knees , behind the ears, groin area, and armpits. The toxins are purged in the form of perspiration. Anti-perspirant, as the name clearly indicates, prevents you from perspiring, thereby inhibiting the body from purging toxins from below the armpits.

These toxins do not just magically disappear. Instead, the body deposits them in the lymph nodes below the arms since it cannot sweat them out. Nearly all breast cancer tumours occur in the upper outside quadrant of the breast area. This is precisely where the lymph nodes are located. Additionally, men are less likely (but not completely exempt) to develop breast cancer prompted by anti- perspirant usage because most of the anti-perspirant product is caught in their hair and is not directly applied to the skin.

Women who apply anti-perspirant right after shaving increase the risk further because shaving causes almost imperceptible nicks in the skin which give the chemicals entrance into the body from the armpit area .

PLEASE pass this along to anyone you care about. Breast cancer is becoming frighteningly common. This awareness may save lives.

RICHARD, RICKI'S ISSUE STILL HOTT!

GET FULL STORY FROM HERE: THE BONGO SUN ON LINE!

YOU ARE WHAT YOU EAT!


Shinikizo la juu la damu (High Blood Pressure): Suluhisho nil lishe bora-2
Wiki iliyopita tulianza kuelezea tatizo la shinikizo la juu la damu na jinsi ya kukabiliana nalo kwa kutumia chakula na matunda, leo tunamalizia kuangalia orodha ya vyakula na matunda hayo:

ZABIBU NA TIKITIMAJI
Tunda aina ya Zabibu ni maarufu sana mkoani Dodoma. Kama ulikuwa hujui faida na umuhimu wa tunda hili, basi ilewa kwamba lina kiasi kikubwa cha vitamini P ambayo hufanyakazi ya kuimarisha mishipa ya damu mwilini. Mbali ya Zabibu, Tikitimaji nalo ni tunda moja muhimu sana kwa wagonjwa wa shinikizo la damu au watu wanaopenda kujikinga.

Mbegu za Tikitimaji zinaaminika kuwa na uwezo wa kuyeyusha mishipa ya damu iliyoganda na matokeo yake kushusha shinikizo la juu la damu. Unachotakiwa kufanya ili kutumia mbegu za tunda hili kama dawa, chukua mbegu zake, zikaushe kisha zikaange halafu kula kama karanga kila mara.

WALI NA VIAZI VITAMU
Wali ni chakula kingine kizuri kwa mgonjwa wa shinikizo la damu, hasa wali uliopikwa kwa ule mchele wa rangi ya kahawia (brown rice) ambao unaaminika kuwa na kiwango kidogo sana cha mafuta, chumvi na Cholestrol. Aidha mchele wa kahawia una kiwango kikubwa cha madini aina ya Calcium ambayo hutuliza mishipa ya fahamu na kuondoa dalili za ugonjwa.

Mbali na mchele, viazi vitamu, hasa vilivyopikwa na maganda yake, vinaaminika kusaidia sana ushushaji wa shinikizo la damu. Inaaminika kwamba, viazi vitamu vinapopikwa na maganda yake, hunyonya kiasi kidogo sana cha chumvi ambayo mgonjwa hatakiwa kuitumia sana. Viazi vitamu vina kiasi kikubwa cha madini aina ya Potassium na hakina chumvi. Kiwango cha Magnessium kilichomo kwenye viazi, kinasaidia sana ushushaji wa shinikizo la damu.

JUISI YA MATUNDA
Juisi ya matunda halisi, hasa karoti na spinachi, inapotumiwa kwa pamoja au moja moja, huweza kutibu au kuzuia shinikizo la damu. Tengeneza kiasi cha nusu lita ya juisi hiyo mchanganyiko na kunywa kila siku mara moja au glasi mbili kila siku za jusi moja kati ya hizo mbili ili kujitibia au kujikinga na ‘Pressure’.

Kwa kifupi, mgonjwa wa shinikizo la damu, anapswa sana kuzingatia ulaji sahihi wa vyakula (Balanced Diet) kwa kupenda kula vyakula vyote ambavyo husaidia kumpa ahueni kama tulivyoainisha hapo juu baadhi yake. Pia ajiepushe kabisa na vyakula ambavyo huchangia hali yake kuwa mbaya. Kitu kingine muhimu ni kubadili mtindo wa maisha, fanya mazoezi na kupata muda wa kupumzika na kulala usingizi mzuri angalau saa nane kwa siku.

NYAMA NYEKUNDU NA MAYAI
Kama kuna chakula ambacho mgonjwa wa shinikizo la damu anapaswa kukiona kama sumu, basi ni nyama nyekundu (nyama ya ng’ombe, mbuzi, nguruwe, n.k) na mayai. Iwe mwiko kwa mgonjwa huyu kula vyakula hivyo, kwani vinapoliwa moja kwa moja hupandisha shinikizo la damu.

Hivyo kama wewe ni mgonjwa wa ‘pressure’ na unaendelea kula vyakula hivyo, basi ujue kamwe hutapona na unajiharakishia safari ya kifo. Nyama iliyo salama kwa mgonjwa huyu ni ya samaki na kuku aliyeondolewa ngozi.

Monday, November 26, 2007

FRIENDSHIP AND LOVE

Friendship and love defined in a single photo...... .
Now Forward it to all your friends:

Pnc: Kitu kigumu kwangu wakati wa kutongoza, sijui kuongea na madem, nina aibu sana

Mchizi aliyeingia ndani ya kumi na nane ya safu hii ni Pankras Ndaki Charles a.k.a PNC aliyetokea Mkoani Mwanza maeneo ya Pasias na kuhamia Dar es Salaam kunako familia ya Tip Top Connection kwa ajili ya kutafuta maisha kupitia sanaa ya muziki wa Bongo Flava.

Akiwa na umri mdogo, huku jina lake likiwa tayari vichwani mwa watu wengi, PNC alikutana na maswali mapya kibao, yakiwemo ya kizushi. Hebu yacheki.

1. Tabia zipi ulizokuwa nazo utotoni ambazo wazazi wako walikuwa hawazipendi?

Nilikuwa napenda kula sana, kutembea ovyo, vilevile nilikuwa mchafu ile mbaya kwasababu nilikuwa sipendi kuoga, kitu ambacho kiliwakera zaidi wazee.

2. Msichana mwenye umbo gani anakuzingua zaidi?
Nazinguliwa na msichana yeyote mrembo anayejipenda, ila ninaye wangu ambaye tunapendana sana.

3. Umeshawahi kutoswa ama kuwatosa mademu mara ngapi?
Duh! Hiyo kali, binafsi sijawahi kutoswa, ila kutosa nimewahi japo siyo wengi sana.

4. Nani wa kwanza kumkimbilia ukipata tatizo?
Watu wote walionizunguka au walio karibu na mimi Abdul Bonge, Babu Talle, Mully au Tip Top Family.

5. Ustaa umewahi kukusababishia matatizo gani?
Nashukuru Mungu tangu nimejulikana sijawahi kupata tatizo lolote kubwa mpaka nikashindwa kulitatua.

6. Kitu gani kigumu kwako wakati wa kumtongoza msichana?
Kitu kigumu kwangu sijui kuongea na madem, nina aibu sana

7. Uliwahi kugombana mara ngapi?
Niligombana sana wakati mdogo, lakini tangu nimekuwa na kuanza kujitafutia mwenye sijawahi kugombana na mtu.

Mengine kuhusu mchizi ambaye katika game ya muziki wa Bongo Flava kupitia 'kategori' ya kizazi kipya alitoka zaidi na kazi yenye jina la 'Mbona' bado anaisimamia albamu yake ya kwanza ambayo ipo kwa wadosi kitambo ikifanya vizuri sokoni na kazi nyingine kama I Need U, Huzuni, Nalia na nyinge kibao.

TAMASHA LA UKIMWI bado siku 6

Zikiwa zimesalia siku sita ili itimie Desemba Mosi, siku ya Ukimwi dunia, wakazi wa Mwanza na vitongoji vyake wanaisubiri kwa hamu kubwa burudani itakayoshushwa na mastaa mbalimbali wa muziki nchini.

Waandaaji wa tamasha hilo ambao ni Kamati ya Umoja wa Vijana CCM 'inayodili' na mapambano dhidi ya Ukimwi, wanawaomba wakazi wa Kanda ya Ziwa watakaofurika katika Uwanja wa CCM Kirumba siku hiyo, wajitolee vitu mbalimbali kwa ajili ya kuwasaidia watoto yatima ambao wazazi wao walifariki kwa Ukimwi.

'Tunaomba watu wenye nguo hata zilizotumika, madaftari, kalamu, chakula na vingine ambavyo wanahisi vinaweza kuwasaidia yatima hao, sisi tutashukuru na kuwafikishia popote walipo' ilisema sehemu ya taarifa ya waandaaji waliyoitoa kupitia safu hii.

Baadhi ya wasanii watakaopanda stejini siku hiyo ni pamoja na Fareed Kubanda 'Fid Q', Joseph Haule 'Profesa Jay', Hamis Baba 'H. Baba', Hardmad, Ambwene Yesaya 'AY', Flora Mbasha na wengine wengi. Mbali na shoo hiyo vijana watapata fulsa ya kupiga stori na wenzao kuhusiana na gonjwa la Ukimwi, huku kauli mbiu yake ikiwa ni 'Zuia Ukimwi, tunza ahadi'. Hiyo siyo siku ya kukosa mtu wangu, kumbuka kwamba hakuna kiingilio.

Wakali wa Taarab uso kwa uso Diamond Jubelee wiki hii

Ule mpambano wa Taarab uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa sanaa hiyo sasa umewadia, tunahesabu siku tatu tu iwadie Novemba 30, mwaka huu wapambanaji wakutane dani ya ukumbi wa Diamond Jubilee.

Kampuni za QSSP Group kupitia Kituo chake cha Televisheni cha C2C na LIRO Promotion ndiyo waandaaji wa shughuli hiyo nzito ambao waliyataja makundi yaliyofanikiwa kupenya na kuingia kunako fainali hizo ambayo ni Jahazi Modern Taarab (Wana wa Nakshi nakshi), Dar Modern Taarab (Watoto wa Kandoro, Wajukuu wa Makamba) East African Melody (Watoto wa mjini).

Meneja wa C2C, Bahati Singh alisema kwamba baada ya kutolewa kwa kundi la Zanzibar Stars kupitia mchuo uliokuwa unafanyika katika kituo hicho cha televisheni, mashabiki wanatakiwa waendelee kuyapigia kura makundi hayo matatu ili kuliwezesha moja kuibuka na ushindi siku hiyo ya fainali.

'Mashabiki wanatakiwa kupiga kura zao ili apatikane mshindi mmoja. Ili kuliwezesha kundi la East African Melody unaandika neno 'EAM' kupitia simu yako ya mkononi kisha unatuma kwenda namba 15551, Dar Modern Taarab unaandika 'DMT' kwenda namba 15551 na Jahazi Modern Taarab unaandika 'JMT' kwenda 15551', alisema Singh.

Mpambano huo unakujia chini ya wadhamini kibao, ikiwemo Kampuni ya Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Uwazi, Amani, The Bongo Sun, Championi, Risasi, Ijumaa na Ijumaa Wikienda.