Wednesday, May 29, 2013

Katika maadhimisho ya siku ya kimataifa ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa Tanzania yaahidi kuendelea kutoa ushirik

IMG_0224
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani Dk. Emmanuel Nchimbi akiwasili kwenye Mnara wa Mashujaa viwanja vya Mnazi Mmoja katika maadhimisho ya kumbukumbu ya Askari wa Kulinda amani wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na mabalozi wa nchi mbalimbali pamoja viongozi wa dini. (Picha na Dewji Blog).
IMG_0169
Mwakilishi wa Shirika la Chakula Duniani nchini Tanzania (WFP) Bw. Richard Ragan akiwasili kwenye viwanja hivyo jijini Dar es Salaam kushiriki kwenye maadhimisho ya kumbukumbu ya Askari wa Kulinda amani wa Umoja wa Mataifa.
IMG_0231
Mgeni rasmi Waziri Mambo ya Ndani nchini Dk. Emmanuel Nchimbi, Mwakilishi wa Shirika la Chakula Duniani nchini Tanzania (WFP) Bw. Richard Ragan na Kanali Dominic Mrope wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) wakitoa heshima kwa wimbo wa mataifa kwenye maadhimisho hayo.
IMG_0259
Mgeni rasmi Waziri Mambo ya Ndani nchini Dk. Emmanuel Nchimbi akielekea kuweka shada la maua kwenye Mnara wa Mashujaa ikiwa ni ishara ya kuwakumbuka askari wa kulinda Amani wa Umoja wa Mataifa walipoteza maisha wakiwa kazini.
IMG_0267  
Mh. Dk. Emmanuel Nchimbi akiweka shada la maua kwenye Mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa uliopo katika viwanja vya Mnazi Mmoja wakati wa maadhimisho ya kuwakumbuka Askari wa Kulinda Amani wa Umoja wa mataifa walipoteza maisha wakiwa kazini.
IMG_0269 
Mgeni rasmi Mh. Dk. Emmanuel Nchimbi akitoa heshima mara baada ya kuweka shada la maua kwenye mnara huo.
IMG_0271
Mwakilishi wa Shirika la Chakula Duniani nchini Tanzania (WFP) Bw. Richard Ragan akielekea kuweka shada la maua kwenye maadhimisho ya kuwakumbuka Askari wa Kulinda Amani wa Umoja wa Mataifa yaliyofanyika leo kwenye mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa uliopo viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar.
IMG_0274
Mwakilishi wa Shirika la Chakula Duniani nchini Tanzania (WFP) Bw. Richard Ragan akiweka shada la maua kwenye mnara huo.
IMG_0281
Kanali Dominic Mrope wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akiweka shada la maua kwenye mnara wa kumbukumbu ya Mashujaa kwa niaba ya Meja Jenerali Salum Mustafa Kijuu wakati wa maadhimisho ya siku ya kuwakumbuka Askari wa kulinda Amani wa Umoja wa mataifa yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja leo.
IMG_0284
Kanali Dominic Mrope wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) akitoa heshima zake mara baada ya kuweka shada la maua.
IMG_1145
Mmoja wa askari wa JWTZ akipendisha bendera ya Umoja wa Mataifa kama ishara ya kumbukumbu ya Askari wa Umoja huo wanaolinda Amani katika nchi mbalimbali za Afrika.IMG_0433
Mgeni rasmi Waziri wa Mambo ya Ndani Dk. Emmanuel Nchimbi akizungumza na wageni waalikwa wakati wa maadhimisho ya kuwakumba Askari wa Umoja wa mataifa wa Kulinda Amani yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja jijini Dar es Salaam leo.
IMG_0374
Mwakilishi wa Shirika la Chakula Duniani nchini Tanzania (WFP) Bw. Richard Ragan akizungumza kwa niaba ya Mratibu Kazi wa Umoja wa Mataifa hapa nchini Dk. Alberic Kacou kwenye maadhimisho ya Siku ya kumbukumbu ya Askari wa Umoja wa Mataifa wa kulinda Amani yaliyofanyika jijini Dar es Salaam leo.
IMG_0389
Zainab Abdallah moja ya Vilabu vya Umoja wa Mataifa akighani shairi wakati wa maadhimisho hayo.
IMG_0406
Baadhi ya Askari wa Umoja wa mataifa wa Kulinda Amani wakati wa maadhimisho hayo.
IMG_0407 IMG_0192

No comments: