Monday, December 7, 2015

CHUO KIKUU CHA USHIRIKA MOSHI (MoCU) CHAFANYA MAHAFALI YA KWANZA.

Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi  (MoCU) Pius Msekwa akitunuku Shahada ,Stashahada na Astashahada kwa wahitimu wa Chuo hicho wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo hicho.
Wahitimu wa kozi mbalimbali waliohitimu katika Chuo Kikuu cha Ushirika mjini Moshi,(MoCU)
Miongoni mwa wageni waalikwa alikuwepo pia Mbunge wa jimbo la Moshi mjini ,Jafary Michael.
Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika (MoCU) Profesa Faustine Bee akizungumza wakati wa sherehe za mahafali ya kwanza ya Chuo hicho yaliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Chuo hicho.
Miongoni mwa wahitimu walikuwepo pia Mbunge wa viti maalum,Sharry Raymond pamoja na Mkuu wa wilaya ya Mwanga ,Shaibu Ndemanga.
Baadhi ya wakufunzi katika chuo hicho.
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro ,Severine Kahitwa (Kulia) akiteta jambo na Meneja wa benki ya NMB ,tawi la Mandela mjini Moshi ,Emanuel Kashusho wakatiwa mahafali ya kwanza katika chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Kaimu Naibu Makamu wa Mkuu wa Chuo (Utawala na Fedha) Ndayizera Manta (Kushoto) akiwa na Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) Profesa Gerald Monera wakati wa mahafali ya kwanza ya chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Muongozaji wa sherehe ya mahafali hayo Cyril Komba akitoa muongozo wa shughuli hiyo iliyofanyika viwanja ya Chuo kikuu cha Ushirika Moshi.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ushirika ,Pius Msekwa akitoka katika viwanja vya Ushirika mara baada ya kumalizika kwa sherehe ya mahafali ya kwanza ya chuo hicho.
Baadhi ya wakufunzi wa Chuo hicho,Profesa Wakuru Magigi (kulia ) wakiwa na Mkuu wa Shule ya Polisi zamani Chuo cha Polisi Moshi,Matanga Mbushi .
Mkuu wa wilaya ya Ilala,Raymond Mushi (kushoto) akiwa na mmmoja wa wakufunzi katika chuo hicho Dkt Kaleshu ,wakipozi katika picha ya pamoja na Mbunge wa Viti maalum CCM ,Sharry Raymond.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini (0755659929).

No comments: