Saturday, December 5, 2015

Kwenye Gazeti La Jana Sweden; Magufuli Atajwa Kuwachonganisha Marais Wenzake Na Wapiga Kura Wao!

Ndugu zangu, 
Dagens Nyheter ni gazeti kubwa kushinda yote nchini Sweden, ndio ' Daily News' lao kwa maana ya jina la gazeti.

Katika toleo lake la jana Desemba 4, habari za John Magufuli zimepamba pia gazeti hilo. Amemwagiwa sifa, na ikaandikwa pia, kuwa Magufuli amewaweka katika wakati mgumu marais wenzake wa nchi jirani kwa vile wapiga kura wao wameonyesha wivu wao kwa Watanzania kupata Rais wa aina ya Magufuli.
Hata hivyo, kwenye gazeti hilo, imeandikwa pia, kuwa hata kabla ya kuingia milango ya Ikulu, Magufuli tayari ameshajipatia maadui wakiwamo wa ndani ya chama chake kwa hatua zake anazozichukua, hususan za kubana matumizi ya Serikali.
Hapa chini ni kipande cha habari za gazeti hilo na link ya habari nzima kwa lugha ya Kisweden. ( Picha iliyotumika gazetini humo ni ya Mpiga picha Halfan Said, ana malipo yake mazuri tu, akiyadai!)
"DAR ES SALAAM. Den nyvalde presidenten John Magufuli hann knappt flytta in i Tanzanias presidentpalats innan han fick sina första fiender – medlemmarna i det egna partiet CCM" link http://www.dn.se/…/president-skaffar-fiender-nar-han-later…/

Maggid Mjengwa,
0754 678 252

No comments: