Monday, February 29, 2016

DK.KIGWANGALLA AHIMIZA JAMII KUWA NA UTAMADUNI WA KUPIMA AFYA

Tazama MO TV Online, kuona video ya tukio hapa:
Imewekwa na Andrew Chale,modewjiblog
dk hkNaibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akitoa hutuba fupi wakati wa tukio hilo la kambi maalum ya matibabu ya bure kwa wananchi wote iliyoandaliwa na Care Foundation kwa kushirikiana na wadau wengine akiwemo Mbunge wa jimbo la Ilala, Mh. Mussa Hazan Zungu.

yiTukio likiendelea
DK KIGWANGALLA 65Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla akiwa katika meza ya kupima afya ya mwili ikiwemo magonjwa yasio ambukiza kama vile Magonjwa ya moyo, sukari, shinikizo la damu na mengine mengi katika zoezi linaliendelea katika viwanja vya Bustani ya jiji iliyopo mkabara na Ukumbi wa Karimjee.
Dk. KigwangallaNaibu Waziri wa Afya. Dk.Kigwangalla akiwa katika vipumo hivyo..
DKMbunge wa Ilala, Mh. Mussa Hazani Zungu, akipima afya katika zoezi hilo..
TIBA 3Dk. Efrahim Mika Zaky wa Msimbazi Eyes Vision Center, (kushoto) akimpima macho mmoja wa wananchi waliojitokeza katika zoezi hilo linaloendelea leo jijini Dar es Salaam katika viwanja vya Bustani ya jiji, mkabara na Ukumbi wa Karimjee.
TIBAUchunguzi wa macho ukiendelea..
TIBA3
Dk. Efrahim Mika Zaky wa masuala ya macho, akimpima macho Naibu Waziri wa Afya, Dk. Kigwangalla wakati wa zoezi hilo..
TIBQ667Naibu Waziri wa Afya Dk. Kigwangalla akiwa katika kupima macho kwenye kambi maalum ya kutoa huduma za matibabu ya bure yaliyoandaliwa na Care Foundation na wadau wengine katika viwanja vya Bustani ya Jiji, Posta Jijini Dar es Salaam.
TIBA222Naibu Waziri Dk.Kigwangalla akiwa katika moja ya sehemu ya kutolea dawa na miwani kwa watu watakaobainika kuwa na matatizo katika macho..
DK KIGWANGALLA 685Naibu Waziri akipokea ua maalum kama ishara ya kukaribishwa katika ufunguzi huo wa kambi maalum ya matibabu ya bure yaliyoandaliwa na CARE Foundation na wadau wengine akiwemo Mbunge wa jimbo la Ilala, Mussa Hazzan Zungu.(Picha zote na Andrew Chale, modewjiblog/Mo tv).

Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla amehimiza Jamii kuwa na utaratibu wa kupima afya mara kwa mara katika hali ya kubaini matatizo yanayowakabili ilikuchukua hatua ikiwemo kupata tiba mapema
Dk. Kigwangalla ametoa kauli hiyo mapema leo Februari 28.2016, jijini Dar es Salaam, wakati alipokuwa mgeni rasmi katika kambi maalum ya kupima afya bure kwa wananchi mbalimbali wakiwemo wa Jimbo la Ilala kwa kuandaliwa na Care Foundation na wadau wengine wa afya ikiwemo Hospitali ya Ebrahim Haji Chartable Health Centre ambao wanasimamia kutoa huduma za matibabu kwa kushirikiana na taasisi zingine.
Akitoa hutuba yake fupi, kwa wananchi mbalimbali walifika katika tukio hilo la kupatiwa matibabu hayo ya bure, Naibu Waziri, Dk. Kigwangalla amesema Jamii wanatakiwa kuwa na maisha yenye afya hivyo zoezi la kupima afya mara kwa mara ni bora zaidi kaika kuimalisha afya ya mwili.
“Wananchi wapo na wakati mwingi wakifanya shughuli zingine na hata muda kupima afya inakuwa ngumu. Kukinga ni bora Zaidi kuliko tiba. Zoezi hili litasaidia sana wananchi wengi na tunaomba muendelee na maeneo yote ya nchi yetu.” Ameeleza Dk.Kigwangalla.
Aidha, Dk. Kigwangalla amempongeza Mbunge wa Jimbo la Ilala, Mussa Hazan Zungu kwa kuwezesha kuandaa zoezi hilo kwa kushirikiana na wadau hao kwani ni mfano bora wa kuigwa na wabunge wengine pindi wapatapo nafasi ya kutumikia jamii iliyowachagua.
Pia katika zoezi hilo, Mbune wa jimbo la Ilala, Mh. Mussa Zungu na Naibu Waziri Dk. Kigwangalla walipata wasaha wa kupima afya zao pamoja na kutembelea maeneo ya kutolea huduma na kushuhudia namna huduma zinavyotolewa kwa wananchi.
Kambi hiyo ya matibabu, inatoa matibabu hayo bure kwa wananchi wote wanaofika hapo ambapo pia mbali na matibabu wanatoa huduma ya dawa huku wakitoa pia mawani kwa watu wenye matatizo ya macho. Watu mbalimbali wamekaribishwa kupatiwa matibabu hayo ambayo pia yanatolewa na madaktari bingwa wa magonjwa husika.

No comments: