Friday, February 26, 2016

MWANAHABARI SULEIMAN MSUYA WA GAZETI LA JAMBO LEO AACHANA NA UKAPERA

 Mwanahabari Suleiman Msuya wa Gazeti la Jambo Leo akitafakari jinsi atakavyoyaanza maisha ya ndoa baada ya kufunga ndoa na Shamim Rabim nyumbani kwa bibi harusi Jet Lumo jijini Dar es Salaam leo mchana.
 Mke wa Mwanahabari, Suleiman Msuya, Shamim Rabim akiwa katika pozi.
 Suleiman Msuta akimbusu mke wake.
 Ndugu, jamaa na marafiki wa Msuya wakiwasili ukweni kuoa.
 Msuya na mpambe wake wakiwa katika gari.
 Ndugu na Jamaa wa Msuya wakipunga upepo wakati wakisubiri ndoa kufungwa.
 Wakina mama wakiserebuka katika ndoa hiyo.
 Bibi harusi akipambwa.
 Wageni waalikwa wakishuhudia wakati ndoa ikifungwa.
 Sheikh Nurdin Ali (katikati), akifungisha ndoa hiyo. Kulia ni Bwana harusi Suleiman Msuya na kushoto ni Kaka yake bibi harusi Habib Hashim.
 Sheikh Nurdin Ali akitoa mawaidha baada ya kufungisha 
ndoa hiyo.
 Ubwabwa ukiliwa baada ya kufungwa kwa ndoa hiyo.
 Bibi harusi akitia saini kwenye hati ya ndoa.
Bwana harusi Suleiman Msuya akiwa amemshika kichwani mke wake  ni kama anasema "Wewe ndiye mke wangu wa kufa na kuzikana na chochote nitakacho kuomba usininyime"

No comments: