Tuesday, March 1, 2016

TIGO HALF MARATHONI" YAVUNJA REKODI YA IDADI YA WASHIRIKI

Washiriki zaidi ya 4000 wakiwa wamejitikeza kushiriki mbio za "Tigo Half Marathoni " km 21 ikiwa ni rekodi mpya tangu kuanza kwa mbio za Kilimanjaro Marathoni.

Raia wa Kigeni wakipiga serfie kabla ya kuanza mbio za Tigo Half Marathoni kwa wakimbiaji wa mbio za Km 21.
Wanariadha waloifanya vizuri katika mbio za Igombe Marathoni za mkoani Tabora waliodhaminiwa na kampuni ya Tigo wakiwa katika mavazi maalum toka kwa mdhamini wao.
Washiriki wa Mbio za Km 21 za Tigo Half Marathon wakianza mbio nje ya geti la chuo kikuu cha Ushirika mjini Moshi.
Mrembo wa Tanzania mwaka 2004 Faraja Kota pia laikuwa ni miongoni mwa wakimbiaji walioshiriki mbio za Km 21.
Wakimbiaji wa timu ya Taifa ya riadha ya Tanzania walioshiriki mbio za Km 21 wakifarijiana,wanariadha hao walitumia mbio hizo kama sehemu ya mazoezi
Rais wa Shirikisho la Riadha Tanzania RT Anthony Mtaka akizungumza jambo na msatahiki Meya wa manispaa ya Moshi,Raymond Mboya,katikati ni mkuu wa wilaya ya Moshi,Novatus Makunga.
Mshindi wa kwanza wa mbio za Km 21 ,Grace Kimanzi raia wa Kenya akimaliza mbio katika uwanja wa c huo kikuu cha Ushirika.
Mshindi wa kwanza wa  mbio za Km 21 upande wa wanawake Grace Kimanzi  akitoka katika eneo la kukimbilia mara baada ya kumaliza mbio hizo,
Mshindi wa tatu  katika mbio za Kilimanjaro Marathoni ,Km 21 upande wa wanawake Failuna Abdi akipewa msaada na mkurugenzi wa mbio hizo John Bayo na baadae kuwekwa katika kiti cha kubebea watu wenye matatizo muda mfupi baada ya kualiza mbio hizo .
Washiriki wa mbio za Km 21 upande wa wanaake ,nafasi ya kwanza hadi ya 10 wakiwa katika jukwaa kungojea kupokea zawadi toka kwa mgeni rasmi.
Mgeni rasmi katika mbio hizo Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo Nape Nnauye akipeana mkono na mmoja wa washiriki wa Mbio hizo .
Katibu tawala mkoa wa Kilimanjaro,Severine Kahitwa akipeana mkono na mwanariadha wa Tanzania ,Fabian wakati wa zoezi la utoaji zawadi kwa washindi.
 Waziri wa Habari ,Utamaduni ,Sanaa na Michezo Nape Nnauye akikabidhi mfano wa hundi kwa washindi wa mbio hizo.
Washiriki wa mbio hizo wa nafasi ya kwanza hadi ya kumi wakiwa katika picha yi a pamoja na mgeni rasmi Waziri Nape Nnauye.
Waziri Nape Nnauye akitoa mfano wa hundi kwa washindi wa mbio hizo upande wa wanawake.
Mkurugenzi wa kampuni ya Tigo George Lugata akibadilishana mawazo na mmoja wa maofisa wa kampuni hiyo walipokutana uwanjani hapo.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro wa zamani,Mohamed Babu (kushoto) akizungumza jambo na mkurugenzi wa kampuni ya utalii ya Uhuru Expedition ,Joseph Kitani kabla ya kuanza kwa mbio hizo.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kasakazini.

No comments: