Wednesday, April 19, 2017

VIJANA WAUZA TAMTHILIA NA FILAMU ZA NJE WAANDAMANA KUIOMBA SERIKALI KUWARUHUSU WAUZE CD HIZO.


 Vijana ambao ni machinga wanaouza CD za Tamthilia na filamu za kizungu,Kihindi na za kutoka bara la asia  wakionesha cd hizo juu wakati wa mkutano na waandishi wa habari mtaa wa Aggrey eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo.(PICHA ZOTE NA ELISA SHUNDA)



 Muuza CD za Tamthilia na Filamu za nje,Marick Omary,akizungumza na waandishi wa habari katika Mtaa wa Aggrey eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo kuhusu kuiomba serikali kuwasaidia na kutowafungia vijana hao kuuza cd hizo kwa kuwa zinawapatia ridhiki ya kihalali tofauti na kufanya kazi zingine zisizo za kihalali.



 Muuza CD za Tamthilia na Filamu za nje,Andhuhuri Mohamedy,akichangia hoja kwa waandishi wa habari katika Mtaa wa Aggrey eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo kuhusu kuiomba serikali kuwaruhusu wafanyabiashara hao (Machinga) kuendelea na biashara hizo ambayo inawawezesha kulisha na kusaidia familia zao na kusema kama kuna maboresho ni bora serikali wakae kwa pamoja wazungumze siyo kupiga marufuku watakufa njaa.


 Muuza CD za Tamthilia na Filamu za nje,Halima Bakari,akizungumza kwa majonzi kuhusu kuiomba serikali kuweka utaratibu mzuri wa kuwaruhusu wafanyabiashara hao waendelee na uuzaji wa tamthilia na filamu za nje kuendelea kuuza kwa kuwa kuna wanawake wengi wameachana na suala la kuuza miili yao (Biashara ya Ngono) ambayo siyo halali wakajiingiza kuuza cd hizo ili wapate kipato cha kihalali kwa hiyo kuwafungia ni kuwarudisha nyuma kifikra.

 Baadhi ya wauzaji wa CD hizo waliokusanyika katika eneo hilo la Mtaa wa Aggrey eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo.


  Vijana ambao ni machinga wanaouza CD za Tamthilia na filamu za kizungu,Kihindi na za kutoka bara la asia wakionesha cd hizo juu wakati wa mkutano na waandishi wa habari mtaa wa Aggrey eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya wauzaji wa CD hizo waliokusanyika katika eneo hilo la Mtaa wa Aggrey eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo.

Baadhi ya maduka yaliyokuwa yakiuza CD za Tamthilia na filamu za kizungu,Kihindi na za kutoka bara la asia yakiwa yamefungwa kama yanavyoonekana katika Mtaa wa Aggrey eneo la Kariakoo jijini Dar es Salaam leo.
Imeandaliwa na mtandao wa www.elisashunda.blogspot.com/ Email:elisashunda@gmail.com /0719976633

NA ELISA SHUNDA,DAR
WAFANYABIASHARA wadogo wadogo ‘Machinga’ wanaouza filamu za kigeni wameandamana wakiomba kukutana na Rais John Magufuli ili kusikilizwa juu ya kupigwa marufuku kuuza filamu hizo hapa nchini.
Marufuku hiyo ilitolewa na Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo Harrison Mwakyembe, siku chache baada ya kuteuliwa katika nafasi hiyo mara baada ya kukutana na waigizaji wa ndani ambapo walieleza malalamiko yao juu ya filamu za nje kuharibu soko la kazi zao.
Wamachinga hao waliandamana jijini Dar es Salaam jana katika soko la Kariakoo katika Mtaa wa Aggrey ambako  kuna maduka wanakoenda kuchukua mikanda ya filamu za nje ‘CD’ na kusambaza mtaani huku wengine wakiweka katika vibanda kwa ajili ya kukodishia wateja wanaohitaji.
Wakizungumza na waandishi wa habari wafanyabiashara hao walisema Waziri huyo alitoa maamuzi hayo kwa kusikiliza upande mmoja ambao ni walalamikaji bila kuwapa nafasi ya kujieleza jambo ambalo wanalipinga.
Mmoja wa machinga hao Hanzuruni Mohamed alisema aliyekuwa Waziri katika Wizara hiyo Nape Nnauye alikuwa akisikiliza pande zote kabla kufanya maamuzi na kuongeza kwamba walishakaa vikao mbalimbali kwa ajili kutafuta mwafaka lakini Mwakyembe ameshindwa kufanya hivyo.
“Nape alikuwa anafanya maamuzi kwa kufuata pande zote mbili, huyu katoa siku 10 tu kufungia filamu za nje, hapa kuna vijana zaidi 1000 fikiria tutafanya kazi gani, tukiwa panya road nchi itakuwaje tunakuomba Rais uliangalie hili sisi ni vijana wako” alisema Mohamed.
Naye Halima Bakari alisema kufungwa kwa biashara hiyo kutamwathiri maisha yake kwani alikuwa akitegemea biashara ya filamu kuendesha maisha yake na kuhudumia familia yake na kusema awali alikuwa akifanya biashara ya kujiuza biashara aliyoiacha baada ya kujiingiza katika soko la filamu.
“Mwanzo nilikuwa najiuza nategemewa na mdogo wangu yatima, sasa hivi mabosi wamefunga maduka wakisema wanaogopa kufungwa kutokana na kauli ya Waziri, sasa hivi hatuna ajira nyingine mimi ni binti bila kutoa penzi sipati kazi na kauli mbiu ni Hapa kazi tu, Rais tusaidie tutaenda wapi” alisema Bakari.
Kwa uapnde wake Maliky Ally alisema wametii kuacha kuuza filamu lakini wamaomba kusikilizwa upya ili kuwe na makubaliano yatakayohusisha pande zote kwasababu hiyo ni ajira wanaoitegemea kuendesha maisha yao.

No comments: