Tuesday, May 9, 2017

Mwakilishi na Mbunge wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Wakabidhi Vifaa Kwa Shughuli za Kijamii Jimboni.

Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Simai Mohammed Said akizungumza nas Wananchi wa Shehia tatu za Bungi, Ubago na Tunguu wakati wa kukabidhi vifaa kwa ajili ya shehia hizo tatu kwa matumizi ya Kijamii wakati wa shida na raha, Vifaa walivyokabidi majiko ya gesi 3, sinia 800  mitungi ya gesi 6 na mabusati. kwa ajili ya matumizi yao katika shughuli za kijamii, hafla hiyo ya makabidhiani imefanyika katika Tawi la CCM Tunguu Wilaya ya Kati Unguja. Na kuhudhuriwa na Viongozi wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja. 
Mbunge wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe. Khalifa Salim Suleiman akizungumza na wananchi w
a jimbo lake wakati wa hafla ya kukabidhi vifaa kwa ajili ya matumizi ya shughuli za kijamii katika jimbo lao ikiwa ni kutimiza ahadi kwa wananchi wa jimbo lao walioitowa wakati wa kampeni ya uchaguzi.hafla hiyo imefanyika katika tawi la CCMTunguu Wilaya ya Kati Unguja.
Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu wakikabidhi vifaa mbalimbali waliohidi kwa wananchi wa jimbo lao wakikabidhi vifaa hivyo kwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kusini Unguja Ndg Ramadhan Abdallah na Uongozi wa jimbo hilo, hafla hiyo imefanyika katika ukumbi wa Tawi la CCM Tunguu Unguja. wakikabidhi mabusati na sinia.
Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar wakikabidhi majiko ya gesi kwa ajili ya shia tatu kila shehia imepata jiko moja na mitungi ya gesi miwili. na sinia 200, kwa ajili ya matumizi ya kijamii katika shehia zao.Hafla hiyo ya makabidhiano imefanyika katika Tawi la CCM Tunguu Unguja. 
Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu wakikabidhi sufuria kwa Uongozi wa Jimbo kwa ajili ya matumizi ya Shehia za Jimbo hilo tatu kila shehia imepata sufuria mbili kubwa.
Mbunge na Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu wakikabidhi mitungi ya gesi kwa Uongozi wa Jimbo kwa ajili ya matumizi ya Shehia za Jimbo hilo tatu kila shehia imepata mitungi miwili ya gesi mikubwa kwa ajili ya matumizi ya shughuli za kijamii katika jimbo lao zilizotolewa na viongozi hao..
Mwenyekiti wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mzee Khatib Ramadhani akitowa shukrani kwa Mwakilishi na Mbunge kwa msaada wao huo kwa ajili ya kuwajali wananchi wa jimbo lao kwa msaada huo na kuahidi kuutumia kwa malengo yaliokusudiwa katika shughuli za kijamii katika shehia husika za jimbo hilo. 
Mwakilishi wa Jimbo la Tunguu Zanzibar akizungumza na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali dhamira wa msaada huo kwa wananchi wa jimbo lao kuweza kuwasaidia katika matumizi yao ya shughuli za kijamii zinazotokea kwa wananchi hao ili kuweza kuvitumia kupunguza gharama za kukodi vifaa hivyo.

Imetayarishwa na OthmanMapara,zanzinews.com.
email. othmanmaulid@gmail.com.

No comments: