Tuesday, July 4, 2017

MAONESHO YA SABASABA 2017; WAAJIRI NA WAFANYAKAZI WAJITOKEZA KWA WINGI BANDA LA MFUKO WA FIDIA KWA WAFANYAKAZI (WCF) KUPATA ELIMU ZAIDI KUHUSU MFUKO HUO

 Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCD), Dkt. Abdulsalaam Omar, akimfafanulia mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo lililoko kwenye hema kubwa la Jakaya Kikwete, kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam 2017, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kuhusu hatua ambazo mfanyakazi anapaswa kuchukua baada ya kupata maradhi au kuumia wakati akitekeleza majukumu yake ya kikazi kabla ya kupatiwa Fidia na WCF.
Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), Bw. Masha Mshomba, akizungumza wakati akiwa kwenye banda
la Mfuko huo
NA K-VIS BLOG/Khalfan Said
WAAJIRI na wafanyakazi wamejitokeza kwa wingi kupata elimu kuhusu kazi za Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), kwenye banda la Mfuko huo lililoko kwenye hema kubwa la Jakaya Kikwete kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kunakofanyika maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam.
Maonesho hayo ya kila mwaka huwaleta pamoja wafanyabiashara ya makampuni makubwa ya kimataifa kutoka nje na dnani ya nchi, lakini pia kunakuwepo na mkusanyiko mkubwa wa wafanyakazi wa umma na binafsi wanaotoa huduma mbalimbali kwa watu wanofika kutembeela maonesho hayo.
Mfuko wa Fidia kwa wWafanyakazi, (WCF) imetumia fursa hiyo kutoa elimu kwa waajiri na wafanyakazi ambao walifika kwenye banda la Mfuko huo na kupatiwa maelezo ya kina kuhusu kazi za Mfuko kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wake Bw. Masha Mshomba, wakurugenzi na wakuu wa idara pia.
“WCF ni Mfuko wa Hifadhi ya Jamii ulioanzishwa kwa mujibu wa sheria namba 5 ya Fidia kwa Wafanyakazi kifungu namba 263 ya mwaka 2015.” Bw. Mshomba aliyasema hayo akiwa kwenye banda hilo ambapo waajiri na wafanyakazi walifika kupata elimu zaidi ya kuhusu Mfuko huo.
Bw. Mshomba aliendelea kufafanua kuwa, kwa mujibu wa sheria iliyoanzasha Mfuko huo, tofauti na Mifuko mingine ya Hifadhio ya Jamii, ambapo mwajiri na mfanyakazi hutoa michango ya kila mwezi, kwa upande wa WCF, ni mwajiri pekee ndiye anawajipika kumchangia mfanyakazi wake kila mwezi na mfanyakazi hawajibiki kutoa mchango wowote. Aidha Bw. Mshomba alieleza kuwa, dhumuni kuu la kuanzishwa kwa Mfuko huo ni kutoa Mafao ya kutosha na stahili  kwa Mfanyakazi aliyepatwa na maradhi au majeraha yaliyotokana na kazi anazozifanya Mfanyakazi huyo.
“Na ifahamike kwamba, Mafao haya analipwa Mfanyaakzi aliyepatwa na madhara hayo imma wakati akiwa kazini au madhara hayo yanapojitokeza hata baada ya kuacha kazi ilimradi madaktari wathibitishe kuwa madhara hayo yametokana na kazi alizokuwa akifanya au kifo ambapo watalipwa wategemezi wake.” Alifafanua Bw. Mshomba.
Miongoni mwa Mafao ambayo Mfuko utatoa kwa Mfanyakazi aliyepatwa na maradhi au majeraha ni pamoja na fao la matibabu, Fidia kwa ulemavu wa muda, (Temporary disability), Msaada wa uangalizi wa kudumu, Msaada wa mazishi kwa mfanyakazi aliyefariki kutokana na kazi aifanyayo, lakini pia Fidia kwa wategemezi wa marehemu aliyepatwa na umauti akiwa kazini.
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini wa Mfuko huo, Dkt. Abdulsalaam Omar, alisema Mfanyakazi aliyeumia kutokana na kazi aifanyayo au maradhi yaliyosababishwa na kazi aifanyayo, Mfuko utagharimia huduma za gari la kubeba wagonjwa, kumuona daktari, upasuaji, pamoja na matibabu kwa ujumla baada ya kufanyiwa tathmini na madaktari ambao tayari wamepatiwa mafunzo ya namna ya kufanya tathmini kwa Mfanyakazi aliyeumia au kupata maradhi kutokana na kazi anayoifanya.
Naye Mkuu wa kitengo cha Mawasilianonna Uhusiano wa Mfuko huo, Bi. Laura Kunenge, aliwahimiza waajiri na wafanyakazi kutembelea banda hilo ili kupata elimu lakini pia kujua haki za Mfanyakazi na mwajiri pia.
“Mfulo huu unatoa nafuu sio tu unasaidia Mfanyakazi kulipwa Fidia Stahili bali pia unatoa nafuu kwa mwajiri kwani ghara hizo zitasimamiwa na WCF na sio Mwajiri. “Ndio maana tunawahizimiza waajiri kote nchini kutoka sekta binafsi na umma, kutoa michango ya kila mwezi kama sheria inavyotaka.” Alisema Bi. Laura.
 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Mfuko huo, Bi. Laura Kunenge, (kulia), akizungumza na Posta Masta Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Posta Tanzania, Bw. Deo Kwiyukwa, wakati alipotembelea banda hilo.
  Mkurugenzi wa Huduma za Tiba na Tathmini wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCD), Dkt. Abdulsalaam Omar, akimfafanulia mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo lililoko kwenye hema kubwa la Jakaya Kikwete, kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam 2017, barabara ya Kilwa jijini Dar es Salaam kuhusu hatua ambazo mfanyakazi anapaswa kuchukua baada ya kupata maradhi au kuumia wakati akitekeleza majukumu yake ya kikazi kabla ya kupatiwa Fidia na WCF.
 Wafanyakazi hawa wakipatiwa maelezo mbalimbali yahusuyo huduma zitolewazo na Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, (WCF), walipotembelea banda la Mfuko huo kwenye maonesho ya 41 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam
 Afisa Uhsuiano Mwandamizi wa WCF, Bw. Sebera Fulgence, (wapili kushoto), akimpatia maelezo mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo.
 Mkurugenzi Mkuu wa WCF, Bw. Masha Mshomba, (kushoto), akizunguzma jambo na Mkurugenzi wa Mawasiliano na Elimu wa Mamlaka ya Udhibiti Hifadhi ya Jamii, (SSRA), Bi. Saraha Kibonde Msika, ambaye alitembelea banda hilo. SSRA imeweka maafsia wake kila banda linalotoa huduma ya hifadhi ya jamii kwenye maonesho ya mwaka huu.
 Afisa wa WCF, (kulia), akimuhudumia mwananchi huyu aliyefika kwenye banda la WCF
  Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Mfuko huo, Bi. Laura Kunenge, (kushoto), akimsikilzia mwananchi huyu aliyefika kwenye banda la Mfuko huo.

 Afisa wa WCF, Bi.Inocencia William, (kulia), akimpatia maelezo yenye kuhusu huduma za WCF mwananchi huyu aliyefika kujua nini hasa kazi ya Mfuko huo na faida zake kwa Mfanyakazi na Mwajiri
 Bw. Mshomba, (kulia), akiongongozana na Bi Laura, (kushoto) wakati akiwasuli kwenye banda hilo ili kuwahudumia wananchi. Kushoto ni Sebera Fulgence, Afisa Uhusiano mwandamizi wa Mfuko.

No comments: