Monday, May 11, 2015

“NIPO STUDIO” YA JENNIFER MGENDI KUACHIWA

Mtayarishaji wa filamu na mwimbaji wa siku nyingi Jennifer Mgendi anakusudia kuachia filamu yake ya “Nipo Studio” mapema wiki hii. Akiongea na blogu hii Jennifer amesema filamu hiyo imekamilika kwa kila kitu na itaingia sokoni wiki hii ikiwa imewashirikisha wasanii mbalimbali akiwamo shosti wake wa siku nyingi Bahati Bukuku, Bibi Esta, Hassan Mbangwa, Gwamaka Kametta na wengine wengi.

Jennifer amesema filamu hii inazungumzia changamoto mbalimbali anazokutana nazo Bibi Esta pale anapokuwa na ndoto ya kuwa mwimbaji huku umri na kipato vikiwa kikwazo kwake.


Wakati huo huo Jennifer  amesema maandalizi ya tamasha lake la uzinduzi wa video ya Wema ni akiba yanaendelea vizuri na tamasha hilo litafanyika kama ilivyopangwa tarehe 28 Juni katika kanisa la DCT Tabata Shule huku Mgeni Rasmi akitarajiwa kuwa Askofu Mkuu wa kanisa la Tanzania Assemblies of God , Dr. Barnabas Mtokambali.

No comments: