Tuesday, February 9, 2010

Vijue vyakula vya mgonjwa wa presha


Hakuna kitu kibaya kwa mgonjwa kama kula vyakula ambavyo huongeza tatizo alilonalo bila kujijua. Kwa kuwa tunaamini kwamba, jinsi tulivyo tunatokana na tunavyokula, basi kupona au kuendelea kuugua nako kutategemea sana vyakula tutakavyokula.

Vyakula viko vya aina mbalimbali na kila kimoja kina umuhimu wake katika mwili wa binadamu. Lakini mtu ukishakuwa mgonjwa, hasa wa maradhi sugu kama vile presha, kisukari, ukimwi, n.k, ni lazima ujue vyakula gani unapaswa kula na vyakula gani unapaswa kuviepuka.

Leo tunaangalia vyakula anavyopaswa kuvila ama kuviepuka mgonjwa wa shinikizo la juu la damu (High Blood Pressure). Kama inavyojulikana, maradhi haya hutokana na staili ya maisha anayoishi mtu, vivyo hivyo hata udhibiti wake utategemea na atakavyoishi.

NYAMA NA MAYAI
Nyama na mayai ni adui mkubwa wa mgonjwa wa presha. Ni wagonjwa wangapi wanafahamu kwamba vyakula hivi ni hatari kwa maisha yao na wakaacha kabisa kuvitumia? Naamini ni wachache sana wanaolifahamu hili na kulizingatia, hasa ukizingatia utamu wa vyakula hivyo.

Inaelezwa kuwa katika vyakula ambavyo mgonjwa wa presha akivila huchangia kupandisha presha ni mayai na nyama, hasa ile itokanayo na ng’ombe, mbuzi, nguruwe na nyingine za jamii hiyo.

ZINGATIA VYAKULA HIVI
Ukisha kuwa mgonjwa wa presha, ulaji wa vyakula vitokanavyo na nafaka halisi, matunda na mboga za majani, linakuwa suala la lazima na siyo hiyari. Mgonjwa wa presha anashauriwa kula zaidi vyakula hivyo na kupunguza ulaji wa vyakula vyenye protini nyingi, ikiwemo nyama kama ilivyoolezwa awali.

Katika orodha ndefu ya matunda anayopaswa mgonjwa kula na kupata nafuu, ni pamoja na hii ifutayao, ambayo huweza kutumika pia kama tiba, kwani matunda haya yameonekana kuwa na virutubisho vingi zaidi vinavyoweza kudhibiti presha:

Vitunguu saumu
Kula vitunguu saumu kwa wingi, hutoa nafuu kubwa kwa mgonjwa. Unaweza kula punje mbili hadi tatu kwa siku na kuchanganya kwenye mboga pia.
Limau
Pia penda kula limau mara kwa mara, nalo ni miongoni mwa matunda yanayotoa nafuu kwa mgonjwa wa presha. Limau lina Vitamin P ambayo utaipata kwa kunywa juisi yake au nyama na maganda yake.

Zabibu mbivu
Zabibu nazo zimeorodheshwa miongoni mwa matunda anayotakiwa kula mgonjwa wa presha ili kupata nafuu, nayo yana vitamin P ambayo huzuia kuziba kwa mishipa ya damu.

Tikiti maji
Tikitimaji nalo ni miongoni mwa matunda anayopaswa kula mgonjwa wa presha. Halikadhalika, mbegu za tikiti maji zinaweza kutengenezwa na kuliwa kama dawa inayoweza kumpa nafuu kubwa mgonjwa. Kausha mbegu zake, kisha zikaange, ziliwe mara kwa mara kama karanga.

Mchele
Mchele una kiwango kidogo cha ‘fat’ na pia una kiwango kidogo cha ‘kolestrol’, hivyo kukifanya kuwa chakula bora kwa mgonjwa wa presha. Hivyo wali ni sawa kuliwa na mgonjwa wa presha, hasa ukipata ule mchele usioondolewa virutubisho vyake (brown rice).

Viazi vitamu
Viazi vitamu, hasa vile vya kupika na maganda yake, vinafaa sana kuliwa na mgonjwa wa presha kwani vina madini mengi ya ‘potasiamu’ na havina madini chumvi.

Juisi ya mboga majani
Ulaji wa mchanganyiko wa juisi ya mboga, hasa karoti na mchicha (spinach) ni mzuri sana kwa mgonjwa wa presha, huweza kutumika pia kama tiba. Kunywa glasi moja kutwa mara mbili au tatu.

Kwa kuzingatia ulaji wa vyakula vilivyoainishwa hapo juu na kufanya mazoezi mara kwa mara, mgonjwa wa presha anaweza asisumbuliwe kabisa na tatizo hilo na kujihisi kupona hata bila kutumia dawa. Hata hivyo, hilo linawezekana tu iwapo utajitambua mapema na kuanza kuchukua hatua za ulaji sahihi wa vyakula sasa na siyo baadaye!

Monday, February 8, 2010

JIHADHARINI NA MARAFIKI WA KWENYE FACEBOOK!


A reminder to those who are on facebook not to give too much of your personal details!!
The girl in the picture posted the nice looking pictures on Facebook and of course she got like a million friend request she accepted all of them. One of the guys started asking her to meet up and I guess to have sex she deny him but since it was Facebook she had put all her info there too so he had her address phone number etc etc so he showed up at her place and then the last 4 pictures tell the story of what happen.....!!!!


WIKIENDA SHOWBIZ!

Fella na briefcase la mwaka wa fedha 2010
Meneja mshika MIC wa TMK Wanaume Family, Said Fella ‘Mkubwa’ ametua briefcase lenye maelezo kuhusu programu za kazi na fedha kuhusu yeye na kundi lake kwa mwaka wa fedha 2010-2011. Mkubwa alidondosha program hiyo kwa Abby Cool & MC George over the weekend ambayo tunaichambua kama ifuatavyo:

1.Kumtoa Said Juma ‘Chege’ na albamu yake, inayoitwa Karibu Kiumeni. 2.Ipo albamu ya kundi, inayoitwa Wanaume Kazini. 3.Analipa gharama za albamu ya qaswida, ya Madrasat Salama Islamiah, iliyopo Mbagala. 4.Atawatoa Amani James Temba a.k.a Mheshimiwa na Chege katika mradi wa pamoja, albamu yao inaitwa Vita Mbele. 5.Amefungua studio ya kurekodi Audio ambayo inaitwa Poteza Records. 6.Mwisho anaelekeza nguvu kwa underground, mwaka huu amejiwekea mkakati wa kumtoa mmoja wa kiume.
*************************************************


Kifo cha Bongo Fleva
Yap, ni mjadala kuhusu kifo cha kibudu cha Bongo Fleva. Huko nyuma tumepitia maeneo mbalimbali ambayo kwa maana moja au nyingine yamesababisha muziki huo ambao ulikuwa umeanza kung’ara, kubadili uelekeo na kushika njia ya kaburini.

Baada ya kugusa maeneo hayo, leo tunageukia studio za uchochoroni a.k.a studio uchwara, hizi kwa kiasi kikubwa zimesababisha Bongo Fleva ishike kasi kwenye njia ya kaburini.

Iko hivi, wakati watu wapo serious, wanafanya kazi za ukweli, kuna watu fulani kwa kufuata mkumbo, wakaona kumbe nao wanaweza kufanya biashara. Wakafungua studio na kuanza kutoa rekodi mbuzi.

Enzi zile anavuma Enrico na Sound Crafters, P. Funk na Bongo Records, Master Jay na MJ Production, Miika Mwamba na FM Studio, mara tukasikia Mbagala Charambe nako kuna studio. Heee!

Watu wakaona dili kwa sababu mzuka wa Bongo Fleva ulikuwa juu, watoto bila kujua quality ya muziki, wao wakawa wanalipa mkwanja, wanaingia chumba cha sindano, wanaingiza vocal baada ya nusu saa, mixing tayari anakabidhiwa mzigo kwenye CD.
Studio uchwara wakawa wanapata dili nyingi kwa sababu chaji yao haikuwa kubwa.

Wakati watu serious walitoa ngoma ikiwa na kiwango kwa shilingi 200,000 wakati huo, kule uchochoroni kuna track zilifanywa mpaka kwa wekundu watatu (30,000).

Tatizo kubwa likaja, washkaji baada ya kukabidhiwa CD, wakapeleka redioni. Zile redio serious zikagoma kucheza nyimbo hizo ambazo ni chafu katika quality ya muziki, lakini kule kwa ma-DJ na watangazaji njaa, ngoma zilichezwa na matokeo watu wakaanza kuchoka.

Zipo track mbovu masikioni, zilizorekodiwa ambazo ziliingizwa kwenye chati fulani fulani, kisa eti, msanii alikata mpunga kwa DJ au mtangazaji wa program husika. Taratibu muziki ukaanza kushuka thamani. Hao waliorekodi kwa kiwango duni, wakatengeneza albamu, wakampelekea mdosi ambaye hajui quality ya muziki, akaanza kuuza, matokeo yake akajaza nyimbo nyingi zisizokuwa na kiwango mtaani.

Kutokana na kuwa na kazi nyingi, mdosi akaanza kudengua, akipewa kazi na watu serious, anapanga bei ya chini. “Vevee iko kama hutaki kwenda bana, hapa ipo na kazi nyingi.”

Ikafikia kipindi, wasanii wakali wakabanwa, maprodyuza serious wakapungukiwa na kazi. Walikuwa wanafanya kazi usiku na mchana, lakini ikawa mchana ni miayo tu, wasanii hawaendi kurekodi.

Mtu ana Mic moja, kompyuta moja, mixer ya disko vumbi, keyboard ya bei chee kwa wamachinga wanaopitisha barabarani, eti naye anamiliki studio. Anarekodi. Ni wengi sana wameuroga muziki huu.
*******************************************************

Rocky City: Wasanii kukwea ‘level’ nyingine
Tabia ya wasanii wengi wa Rocky City a.k.a Zoo au ukipenda unaweza kuita Mwanza, kukimbilia Dar, imepata dawa! Abby Cool & MC George over the weekend inatonya kuwa pande hizo za Kamanda Jamal Rwambow, imefunguliwa bonge ya studio.

Studio hiyo ya audio, ina kiwango cha kimataifa, hivyo badala ya wasanii kukimbilia Dar au Nairobi kutafuta studio zenye ubora, wanaweza kufanya kazi ‘babkubwa’ Zoo na zikachezwa kwenye vituo vya redio vya kijanja.

Studio hiyo inakwenda kwa jina la ATP na inapatikana pande barabara ya Rufiji jijini humo, na Meneja wa Studio hiyo, Iku Mwakisambwe, alisema nasi kwamba lengo ni kupandisha kiwango cha wasanii wa Rocky City ili kikubalike kimataifa.

Mastaa ambao tayari wameingiza voko kwenye studio hiyo ni Dark Master, Geez Mabovu, Z- Anto, Bwana Misosi, Chelea Man na wengine. Hey, Jitaman, H. Baba, Fid Q, Hard Mad, Rado na wengine, mnaweza kufikiria kurudi nyumbani?

**************************

JenniferLove
Aanza ngono akiwa na miaka 14, ametoa uroda kwa njemba 24
Ebwana Dah! Staa wa muvi, Jennifer Love Hewitt ndiye anaye take cover kwenye safu hii na hapa inatajwa orodha ya njemba ambazo kwa nyakati tofauti amezikabidhi penzi lake.

Kwa mujibu wa ripoti ya tovuti inayodili na ishuz za uhusiano wa mastaa wa mbele kwenye eneo la nani kamrukia nani, Jennifer Love alianza kuchangamkia sanaa ya kitandani akiwa na umri miaka 14 tu. (Aliwahi sana).

Scott Bairstow ndiye kidume anayetajwa kuanza kuchangamka naye mwaka 1994 ambapo Jennifer alikuwa na umri wa miaka 14. Akaja Joey Lawrence ambaye alichangamsha damu kwa mwaka mmoja, 1995 – 96, akiwa na miaka 15.

Alipotoka kwa Joey, Jennifer kwa mtindo wa bandika bandua, alijiweka kwa Will Friedle ambapo penzi lao lilidumu kuanzia mwaka 1996 – 97 kabla kuamua kuutua mwili wake kwa Andrew Keegan, 1997.

Penzi la Jennifer na Andrew lilidumu kwa muda mfupi mno na baada ya kutoka kwake alihamishia majeshi kwa Carson Daly kuanzia mwaka 1997 – 99.

Hata hivyo, akiwa na Carson, Jennifer ‘alichiti’ na kumgea kidogo Jeff Timmons mwaka 1998. Mwaka 1999 alijipumzisha kwa muda kwa Diego Serrano kabla ya mwaka huo huo kutuliza mizuka kwa Rich Cronin ambaye alikaa naye mpaka mwaka 2001.

Kwa mara nyingine, Jennifer akiwa na Rich, mwaka 1999 ‘alimchiti’ na kumegana kisela na Wilmer Valderrama, pia mwaka 2000 kwa Alec Baldwin.

Aidha, mwaka 2000 huo huo, alianzisha uhusiano na Craig Bierko na kudumua naye mpaka mwaka 2001. Hii inamaana kuwa mbali na ‘kuchiti’ mara kwa mara kwa watu tofauti, pia kati ya kipindi cha mwaka 2000-01, Jennifer alikuwa na wanaume wawili permanent, Craig na Rich.

Mwaka 2001-02, Jennifer alijiweka kwa Patrick Wilson, pia mwaka 2001, hakuona soo kumpa penzi lake Enrique Iglesias, mwaka 2002, alimegana na Shaggy, mwaka huo huo akajikunja na John Mayer, na kuanzia mwaka 2002-03, alimchagua Paul Nicholls. Baada ya hapo, Jennifer akajiweka kwa John Cusack, hiyo ilikuwa ni mwaka 2003, mwaka huo huo akajikunja na Stephen Dorff, Kip Pardue, Antonio Sabato na Scott Austin ambaye walimwagana mwaka 2004.

Mwaka 2004, alijiweka kwa Will Estes, mwaka uliofuata, hapo unazungumziwa 2005, alikaa kwa Ross McCall ambaye walitosana mwaka 2009 na baada ya hapo akahamia kwa Jamie Kennedy ambaye yupo naye mpaka sasa.

Jennifer, alizaliwa Februari 21, 1979, Waco, Texas, Marekani, kwahiyo ana umri wa miaka 30.
*******************************************
compiled by mc george
for more news visit: www.globalpublisherstz.com





Sunday, February 7, 2010

UNATAKA KUJUA NOKIA YAKO NI FEKI AU ORIJINO?


Nokia - MOBILE-check if original or not
Would like to know if your mobile is original or not?!!
Press the following on your mobile *#06# and the-international mobile equipment identity number appears
Check the 7th and 8th numbers

1

2

3

4

5

6

7 th 8 th

9

10

11

12

13

14

15

IF the digit number Seven & Eight is 02 or 20 that mean it was assembled in the Emirates which is very Bad quality

IF the digit number Seven & Eight is 08 or 80 that means it was manufactured in Germany which is not bad

IF the digit number Seven & Eight is 01 or 10 that mean it's manufactured in Finland which is Good

IF the digit number Seven & Eight is 00 that means it was manufactured in original factory which is the best Mobile Quality ...

IF the digit number Seven & Eight is 13 that means it was assembled in
Azerbaijan which is very poor quality and potentially very dangerous to your health!!!

MATOKEO KIDATO CHA NNE 2009

Wanafunzi wa Marian Girls High School - Bagamoyo, ambao wametoa mwanafunzi bora Tanzania nzima mwaka huu!
KUPATA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE KWA SHULE ZOTE NCHINI TANZANIA, BONYEZA LINK HII:http://www.necta.go.tz/html_csee209/olevel.htm au nenda hapa: BARAZA LA MITIHANI

Friday, February 5, 2010

IJUMAA SHOWBIZ


Ikiwa imekirudisha kwa kasi kile kipengele cha waliyopotea ‘Mwana Mpotevu’, mwishoni mwa wiki iliyopita ShowBiz ilienda hewani pande za Mwanza na kupiga stori na binti aliyewahi kufanya maajabu kunako miaka ya 2000 kupitia game ya muziki wa kizazi kipya huku akiwa na umri mdogo.

Anaitwa Pendo Farida Koshuma a.k.a Farida, kama humkumbuki vizuri, ukitajiwa majina ya ngoma kama Upendo wa mama, Pesa na nyingine, utagundua kwamba binti huyo kitambo alipotea tangu alipodondosha albamu yenye jina la ‘Upendo kwa mama’.

Akipiga stori na ShowBiz, Farida ambaye hivi sasa anamiliki age ya miaka 24 amesema kuwa, alisepa kwenye game baada ya kubanwa na masomo, lakini sasa anarudi upya akiwa ni mama wa mtoto mmoja wa miezi 8 na mwenye jina la Dominatha Kindole, huku akiwa ametia sauti yake isiyochuja kunako ngoma ya msanii Philbert Kabago ambaye alikuwa memba wa Kundi la SWV lenye maskani yake jijini Mwanza.

“Unajua hata kipindi kile nafanya muziki mwaka 2000, nilikuwa nasoma kidato cha pili, baada ya kukamilisha albamu yangu nikaamua ‘kuji-kipu’ bize na masomo mpaka hivi karibuni nilipohitimu katika Chuo Kikuu cha Tumaini, Iringa nilipokuwa nachukua Sheria. Kwa hiyo mbali na muziki hivi sasa natafuta kazi kama msomi,” alisema Farida.

Ndani ya ngoma hiyo ya Kabago yenye jina la Wivu, mrembo huyo ameonesha uwezo wa nguvu kitu ambacho kimeifanya ShowBiz iamini kuwa bado yuko fiti. Kwa upande wa Philbert ambaye pia ni mtangazaji wa kituo kimoja cha redio pande hizi, alisema kwamba aliamua kumshirikisha Farida ili kuleta tofauti katika kazi zake ikiwa ni ‘projekti’ ya albamu mpya.

*********************************

MLELA "Natamani kuchana lakini sauti sina"
Kutoka pande za Kinondoni, Dar es salaam, staa wa muvi za Kibongo mwenye cheo cha ‘Ijumaa Sexiest Bachelor’ Yusuph Mlela a.k.a Angelo amesema na ShowBiz kwamba mbali na kugonga filamu anahusudu sana game ya muziki, lakini tatizo linakuja kwenye sauti, Samirah Phillip alipiga naye stori.

Ndani ya safu hii, juzikati Mlela alitamka ishu hiyo baada ya kuulizwa ni sanaa gani nyingine anaikubali mbali na kuigiza. Pia mchizi alisema kwamba angekuwana sauti ya ukweli tayari angekuwa ameshagonga singo kadhaa kama siyo kudondoka na albamu.

“Lakini pamoja na yote nawaheshimu sana wanamuziki wa Kibongo wanaoendelea kufanya vyema kila kukicha, nawakubali sana,” alisema Mlela huku akimalizia kwamba ushindi wa Ijumaa Sexiest Bachelor unaendelea kumuweka juu kila jua linapochomoza kwa kumfanya aongeze idadi ya dili ikiwemo kupiga matangazo ya makampuni mbalimbali huku mtaani heshima ikiongezeka mara dufu.
*****************************

Benjamin
AT
Benjamini, A.T Wamefulia
Yale maoni tunayoendelea kuandika karibu kila wiki kupitia hapa kuhusiana na kuporomoka kwa game ya muziki wa kizazi kipya yanaonekana kuanza kuleta changamoto kwa wasanii wa muziki huo ambao wengi wameanza kufanya kazi za ukweli zinazoashiria kuwarudisha vizuri kunako mradi huo.

Baadhi yao ni vijana wawili, Benjamini wa Mambo Jambo na A.T kutoka Uswazi Records ambao kazi zao ziko poa ile mbaya. Kama bado haujafahamu ni ngoma zipi nazizungumzia, ‘Nimefulia’ ambayo Benja kampa shavu msela huyo wa Uswazi, huku ‘Nipigie’ ya A.T na Stara ikionekana kuanza mwaka vyema.

Kama wasanii wote wataamua kuumiza vichwa na kufanya kazi za ukweli huku wakipata sapoti ya kutosha kutoka kwa wadau mwaka huu unaweza kuwa wao baada ya kupoteza mwelekeo kwa kipindi kirefu.

Wednesday, February 3, 2010

IT&C SUMIT 2010 LAUCHED

Chief Operations Officer of Wia Company Mr Michael Anderson poses with some of the company's staff at the IT & Communications Summit 2010 press conference at the Paradise Hotel in Dar es salaam some few minutes ago.

Ankal Michuzi 'eating' some konozzzz with Wia ladies at the occasion
(pictures: blog ya jamii)

Ana Miaka 13 Lakini Anaonekana Kama Bibi wa Miaka 50



Siku moja Zara Hartshorn alipanda basi la abiria na kutaka kukata tiketi ya watoto lakini dereva wa basi hilo alimuangalia kwa mshangao na kumwambia kuwa asifanye masihara alipe pesa kamili.

Zara aliposema kuwa yeye ni mtoto na ana umri wa miaka 13, dereva huyo ambaye alikuwa ni mzee wa makamo, alicheka sana na kumwambia kama ndio hivyo basi na mimi nina umri wa miaka 21.

Abiria nao waliingia kwenye mjadala huo na kumuunga mkono dereva kuwa Zara anawachezea watu akili kwani anaonekana wazi kuwa yeye ni kikongwe mwenye wajukuu.

Zara kwa aibu alishuka toka kwenye basi hilo na kusubiria basi jingine kwa imani dereva wa basi lifuatalo angeweza kumuelewa kuwa yeye ni mtoto.

Kusoma zaidi stori ya Zara linki ni hii

http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=4017954&&Cat=7

Tuesday, February 2, 2010

TIBA YA LISHE KWA WAGONJWA WA ANEMIA

Hakuna tiba bora kama chakula na kila ugonjwa una chakula chake kama tiba. Mgonjwa hulazimika kutumia dawa za hospitali pale hali inapokuwa mbaya na ugonjwa unapokuwa umefikia hali mbaya.

Hata hivyo, baada ya mgonjwa kujijua ugonjwa unaomsumbua, hupaswa kujua pia aina ya vyakula anavyopaswa kula au kuacha kula, ili kudhibiti tatizo na hatimaye kuliondoa kabisa mwilini.

Leo tunaangalia aina ya vyakula anavyopaswa kula mgonjwa wa Anemia aina zote, ukiwemo Sickle Cell (magonjwa ya kupungukiwa damu mwilini kutokana na sababu mbalimbali).

APPLES
Tufaha au kama linavyojulikana na wengi ‘Apple’ ni tunda muhimu sana kwa wagonjwa wa Anemia. Wanaosumbuliwa na ugonjwa huu, wanashauriwa kula epo 2 hadi 3 kwa kila siku. Tunda hili linaelezwa kusaidia kuongeza kiwango cha madini ya chuma mwilini ambayo huhitajika sana kwenye damu.

VITAMIN B12
Ulaji wa Vitamin B12 ni muhimu sana kwa kinga na tiba ya ugonjwa wa Anemia. Chanzo kikuu cha vitamini hii ni vyakula vitokanavyo na wanyama, hasa nyama ya maini na figo. Nyama hii ni miongoni mwa tiba bora kabisa za ugonjwa huu.
KAHAWA NA CHAI
Hili ndiyo jambo la kuzingatia sana, kwani ndipo ambapo wagonjwa wengi hufanya makosa. Mgonjwa wa Anemia au Siki Seli hatakiwa kunywa chai wala kahawa kwa sababu vinywaji hivi huwa ni kikwazo kwa ufanyaji kazi wa madini ya chuma mwilini.

Unapokuwa mgonjwa wa wa maradhi hayo na ukawa unakunywa chai na kahawa kama kawaida, huwezi kuudhibiti ugonjwa vizuri na dawa utakazokuwa ukitumia hazitafanyakazi ipasavyo, kwa sababu itakuwa ni sawa na mtu anayelala kwenye chandaru kilichotoboka.

BEETS ROOTS
Beets Roots ni aina fulani ya viazi ambavyo vinajulikana pia kama viazi pori. Viazi hivi ni muhimu sana kwa tiba ya ugonjwa wa Anemia kwani vina protini na madini mengi kama vile potassium, phosphorus, calcium, sulphur, iodine, iron, copper, carbohydrates, protein, fat, na vitamin B1, B2, B6, C na P. kwa sababu hii, beets ni tiba nzuri sana ya asili.

MAJI BARIDI
Aidha, uogaji wa maji baridi nao ni sehmu ya tiba asilia ya Anemia. Mgonjwa anashauriwa kuoga maji baridi mara mbili kwa siku. Aidha, uogaji huku ukiwa juani nao husaidia uzalishaji wa Red Cells ambazo ni kiungo muhimu cha damu.

ASALI NA LIMAU
Asali pia imetajwa kuwa tiba nzuri kwa wagonjwa wa Anemia. Changanya asali na limau kiasi kidogo na kunywa asubuhi kabla hujala kitu chochote. Hii nayo ni miongoni mwa tiba bora asilia za ugonjwa huu. Halikadhalika tende zimetajwa kutibu Anemia.

MASSAGE
Ufanyaji wa masaji kila siku nao ni muhimu kwa mgonjwa Anemia, kwani husaidia kuweka juu kiwango cha damu wakati wote. Hii nayo ni moja ya tiba rahisi kabisa unayoweza kuifanya nyumbani kwako.

MWISHO,
Mazoezi mepesi ya kila siku na yale mazoezi ya kuvuta na kushusha pumzi nayo ni muhimu na husadia sana katika kuweka damu katika hali inayotakiwa. Mgonjwa wa Anemia na siko seli akiishi kwa staili ya kufuata maelekezo haya, anaweza asisumbuliwe sana na ugonjwa huo kwa maisha yake yote.

Monday, February 1, 2010

WIKIENDA SHOWBIZ!

Madee vs Afande: Wanakumbusha 2pac na Biggie
Bongo Fleva unapoteza muelekeo, wanamuziki badala ya kujishughulisha kuhakikisha unasimama ili kurudi kwenye chati yake, wenyewe wanakomaa na malumbano.

Huzuni ni kuwa mtu ambaye alionekana ni mr. wisdom kutokana na mashairi yake kubeba ujumbe unaokemea tabia za wanamuziki kulumbana ndiye anayeonekana kushika kasi! Anataka tuamini katika msemo wa kiongozi wa dini feki eti “fuateni maneno yangu, si matendo yangu!”

Suleiman Msindi a.k.a Afande Sele tuna mashaka naye, ndani ya nyimbo zake mbili, Mtazamo na Darubini Kali anakataza malumbano lakini ni yeye huyo huyo leo hii anatupiana madongo na rapa kutoka Manzese, Tip Top Connection, Hamad Ali ‘Madee’.

Ilikuwa ni bifu ya kimya kimya, baadaye Sele akaamua kumchana Madee kwenye wimbo wake Kingdom kuwa janki huyo wa Tip Top ni rais gani anaongea matusi na hana ofisi?

Juzi kati alipohojiwa na kituo kimoja cha redio Bongo, Sele alisema kuwa ni muda mrefu Madee amekuwa akimuimba akaitolea mfano traki, Mikono Juu ambapo alidai kwamba prezidaa huyo wa Manzese alimtusi katika mstari “Umeshawahi kuona wapi Mfalme ana rasta chafu?”

Madee alipoongea nasi, anakana kuwahi kumlenga Afande na kugandamiza kuwa anachojua yeye ni kwamba Mfalme Sele ameishiwa, hivyo anataka kutoka kupitia jina lake. Is it?

Sele alisema: “Bwa’ mdogo Madee ananikubali, unajua yule ni mazao yetu sisi wakongwe ndiyo maana hawezi kuimba bila kunitaja. Mimi mwenyewe namkubali kwa sababu ni mazao yetu yanayofanya vizuri kwenye fani.”

Ni picha mbaya mno, Mfalme Sele ambaye ni mhubiri mzuri wa nyimbo za mipasho, huko nyuma aliwahi kuingia kwenye malumbano na dogo wa Kora Hill Moro, Philipo Nyandindi ‘O Ten’.

Afande na Madee, Wabongo hawapo tayari kusikiliza malumbano yenu kwa sasa, kuna vitu vingi vya kuimba vyenye maana kubwa kwa jamii. Bongo Fleva unaporomoka badala ya kuandika tenzi za kuujengea afya, ninyi mnapigana misumari. Inakera!
************************************

Wakali Bongo Flava wanyoosha mikono MAAFA KILOSA
Wakali kibao wanaofanya game ya muziki wa Bongo Flava, wameungana na kutoa walichowezeshwa na Muumba Ardhi na Mbingu kwa ajili ya kuwasaidia waathirika wa mafuriko ya Kilosa, Moro.

Mradi wa kuchangia Maafa ya Kilosa kwa wasanii wa Bongo Flava, ulianzishwa na Redio ya Watu Clouds FM na imekuwa ikiwasiliana na mmoja mmoja ili kuhakikisha mastaa wanahusika kwenye matatizo ya jamii.

Tangu Clouds ilipoanzisha harambee hiyo, wasanii wengi wamekuwa wakijitokeza na kutoa kile walichowezeshwa, hivyo kuifanya industry ya muziki Bongo kusogea hatua nyingine kwa wasanii wake kugeuka wahisani kwenye shughuli za kijamii kama ilivyo Mamtoni.

Katika kusindikiza mradi huo wa uchangiaji, mkali wa Hip Hop mwenye vocal za kigumu, Fareed Kubanda ‘Fid Q’ amewahamasisha wenzake na kuingia studio kisha kutoa traki ya maana ambayo hivi sasa inabamba kupitia redio.

Bravo Clouds kwa wazo lenu la maana, pia wasanii na wengine wengi kwa kuitikia wito na kukubali kuvunja benki zenu kwa ajili ya kuwachangia ndugu zetu walioathirika na maafa hayo huko Kilosa, mkoani Morogoro.
*******************

Pipi: Mawe 10 tayari, albamu njiani!
Black cutie on Bongo Fleva industry, Doreen Aurelian a.k.a Pipi, yupo tayari kutoka, akiwa na mawe yake 10 mazito anayotaraji kuyajaza kwenye albamu yake ya kwanza ambayo ipo njiani.

Pipi ambaye ni product ya Tanzania House of Talent (THT), amekamilisha mawe hayo ambayo ni strongly katika soko la muziki nchini lakini jina kamili la albamu bado hajapata.

“Albamu tayari lakini jina bado, nipo natafakari pamoja na menejimenti yangu kuhusu wimbo utakaonza kuchezwa hewani ili kuitangaza albamu yangu,” alisema Pipi ambaye alichomoza kupitia traki ya Njiapanda ambayo ni mali ya Barnabas na kuongeza:

“Inawezekana nikarelease Usinune ambao nimefanya na Barnabas au Bora Wewe ambao nimekomaa nao mwenyewe.”

Aliongeza, mzigo mzima umesimamiwa na THT na nyimbo zimerekodiwa Bongo Record kwa Majani, 59 Records, B Hits Company kwa Hermy B na Duke.

Alitaja nyimbo nyingine na wasanii aliowashirikisha kuwa ni Moyo ft G. Nako & Juacali, Ukiniacha, Usikatae, Bora Wewe, Nilikupenda, Njiapanda (amekubaliana kushea na Barnabas) na Usinune.
******************

Nyota Ndogo Ageukia muziki wa Injili
Mkali wa muziki wa kizazi kipya Afrika Mashariki, Nyota Hassan Ndogo amefanya ‘wandaz’ na hivi sasa kule pande za Kenya ni gumzo baada ya kuingiza vocal kwenye wimbo mmoja wa Injili.

Inajulikana kwamba Nyota ni Muislamu, kitendo chake cha kuimba Injili kimechukuliwa kama anaisaliti imani yake, hivyo kuibua mjadala mkubwa nchini Kenya hususan Mombasa.

Katika wimbo huo, Nyota ameshirikishwa na mwimbaji wa Injili, Gabriel.
Hata hivyo, Nyota amesema kwamba yeye ni Mwislamu kamili na imani yake haijatetereka isipokuwa aliingiza vocal kwenye wimbo huo kwa sababu aliombwa na mwenzake kufanya hivyo kisanii.
***********************

Megan
Megan Fox: Asaliti, ampa penzi Cristiano Ronaldo
Abby Cool & MC George over the weekend bado ipo kazini na Ebwana Dah! Ndiyo jina la column yetu. Kama kawa ikiachana na mmoja, wiki inayofuata inahusika na mwingine katika mtindo bora zaidi.

Muigizaji Megan Fox ndiye staa anayepanda kizimbani leo na hapa inatajwa orodha ya wanaume ambao kwa nyakati tofauti, kwa ridhaa yake na mapenzi tele aliamua kujipurua mavazi mwilini na kuwapa penzi lake.

Kwa mujibu wa ‘site’ ya intaneti inayojihusisha zaidi na habari za uhusiano wa mastaa katika eneo la nani kamrukia nani, wanaume ambao wanatajwa kuwahi kufaidi penzi la Megan ni wanne!

Kubwa linalochukua nafasi kwenye ishu ya Megan ni staa huyo kumsaliti mpenzi wake Brian Austin Green na kumpa penzi mwanasoka wa kimataifa wa Ureno, anayekipiga Klabu ya Real Madrid ya Hispania, Cristiano Ronaldo.

Inaelezwa kuwa wakati Megan akiwa na sweetheart wake Brian, alikolea kwa Ronaldo, hivyo bila hiyana akaamua kukwea naye on bed na kujikunja kisela kwa mahaba motomoto.

Hata hivyo, inawekwa wazi kuwa pamoja na Megan kumpa penzi Ronaldo lakini Brian alichukulia poa, hivyo mpaka leo bado wapo pamoja na yote yanayohusu mapenzi wanayanogesha kama kawa!

Katika listi ya wanaume wa Megan, anayetajwa wa kwanza kuchangamka naye ni Ben Leahy aliyechetuana naye kati ya mwaka 2000 – 03, akaja David Gallagher mwaka 2003 – 04, mwaka 2005 akahamishia majeshi kwa Brian ambaye kinaeleweka mpaka leo. Mwaka 2009 ndiyo alimuonjesha Ronaldo.

Jina lake kamili ni Megan Denise Fox, alizaliwa Mei 16, 1986, Rockwood, Tennessee, Marekani. Ni mhitimu wa St. Lucie West Centennial High School, Port St. Lucie, Florida, Marekani na muvi iliyomtoa ni Transformers.
********************
compiled by mc george