Sunday, November 15, 2009

NANI NA NANI WAMEOANA WIKIENDI HII?






Kwa picha zaidi zaidi nenda: harusini.blogspot.com

MKONO NA RAIS JK!

Komando Lady jaydee a.k.a Manka, ndani ya 'handshake' ya nguvu na JK. Hii ilikuwa pale Mlimani City mara baada ya Jide ku perform katika shoo maalum ya Mo Foundation usiku wa kuamkia Jumapili, Nov 14, 2009. (Picha: Issa Michuzi)


Mama Mdogo Kuliko Wote duniani Kujifungua Mtoto wa Tatu


Mama mwenye umbile dogo kuliko wote duniani anatarajia kujifungua mtoto wa tatu ingawa madaktari wamemuonya kuwa maisha yake yako hatarini kutokana na tumbo lake kuwa kubwa sana kuliko mwili wake kiasi cha kumfanya ashindwe hata kutembea.

Stacey Herald, ambaye ana urefu wa sentimeta 71 anatarajia kujifungua mtoto wa tatu ingawa madaktari wameendelea kumuonya kuwa maisha yake yako hatarini kutokana na mimba aliyonayo kumuelemea.

Stacey alishayapuuza maoni ya madaktari mara mbili na kufanikiwa kujifungua watoto wawili ambao urefu wao wakati walipozaliwa ulikuwa ni zaidi ya nusu ya urefu wake.

Kwa habari kamili link ni hii:http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=3536918&&Cat=7

Saturday, November 14, 2009

mamaa ndikumana!!!

wenye macho hawaambiwi tazama....! (picha na RAY THE GREATEST)

Tuesday, November 10, 2009

Safisha tumbo lako kwa chakula


WAZUNGU wana msemo usemao ‘death begins at colon’, ukiwa na maana kwamba kifo huanzia kwenye utumbo mpana. Matatizo mengi ya kiafya yanayosababisha maradhi sugu na hatari na hatimaye kuchukua uhai wa mtu, huanzia kwenye utumbo (tumboni).

Chanzo cha hali hiyo hutokana na mtu kula chakula kama kawaida na kushindwa kupata choo cha kutosha kwa muda mrefu. Hali hiyo inapoendelea, mabaki ya chakula yaliyopaswa kutolewa nje ya tumbo kwa njia ya haja kubwa, hugeuka na kuwa sumu na kuathiri mfumo mzima wa mwili.

Kwa kuzingatia ukweli huo, ndiyo maana wataalamu wetu wa masuala ya lishe na afya wamesisistiza kufanya linalowezekana kuhakikisha tunasafisha matumbo yetu kwa kupata choo cha kawiada kila siku. Kuna njia nyingi za kusafisha tumbo, ikiwemo ile maarufu ya ‘enema’ ambayo tumeshaieleza zaidi ya mara moja katika makala zetu zilizopita. Lakini katika makala ya leo tutaangalia usafishaji wa tumbo wa asili kwa kutumia vyakula asilia.

Usafishaji wa tumbo unaweza kufanyika ukiwa nyumbani kwako na ukaufanya bila wasiwasi wowote kwa kula tu vyakula vyenye uwezo wa kufisha tumbo.

Njia hii siyo tu ni rahisi kuifanya, lakini pia ni salama na ni ya kiafya zaidi katika suala zima la kusafisha utumbo. Gharama za kusafisha tumbo huwa ni za juu sana iwapo utataka uipate kutoka clinic au kwa wataalamu wengine wa afya, lakini huwa siyo lazima. Unahitaji kujua tu aina ya vyakula vinavyosaidia kusafisha tumbo.

VYAKULA BORA
Vyakula bora vinavyoaminika kufanyakazi nzuri ya kuimarisha mfumo wa usagaji chakula na hatimaye kusaga chakula kirahisi na kwa haraka ni vile vyenye kiwango kikubwa cha ‘fibre’ (kamba lishe). Vyakula hivyo ni pamoja na mboga na matunda mbalimbali.

Kwa mujibu wa wataalamu wetu, matunda na mboga ndiyo yenye kiwango kikubwa cha ‘fibre’ au ufumwele. Matunda aina ya Tufaha (Apple), Peasi (Peas), makomamanga, n.k, yana kiwango kikubwa cha ‘fibre’ hivyo yanafaa kuliwa kwa wingi.

Kwa upande wa mboga-mboga na nafaka, kuna maharage, kunde, ngano na nafaka nyingine zisizokobolewa, vyakula hivi vyote vinaaminika kuwa na kinwago kikubwa cha ‘fibre’. Hivyo ili kulijengea tumbo lako mfumo mzuri wa kusaga chakula na baadae kupata choo chepesi na cha uhakika kila siku, pendelea kula matunda kwa wingi na vyakula vingine vilivyoainishwa hapo juu.
FAIDA ZA KUSAFISHA TUMBO
Baadhi ya wataalmu wa masuala ya afya wanasema kuwa usafishaji wa tumbo hupunguza uwezekano wa kupata maradhi ya saratani, kidole tumbo na matatizo mengine. Tumbo linapokuwa chafu huathiri uzito wa mwili, afya ya akili na hata ngozi ya mwili.

KIWANGO KINACHOTAKIWA KWA SIKU
Tunapohimizwa kula kwa wingi matunda, mboga na vyakula vingine vyenye kiwango kikibuwa cha ‘fibre’, ni vyema tukajua pia ni kiasi gani kinachopendekezwa. Kwa mujibu wa wataalamu, mtu mzima mwenye umri chini ya miaka 50, anatakiwa kula kiasi cha gramu 38 kila siku. Watu wazima wenye umri zaidi ya miaka 50 wanatakiwa kula kiasi cha gramu 30. Wanawake wenye umri chini ya miaka 50 wale gramu 25 na wale wa zaidi ya miaka 50, wale gramu 21.

Monday, November 9, 2009

MRISHO'S PHOTOGRAPHY!


JIONEE PICHA MBALI MBALI ZA MAHARUSI WALIOPENDEZA HAPA: www.harusini.blogspot.com

Vivazi vya madada zetu na kasheshe za upepo



zaidi nenda hapa: http://www.nifahamishe.com/album_preview.aspx?AlbumId=602865

WIKIENDA SHOWBIZ!

Artists Bongo hawana elimu ya mikataba
Kila siku artists wanalalamika kuwa wanadhulumiwa, mara wanamtaja mdosi, wakati mwingine meneja na hata prodyuza. Abby Cool & MC George over the weekend inaweza kutoa comments kuhusu hilo.

Tulifuatilia kwa karibu sakata la Dullayo na prodyuza wake Marko Chali kuwa wamedhulumiana. Dullayo akilalamika kutiwa ndani mzigo mzima ambao waliusaini kwa mdosi, shilingi 1,000,000 keshi kama utangulizi wa nakala za albamu ambazo waligonga.

Dullayo ndiye aliyekuwa wa kwanza kuzungumza kwenye vyombo vya habari kuwa alikwenda na Marko Chali na kusaini kopi za albamu yake, lakini baada ya kukabidhiwa M 1, prodyuza huyo alimtosa na hakumpa hata kumi.

Baada ya dogo kuharibu, Ijumaa iliyopita, Marko Chali akiwa na Mkurugenzi wa MJ Production, Joachim Kimaryo ‘Master Jay’, walitinga studio za Clouds FM na kuweka ukweli ili watu wajue.

Kilichoelezwa na Marko pamoja na MJ ni kuwa Dullayo aliingia mkataba na Marko Chali kwa ajili ya kurekodi albamu, kwahiyo M 1 iliyotolewa na mdosi, imetumika kufidia gharama ya uzalishaji wa nyimbo.

Ilielezwa kuwa Dullayo alikuwa anadaiwa shilingi 3,500,000, kwahiyo baada ya mdosi kukata milioni moja, bado anadaiwa shilingi 2,500,000. Eti, hili msanii huyo analijua na lipo kwenye mkataba.

MJ na Marko waliweka wazi kuwa msanii akiwa kwenye label, anagharimiwa kila kitu, lakini wakati wa mauzo, hukatwa kwanza fedha zilizotumika kuandaa kazi yake yote, halafu faida ndiyo hugawanywa kati ya msanii na label.

Kinachoonekana kutoka kwenye mazungumzo hayo ni kuwa Dullayo alipoona M imetolewa, alijua ni yake moja kwa moja, wakati kuna makato ya gharama za kumuandalia albamu yake ili iende soko. Hili ni tatizo na wasanii wengi wapo kwenye msafara huu.

Wasanii wengi hawajui mikataba, wanapaswa kuelimishwa kuhusu hili. Maelezo ya mkataba yanasema utaanza kuvuna mafao baada ya gharama zilizotumika kukuandaa wewe msanii kurudi, lakini saini ya kwanza tu unataka mgao, halafu unatangaza umeibiwa. Hapa tunataniana.

Hapa juzi kati, Tundaman alisaini mkataba na meneja wa Berry 9 wa kufanyakazi pamoja, lakini baadaye dogo akakana, wakati saini yake ipo. Hii ni wazi kuwa artists wetu wengi hawajui mikataba, inabidi waelimishwe.
**************************

Cassie amelegeza kwa wawili tu, P. Diddy ndani
Ni ishu ya staa gani katoka na nani, mwanamuziki Cassie ndiye yupo kizimbani leo na hapa itatajwa orodha ya wanaume ambao kwa nyakati tofauti, tena kwa hiari yake alilegeza na kukwea nao on bed.

Kwa mujibu wa mtandao unaodili na ‘ishuz’ za mastaa wa kiwanja, Ryan Leslie ndiye kidume namba moja anayetajwa kupumzika na mrembo huyo, inatajwa kwamba walianza kucharukiana mwaka 2006 na kuachana 2007.

Staa mwenye fedha zisizosumbua, Sean Puffy Combs ‘P. Diddy’ au Puffy Daddy kama alivyokuwa akijulikana zamani, anatajwa nambari mbili kwamba alianza kuchetuka naye mwaka 2008.

Mrembo Cassie, jina lake kamili ni Cassandra Ventura, umri wake ni miaka 23, alizaliwa Agosti 26, 1986, New London, Connectcut, Marekani. Nyota yake ni Virgo, ana urefu wa futi 5.75.
*************************


Blu:Mimi shule sasa basi
Dogo mwenye uwezo mkubwa wa kuishi kistaa, Heri Samir ‘Blu’ amesema kuwa hivi sasa akizungumzia ishu ya shule atakuwa anadanganya kwa sababu haipo kwenye programu yake.

Blu, staa wa Bongo Flava asiyefunikika, alisema kupitia kipindi cha XXL, Clouds FM kuwa ana mambo mengi yanayomkip busy lakini ishu ya elimu haipo kwenye ratiba yake.

Dogo huyo ambaye anajulikana pia kwa jina la Kabayser, alizungumza hivyo kama jibu la swali aliloulizwa na presenta wa Clouds, Fatma Hassan ‘DJ Fetty’.

Mbali na ishu ya elimu, Blu alisema kuwa sasa hivi hayupo kwenye mikakati ya albamu, isipokuwa atakachokuwa anakifanya ni kudondosha singo kali kila mara ili kuwapa raha ‘fans’ wake.

Aidha, Blu alimpa shavu Dogo Hamidu a.k.a Nyandu Tozz kuwa ndiye mtu aliyempeleka studio kwa mara ya kwanza, MJ Record ambapo alifanya singo yake ya kwanza inayoitwa Kwa Mama.
*******************************
Eliza ampa onyo Kelvin
The Most Beautiful Girl ndani mjengo wa Big Brother Revolution, Elizabeth Gupta ‘Queen’ amemuonya ‘best friend’ wake, Kevin kuwa kama kuna msichana anayemuumiza nje ya jengo basi aache mara moja.

Eliza, alimtolea uvivu Kevin wiki iliyopita kwa kumwambia kuwa anaona vitendo vyake kwa macho, hivyo kuendelea kumsihi aache mchezo huo.

“Kama kuna msichana ambaye unamuumiza huko nje ya nyumba tafathali acha,” alisema Elizabeth.

Kabla ya kusema hayo, Elizabeth na Emma walikuwa na mazugumzo ambayo yalichukua muda mrefu kumzungumzia Kevin.

Eliza alimwambia Emma kuwa walipokutana kwa mara ya kwanza na Kevin, alimueleza kwamba ana mpenzi.
****************
Leonel amueleza Mzamo anachopendelea faragha

Mshiriki wa Msumbiji, Leonel wikiendi iliyopita alifanya ‘wonders’ baada ya kumueleza Mzamo mitindo ya kimapenzi ambayo yeye huifurahia kiawa faragha.

Katika kile kilichoonekana kuwa alikuwa akimtega mwenzake, wakiwa wamelala kitanda kimoja kwa staili ya mzungu wa nne, Leonel alimwambia Mzamo kuwa akiwa faragha hupendelea kuangalia juu.

Aidha, Leonel pia alimuonesha kwa ishara jinsi anavyoweza kukubaliana na mtindo huo akiwa faragha.

Hata hivyo, baada ya maongezi hayo, watazamaji wengi walituma maoni, wengi wa
**********************
compiled by mc george

Sunday, November 8, 2009

MASIKINI MAISHA CLUB!





Mashabiki wa muziki wa disco wa ukumbi wa kisasa wa Maisha Club ulikuwa pale Hotel Karibu, Oysterbay jijini Dar, watakosa burudani hiyo kwa muda usiyojulikana baada ya kuteketea kwa moto leo mchana..ja ajabu hadi sasa moto huo unawashangaza wengi jinsi ulivyoibuka kwani kulikuwa hakuna disco na umeme ulikuwa umezimwa ndani ya jengo hilo kama ilivyo ada!! Ni hivi karibuni tu ukumbi huo ulifunguliwa baada ya kufanyiwa ukarabati wa hali ya juu ulioufanya uonekane wa kisasa zaidi!

Friday, November 6, 2009

IJUMAA SHOWBIZ!


Busta Kudondoka Bongo. Fiesta yasogezwa mbele
Mchizi kutoka pande za kwa Obama, Trevor Tahiem Smith Jr a.k.a Busta Rhymes anatarajiwa kudondoka Bongo hivi karibuni kwa ajili ya shoo ya Fiesta ‘One Love’ itakayogongwa ndani ya Viwanja vya Posta, Kijitonyama, Dar es Salaam.

Mratibu wa Tamasha hilo, Godfrey Kusaga alisema na ShowBiz kwamba, shoo hiyo ambayo ilikuwa ifanyike kesho Jumamosi imesongezwa mbele hadi Novemba 21 mwaka huu na kwamba Busta atadondoka siku chache kabla ya ishu hiyo.

“Tumelazimika kusogeza shoo mbele kwasababu ya msiba wa Mzee wetu, Alex Kussaga ambaye alifariki dunia jana (Jumanne) na mazishi yanatarajiwa kufanyika Jumamosi (kesho). Tunachukua fursa hii kuwaomba radhi mashabiki wa Fiesta na wapenda burdani kwa ujumla kwakuwa msiba huja bila taarifa,” alisema Godfrey.

Mbali na Busta wakali wengine kutoka Bongo watakaosimama kunako steji ya Fiesta ni pamoja na Mwasiti, Prof. Jay, TMK Wanaume Family, Maunda Zorro, Lady Jaydee, Baby Madaha, Ngwea, Mr. Blue na wengine kibao.
********

50 Cent “Obama akiniita ntakwenda fasta”
Mwana Hip Hop aliyewahi kushuka Bongo na kupiga shoo ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee, Cults Jackson a.k.a 50 Cent ambaye ni Kiongozi wa Kundi la G-Unit amesema kuwa anatamani kama angekuwa Mshauri wa mambo ya Fedha wa Rais wa Marekani, Barack Obama.

Akipiga stori na mtandao mmoja hivi karibuni alipokuwa London akitangaza muvi yake mpya yenye jina la Dead Man Running, 50 Cent alisema kuwepo kwa uongozi wa Obama nchini kwao ni kitu kikubwa na ikitokea rais huyo akamwita basi atafanya hivyo mara moja.

Watu wengi duniani wanaamini kwamba 50 alikuwa akimsapoti Rais Bush lakini ukweli ni kuwa yeye anamkubali zaidi Obama na hakuwahi kufikiria juu ya uongozi wa Bush hata siku moja.
*********

Wednesday, November 4, 2009

MSHALE anakuja kuwashika!

Wapenzi wa muziki kaeni mkao wa kula, MSHALE anakuja, ni msanii mpya anakuja kuwashika na Single yake makini iiitwayo NIWE NAWE. Pini hili limerekodiwa pale Fish Crab, chini ya Producer mahiri, LAMAR. Ndani Ya Single Hii Mshale Amemshirikisha Raper Maarufu katika Tasnia ya Muziki wa Bongo Fleva, ambaye Jina Lake Limehifadhiwa kwanza mpaka single hii Itakapoenda redioni mapema wiki ijayo. Karibu MSHALE ndani ya jukwaa la Bongo Fleva!

KARIBU MSHALE!