Saturday, May 26, 2012

Men in black 3 in 3D movie launch


Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sam Elangallor (kulia)
akimpongeza Monica Joseph mmoja wa wateja wao waliohudhuria uzinduzi
wa filamu ya ‘Men in Black 3 in 3D uliodhaminiwa na Airtel katika
ukumbi wa Century Cinemax, Mlimani City, Dar es Salaam jana. Monica
alishinda simu ya mkononi.



Meneja Huduma wa Airtel, Hilda Nakajumo (kulia) akizungumza wakati
wa uzinduzi wa filamu ya ‘Men in Black 3 in 3D


DJ Fetty wa Clouds Radio naye akipokea zawadi yake kutoka kwa
Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel Tanzania, Irene Madeje Mlola


Mkurugenzi wa Biashara wa Airtel Tanzania, Irene Madeje Mlola
(kulia) akitoa zawadi kwa  Monica Joseph mmoja wa wateja wao


Mbunifu wa Kimataifa, Flaviana Matata (kushoto) akipozi kwa picha
na Hilda Nakajumo, Meneja Huduma wa Airtel Tanzania


Ofisa Mauzo wa Airtel, Babra Ernest (wa pili kulia) akizungumza
wakati wa uzinduzi wa filamu ya ‘Men in Black 3 in 3D


Sehemu ya watu waliohudhuria uzinduzi wa filamu ya ‘Men in Black 3


Friday, May 25, 2012

WAZIRI MAKAMBA ATEMBELEA AIRTEL

Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,  January
Makamba (kushoto) akipokewa na Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania,Sam Elangallor,  alipofanya ziara kukagua shughuli mbalimbali zakampuni hiyo jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni Mkurugenzi wa Mawasilino\ wa Airtel, Beatrice Singano Mallya.
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia,  January
Makamba (kushoto) akipokewa na Ofisa Mkuu wa Biashara wa AirtelTanzania, Chiruwi Walingo
Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel Tanzania, Beatrice SinganoMallya akiongozana na Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi naTeknolojia
Mkurugenzi Mtendaji wa Airtel Tanzania, Sam Elangallor (katikati)akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, January Makamba (kulia)
  

TANZANIA BEGA KWA BEGA NA UNDP KUJENGA AFRIKA YENYE UHAKIKA WA CHAKULA.

Baadhi ya Mabalozi, Maafisa wa Serikali na Umoja wa Mataifa na Taasisi mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Ripoti hiyo.
Baadhi ya Mabalozi, Maafisa wa Serikali na Umoja wa Mataifa na Taasisi mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Ripoti hiyo.
Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa UNDP nchini Tanzania Dk. Alberic Kacou akizungumza kwa niaba ya UNDP kuhusiana na kuzinduliwa kwa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 ambapo amesema huu sasa ni wakati kwa nchi za Afrika haswa zilizo kusini mwa Jangwa la Sahara kujenga mazingira ya kuelekea mustakabali wenye uhakika wa chakula.
Mshauri wa Uchumi UNDP Bw.Amarakoon Bandara akifanya 'presentation' ya Ripoti hiyo. Kushoto ni Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini Dk. Alberic Kacou, Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene na Mkurugenzi wa UNDP Tanzania Bw. Phillipe Poinsot.
geni rasmi Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Mbene na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa Tanzania, Dk. Alberic Kacou (kulia) wakifuatilia maoni ya Uchambuzi wa Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 kutoka kwa Maprofesa wa Vyuo vikuu nchini.

Na Mwandishi wetu.

Bara la Afrika ikiwemo Tanzania limeshakumbwa na matukio kadhaa ya kukabiliwa na uhaba wa chakula, uliokwenda sambamba na matukio ya watu wengi kupoteza maisha haswa Kusini mwa jangwa la Sahara na Ukanda wa Sahel eneo la Afrika Magharibi.

Hali hiyo imekuwa moja ya changamoto kubwa inazozikabili serikali za mataifa hayo ambapo yanapambana ili kuitatua ili kila mwananchi barani Afrika aweze kufurahia kukua kwa uchumi.

Akitoa hotuba wakati akizindua rasmi Ripoti ya Maendeleo ya Afrika 2012 leo jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Fedha Mh. Janet Membe (MB) amesema kwa muda mrefu sura ya eneo la nchi za Afrika zilizo Kusini mwa jangwa la Sahara imekuwa ni ya njaa ya kukithiri, ambapo zaidi ya mtu mmoja katika kila waafrika wane wana tatizo la upungufu wa lishe.

Amesema Ripoti hiyo inaonyesha kuwa pamoja na ukweli kwamba baadhi ya nchi zinazokuwa kwa kasi kiuchumi katika kipindi cha miaka kumi ziko Afrika, lakini bado hali ya maisha ya waafrika ni duni.

Awali Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa UNDP nchini Tanzania Dk. Alberic Kacou alisema bara la Afrika limejaliwa kuwa na ardhi yenye rutuba, maji ya kutosha na hali nzuri ya hewa kwa kukuzia mazao, lakini swali la kujiuliza ni kwanini bado kuna uhaba wa chakula.

Hata hivyo Dk. Kacou ametoa matumaini kuwa bara la Afrika bado lina uwezo wa kujijengea mazingira ya kuwa na akiba ya kutosha ya chakula kwa kipindi kijacho.

Ripoti hii ya Kwanza ya Maendeleo ya Afrika inasema kwamba ongezeko endelevu katika uzalishaji kwenye kilimo kunalinda haki ya chakula na uwezo wa watu kupata chakula.

    Picha na MO BLOG 

Marais Wastaafu nane wa nchi za Afrika wakutana nchini Afrika Kusini kwa siku tatu.

Pichani shoto ni   Rais mstaafu wa awamu ya tatu wa Tanzania,Mh Benjamini Mkapa akichangia mada mbalimbali zilizokuwa zikijadiliwa kwenye mkutano wa kujadili maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,mapema leo jioni,mkutano huo umefanyika kwenye moja ya kumbi ya   chuo  kikuu cha  Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini.Pichani kati ni Rais mstaafu Pedro Pires wa Cape Verde na mwisho ni Rais mstaafu wa Benin,Nicéphore Dieudonné Soglo.
Pichani kulia ni Rais mstaafu wa Benin,Nicéphore Dieudonné Soglo akifafanua jambo kwa makini wakati wa mchakato wa kujadili maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika ulipokuwa umepamba moto jioni ya leo,katika mkutano uliofanyika kweny moja ya kumbi ya   chuo  kikuu cha  Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini mapema leo mchana,Pichani kati ni Rais mstaafu Pedro Pires wa Cape Verde na   Rais wa awamu ya tatu wa Tanzania,Mh Benjamini Mkapa
Wageni waalikwa mbalimbali wakifuatilia yaliyokuwa yakijili kwenye mkutano huo
Wageni waalikwa mbalimbali wakifuatilia yaliyokuwa yakijili kwenye mkutano huo
Pichani juu na chini Mkutano wa kujadili   maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika ukiendelea ndani ya chuo  kikuu cha  Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini mapema leo mchana.
Baadhi ya Marais Wastaafu kutoka nchi mbalimbali za Afrika wakiwa kwenye mkutano wa kujadili   maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika.
Kutoka kushoto ni Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania,ambaye pia ni Mratibu mkuu wa mkutano akifafanua jambo kwa wageni waalikwa mbalimbali waliofika kuhudhuria Mkutano huo mapema leo mchana.
Kutoka kushoto ni Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania,Rais Nicéphore Dieudonné Soglo wa Benin,Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar,Rais Ali Hassan Mwinyi wa Tanzania,Rais Thambo Mbeki wa Afrika Kusini,Rais Olusegun Obasanjo wa Nigeria,Rais Pedro Pires wa Cape Verde, Rais Benjamin Mkapa wa Tanzania na Rais Rupiah Banda wa Zambia wakiwa katika picha ya pamoja mapema leo mchana kabla ya kuanza mkutano wa kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika.
Rais Mstaafu wa awamu ya tatu Tanzania,Mh Benjamini Mkapa akijadiliana jambo na Rais Nicéphore Dieudonné Soglo wa Benin walipokuwa wakiwasili kwenye viunga vya vya chuo  kikuu cha  Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini mapema leo kwa ajili ya kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika.
Pichani  mbele ni Marais Wastaafu wa Tanzania,Ally Hassan Mwinyi na  Benjamin Mkapa sambamba  na  Marais wengine wakiwasili katika viwanja vya chuo  kikuu cha  Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini mapema leo kwa ajili ya kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika.
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali kutoka nchini Tanzania,wakiwa katika picha ya pamoja nje ya ukumbi wa  kikuu cha  Witwatersrand, Johannesburg, Afrika Kusini mapema leo kwa ajili ya kuripoti mkutano wa kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika.Shoto ni Yvonne Msemembo (ITV) ,Joseph Kulangwa (Tanzania Standard News Paper),Nestor Mapund,Absolom Kibanda (Free Media),Mzee Theophili Makunga (Mwananchi Communications), Muondosha Mfanga (The Guardian) pamoja na Deus Mjatta (ITV).
Baadhi ya Wahariri wa vyombo vya habari mbalimbali wakijadiliana jambo nje ya ukumbi,kabla ya kuanza kwa Mkutano huo,Shoto ni Absolom Kibanda (Free Media),Mzee Theophili Makunga (Mwananchi Communications),Joseph Kulangwa (Tanzania Standard News Paper), Muondosha Mfanga (The Guardian).
Baadhi ya wanafunzi kutoka vyo mbalimbali wakiwa katika picha ya pamoja mapema leo kabla ya kuanza kwa mkutano wa kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika,ambao umewashirikisha Marais Wastaafu nane wa Afrika. 
========  ====== ========
Marais Wastaafu nane wa nchi za Afrika wakutana nchini Afrika Kusini.
Marais Wastaafu nane wa nchi za Afrika wamekutana leo jijini Johannesburg, Afrika Kusini na kufanya mkutano wa siku tatu ndani ya chuo kikuu cha Witwatersrand. Ajenda kuu ya mkutano huo ni kujadili  maendeleo ya matumizi ya nishati karne ya 21 kwa nchi za Afrika. Marais wastaafu hao waliohudhuria mkutano huo ni pamoja na Rais Olusegun Obasanjo wa Nigeria, Rais Ali Hassan Mwinyi wa Tanzania, Rais Nicéphore Dieudonné Soglo wa Benin, Rais Pedro Pires wa Cape Verde, Rais Benjamin Mkapa wa Tanzania, Rais Joaquim Chissano wa Msumbiji, Rais Amani Abeid Karume wa Zanzibar na Rais Rupiah Banda wa Zambia. Aidha - mbali ya Marais hao waliohudhuria mkutano huo, pia ulihudhuriwa na  Wataalam mbalimbali wa nishati, viongozi wa umma na sekta binafsi na wanafunzi na kitivo kutoka vyuo vikuu 9 vya kimataifa kikiwemo chuo kikuuu mwenyeji cha Witwatersrand a.k.a Wits. Tanzania iliwakilishwa na wanafunzi watano na walimu wawili kutoka chuo kikuu cha Dar-es-Salaam. Mratibu mkuu wa mkutano huo - Balozi Charles Stith  ambaye aliwahi kuwa balozi wa Marekani nchini Tanzania alisema kuwa lengo la mkutano huo ni kujadiliana juu ya ufumbuzi wa mageuzi ya nishati katika nchi za Kiafrika, na kuhakikisha nchi za Afrika zinajiwakilisha vyema katika kukabiliana na changamoto mbalimbali katika suala zima la Nishati. Balozi Stith alisema kuwa mkutano huo utaleta mshikamano wa pamoja kwa viongozi wa sekta ya nishati na wafadhili mbalimbali wa miradi mbalimbali, ili kuhakikisha nishati hiyo inatosheleza mahitaji ya Afrika kwa ujumla. Mkutano huo wa siku 3 utafikia tamati Mei 25.

Tuesday, May 22, 2012

DOX COSMETICS & BOUTIQUE MAHALI SAHIHI PAKUJIPATIA BIDHAA ZA KISASA






Jipatie Bidhaa bora za Urembo na Mavazi, Perfume, Deodorants, Hand Bags, Jewell's, Viatu, Body Lotions, Weaving's Original, Vifaa vyote vya nywele na ngozi kama Facial Products na vitu vyote vya Kisasa na vya Designers wenye majina makubwa duniani kwa wanaume na wanawake. Duka la DOX COSMETICS & BOUTIQUE linapatikana mtaa wa Jamuhuri karibu na Round about ya Azam maeneo ya Posta mpya jijini Dar es Salaam. Unaweza kuwasiliana nao kwa simu namba +255754204222 na +255787915151 au Barua Pepe d_membe@hotmail.com.




Monday, May 21, 2012

SHEREHE ZA UBINGWA WA SIMBA SC NA KUMUENZI MAFISANGO KUFANYIKA NDANI YA DAR LIVE

BARCODES KUWAKOMBOA WASANII DHIDI YA WIZI WA MALI SANAA ZAO

 
Mkurugenzi wa GS1, Fatuma Makange akitoa ufafanuzi wa namna Barcodes inavyodhibiti uhalali wa kazi za
wasanii.
 
Wadau mbalimbali wa sanaa wakifuatilia mkutano huo.
 
Katibu Mtendaji wa Basata, Ghonche Materego (kushoto) akizungumzia  hoja kutoka kwa wadau wa sanaa (hawapo pichani).   Kulia ni Fatuma Makange.
 
Rais wa Shirikisho la Filamu nchini (TAFF) mwenye shati jeupe) akifuatilia mkutano na wadau mbalimbali.
Kampuni ya GS1 leo ametambulisha mfumo maalum wa teknolojia ya kompyuta wa kusaidia kuZitambua haki miliki Za kazi za wasanii unaofahamika kama Barcodes.  Utambulisho huo umefanywa na Jukwaa la Sanaa  kwenye ukumbi wa Baraza la Sanaa Tanzania (Basata) Ilala jijini, Dar.

Kama mfumo huu utafanikiwa kwa asilimia mia moja, utasaidia kupunguza wizi wa kazi za wasanii kwani kila kazi ya msanii itatakiwa kuwa na Barcode yake itakayotambulika kimataifa na kazi yake itauzwa kwa mfumo wa ‘scanner’ hivyo si rahisi kufanya udanganyifu wowote na Watanzania watatakiwa kununua kazi hizo katika maduka maalum yenye ‘scanner’ hizo maalum.

                                     PICHA ZOTE NA ERICK EVARIST/GPL

MWANAMITINDO FLAVIANA MATATA AKABIDHI MSAADA WA MABOYA 500 JIJINI MWANZA LEO

Mwanamitindo Flaviana Matata akikabidhi msaada wa maboya 500 kwa mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Mwanza, Elias Makori kulia ikiwa ni kumbukumbu ya miaka 16 ya ajari ya meli ya MV Bukoba, anayeshuhudia ni Meneja Masoko na Biashara wa Shirika la Usafirishaji wa majini mkoani Mwanza la Marine Service, Kapten Obadia Nkongoki, Igoma jijini Mwanza leo.

Flaviana akionesha moja ya maboya yenye nembo ya foundation yake aliyokabidhi katika kumbukumbu ya miaka 16 ya ajali ya MV Bukoba ikiwa ni kampeni yake ya kupunguza ajali za majini hapa nchini.
Flaviana Matata akishindwa kujizuia na kuangua kilio wakati wa ibaada ya kumbukumbu ya miaka 16 ya ajari ya meli ya MV Bukoba alipotembelea baadhi ya makaburi ya watu waliopoteza maisha katika ajari hiyo yaliyopi Igoma jijini Mwanza, katika ajali hiyo Flaviana alimpoteza pia mama yake mzazi.

Waombolezaji wengine waliofiwa na ndugu zao wakiombea marehemu wa ajali hiyo.

Flaviana na wageni wakiweka  mashada kwenye makaburi ya waliofariki kwenye ajali hiyo leo Igoma jijini Mwanza.

Airtel yafanya uzinduzi kabambe wa huduma yao mpya ya supa 5 ndani ya coco beach,


Mmoja wa wasanii wa kufoka foka,aliyejitambulisha kwa jina moja la Rich akimwaga mistari mapema leo jioni wakati kampuni ya simu za mikononi ya Airtel, ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar.shoo kubwa ya uzinduzi kufanyika kesho jumapili hapo hapo coco beach siku nzima
Baadhi ya timu ya mauzo kutoka kampuni ya Airtel wakiuza bidhaa mbalimbali za kampuni hiyo mapema leo jioni wakati wa kampuni hiyo ,ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya Airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar.
Baadhi ya Wasanii wa kikundi cha Kinoko,kutoka Mwananyamala wakitumbuiza jukwaani mbele ya umati wa watu (hawapo pichani),mapema leo jioni wakati  kampuni ya simu za mikononi ya Airtel, ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar.
Wateja wapya mbalimbali wakiendelea kuhamia Airtel, mapema leo jioni wakati kampuni ya simu za mikononi ya Airtel, ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar.
Sehemu ya umati wa watu waliofika mapema leo jioni wakati kampuni ya simu za mikononi ya Airtel, ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar.
Mmoja wa wasanii wa kufoka foka,akionesha umahiri wake wa kughani jukwaani mapema leo jioni wakati kampuni ya simu za mikononi ya Airtel, ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar.
Mmoja wa wafanyakazi kutoka timu ya mauzo ya kampuni ya Airtel akiinadi modem ya Airtel 3.75G yenye kasi zaidi kuliko zote nchini, leo jioni wakati wa kampuni hiyo ,ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar. 
Baadhi ya timu ya mauzo kutoka kampuni ya Airtel  wakiuza bidhaa mbalimbali za kampuni hiyo mapema leo jioni wakati kampuni hiyo ilipokuwa ikifanya utambulisho na uzinduzi  wa huduma  mpya ya airtel/Airtel Super 5 uliofanyika kwenye ufukwe wa Coco beach,jijini Dar.
--




Popular Posts