Thursday, July 16, 2009

VIDOKEZO KUBORESHA USAGAJI CHAKULA TUMBONI


You are what you eat
Usagaji mzuri wa chakula una uhusiano wa moja kwa moja na ubora wa afya yako. Hakuna ubishi kuwa usagaji wa chakula ukiwa mbovu, hutapata choo ipasavyo na ukosapo choo ni dalili ya matatizo mengi ya kiafya mwilini. Chakula unachokula ndicho kitakachoamua hatma ya tumbo lako na ndicho kinachoathiri afya yako.

Mfumo wa usagaji chakula, ambao unapita kwenye utumbo unaokadiriwa kuwa na urefu wa futi 30, ndiyo wenye suluhisho la matatizo mengi ya kiafya yanayotukabili kuliko vile ambavyo tunaweza kudhani. Utumbo unapokuwa msafi, afya nayo huwa nzuri.

Katika makala ya leo, tutajaribu kukumbushana kwa kutoa vidokezo muhimu vya kuzingatia katika kufanikisha usagaji mzuri wa chakula utakao kuwezesha kupata choo sawasawa kwa na utumbo msafi utakaopitisha virutubisho muhimu vinavyohitajika na mwili wako:


VYAKULA ASILIA
Pendelea kula vyakula bora na asilia kuliko kupenda kula vyakula vilivyosindikwa na kuhifadhiwa kwa matumizi ya muda mrefu. Mfano, maharage ya kupika mwenyee ni bora kuliko ya kwenye makopo, halidhalika nyanya za kutayarisha mwenywe ni bora kuliko za kwenye makopo. Jaribu kula kila kitu kikiwa ‘fresh’ na asilia kadri uwezavyo.

UTAFUNAJI
Usagaji wa mzuri wa chakula tumboni huanzia mdomoni mwako. Hakikisha unatafuna sana chakula kabla ya kukimeza. Mate yako yanavimeng’enyo muhimu ambavyo husaidia usagaji wa chakula na kupambana na ‘bacteria’. Watu wengi huwa hawatafuni chakula, kitendo ambacho hufanya usagaji wa chakula kuwa mgumu kinapofika tumboni.

ULAJI MATUNDA
Ndani ya tumbo lako kuna mfumo unaotegemea sana ulaji wa matunda na mboga na vinapokosekana vitu hivyo, kunakuwa hakuna uwiano mzuri. Tunashauriwa na kusisitizwa sana kula matunda na mboga mboga kwa wingi, ambazo siyo tu hulinda mwili, bali pia ndiyo kichochoe kizuri cha usagaji chakula tumboni.

UNYWAJI MAJI
Watu wengi wanapenda kunywa kahawa na soda, wengine ndiyo huwa vitu vyao vya kwanza kutia tumboni kila asubuhi. Vinywaji hivyo hukausha maji mwilini na hivyo kupunguza nishati ya mwili. Tunashauriwa kunywa maji ya kutosha kila siku ambayo ndiyo msingi mkubwa wa kuupa mwili nguvu na kusaidia usagaji mzuri wa chakula tumboni.

SAFISHA TUMBO
Njia nyingine bora ya kuwa na utumbo msafi ni kusafisha utumbo mpana kwa njia ya ‘enema’, hasa kwa wale wenye matatizo sugu na ya muda mrefu ya kutopata choo. Enema siyo tu husafisha utumbo, bali huondoa hadi sumu mwilini na kuufanya mwili wako kuwa huru na maradhi mbalimbali.

Ili kujua mwenendo wa utumbo wako, unapaswa kufuatilia haja zako. Kwa kawaida mtu anayekula mlo wake wa kila siku kawaida, anapswa kwenda haja chapo mara moja kwa siku na mara nying huwa kila baada ya kula.

Iwapo unakula milo yote mitatu kila siku lakini hupati choo kwa siku mbili hadi 3, elewa kabisa una matatizo makubwa ya kiafya, kama hayajajitokeza yako njiani. Kwa hali hiyo, huna budi kufanya kila uwezalo uondoklane na tatizo hilo upate choo kama kawaida, tena cha kutosha.
(kumradhi wasomaji wangu kwa kuchelewa wiki hii kupost makala yenu, nilipitiwa)

IJUMAA SHOWBIZ!

MWANA FA WASHKAJI ULAYA MAISHA MAGUMU
Siku chache baada ya kudondoka kutoka pande za Uingereza anakopiga kitabu, mkali wa Bongo Flava, Hamis Mwinjuma a.k.a Mwana FA amesema na ShowBiz amejionea kwa macho yake baadhi ya watu wanaoishi huko wakitaabika bila kuwa na ishu ya kufanya.

Msanii huyo alisema kwamba, baadhi ya vijana wengi bado wana ndoto za kwenda Ulaya wakidhani kwamba maisha ni rahisi kitu ambacho siyo cha kweli kwakuwa huko pia wapo watu wengi wasiokuwa na ajira wanasota mitaani.

“Ulaya maisha magumu washkaji, mtu kama una dili yako ya kupata miambili miambili Bongo bora utulie uendelee kuongeza kipato na kuijenga nchi yako badala ya kukimbilia Ulaya. Ninachoongea watu wanaweza wasiniamini lakini anayeweza aende akajionee mwenyewe,” alisema FA ambaye hivi sasa anafanya vyema na ngoma yake mpya, ‘Nazeeka sasa’ iliyowashirikisha Prof. Jay na Sugu.

Akiizungumzia picha ya Rais Kikwete iliyopo katika baadhi ya tisheti zake (kama anavyoonekana pichani), Hamisi alisema kwamba, hivi sasa ameamua kuachana na ujinga wa kuvaa nguo zenye picha za mastaa wa Ulaya wakati yeye ni Mbongo. “Yaani mimi namfagilia sana JK kuliko Rais yeyote duniani kwa kuwa ni mzalendo wa kweli. Kwangu mimi Kikwete wa kwanza halafu anafuata Obama,” alisema FA.

Aidha, mchizi aliiambia safu kuwa, mwishoni mwa mwezi huu atarudi Uingereza kwa ajili ya kumalizia masomo yake ambapo anatarajia kukusanya mafaili yake na kurudi Bongo Desemba mwaka huu akiwa na Masters yake.
*************

KR, TEMBA, CHEGGE WAKWEA PIPA
Wasanii watatu waliopo ndani ya Kundi la TMK Wanaume Family, Rashid Ziada ‘KR’, Amani Abas ‘Mh. Temba’ na Said Juma ‘Chegge’ katikati ya wiki hii walikwea pipa na kuruka pande za Liberia kwa ajili ya kupiga shoo kadhaa kunako tamasha la amani lililoandaliwa na serikali ya nchi hiyo.

Akipiga stori na Showbiz muda mchache kabla wasanii hao hawajapaa angani, Meneja wa kundi hilo, Said Fella alisema kwamba kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao wameamua kwenda wasanii hao watatu kwa ajili ya kuliwakilisha kundi zima na Tanzania kwa ujumla katika mwaliko huo rasmi.

“Kutokana na bajeti ya waandaaji imebidi waondoke watatu tu, lakini hakijaharibika kitu kwakuwa naamini watatuwakilisha sote na Tanzania kwa ujumla,” alisema Fella. Tamasha hilo la amani Liberia limefanyika juzi na wasanii hao wanatarajia kudondoka Bongo kesho Jumamosi kwa ajili ya kujiandaa na ziara yao ya pamoja na kundi la Tip Top Connection itakayoanza Aprili 24, mwaka huu Sumbawanga, mkoani Rukwa.
******
Tolywood Kuibua vipaji zaidi ya 30, riheso kuanza wiki ijayo
Lile shindano la kutafuta vipaji vitakavyoshiriki kwenye filamu mpya za Kampuni ya Tollywood ‘Movie Star Scouting’ limeingia kunako hatua nyingine ya kupendeza zaidi.

Akipiga stori na safu hii Mkurugenzi wa filamu ndani ya kampuni hiyo, Hamie Rajab alisema kwamba, baada ya usaili uliofanyika Dar es Salaam hivi karibuni wamefanikiwa kupata vipaji kadhaa ambavyo vitaanza kufanyiwa lieso (mazoezi) wiki ijayo.

“Tumepata zaidi ya wasanii 30 ambao tutaanza nao mazoezi Jumatatu ya wiki ijayo katika sehemu ambayo tutaijata hivi karibuni kabla ya kuanza shughuli kubwa ya upigaji picha wa filamu ya ‘Tears On Valentine Day’ ambayo mpaka mwishoni mwa waka huu inatakiwa iwe imekamilika,” alisema Rajab.

Aidha, Mkurugenzi huyo alisema kwamba, mbali na wasanii hao wapya muvi hiyo pia itawapa shavu mastaa wa maigizo kama Steven Kanumba, Vicent Kigosi ‘Ray’ (pichani), Blandina Chagula ‘Johari’, Jokate Mwigelo na wengine kibao.
***********
JINI KABULA NDANI YA HOSTEL YA CHUZI
Staa wa maigizo na muvi za Kibongo, kutoka ndani ya indastri ya muvi za Kibongo, Mariam Jolwa a.k.a Jini Kabula (anayeonekana katika pozi hapo uu) ni miongoni wa wasanii waliopo ndani ya filamu ya Hostel iliyodondoka kitaani hivi karibuni chini ya maandalizi yake, Tuesday Kihangala ‘Mr. Chuzi’.

Kwa mujibu wa muandaaji, muvi hiyo ambayo imetoka chini ya Kampuni ya Tuesday Entertainment, mastaa wengine wanaopatikana ndani ya filamu hiyo ni pamoja na Mohamed Mwikongi ‘Frank’, Aunt Ezekiel, Ahmed Olutu ‘Mzee Chilo’ na wengine kibao.

“Muvi hiyo ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa filamu za Kibongo imetoka ikiwa kwenye DVD, VCD na VHS. Tunashukuru inaendelea kufanya vizuri sokoni, hiyo inaonesha ni jinsi gani hivi sasa Watanzania walivyokuwa na muamko wa kuthamini vitu vya nyumbani,” alisema Chuzi.
********

Ijumaa Sexiest Barchelor inakuja
Shindano la ukweli lililowahi kuwavutia mashabiki wengi, Ijumaa Sexiest Barchelor linaloandaliwa na gazeti hili linakuja tena kwa kasi ya ajabu. Ili kuwapata mastaa wa kiume ambao watashiriki kwenye mpambano huo, wewe msomaji na mpenzi wa shindano hilo unahusika.

Unachotakiwa kufanya ni kututumia jina la staa wa kiume ambaye unadhani anastahili kuingia kwenye mpambano huo utakaoanza hivi karibuni. Andika ujumbe mfupi (SMS) ukilitaja jina hilo kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173.
*****

MKALI WA MWEZI (MONTHLY BEST PERFORMER
Kupitia shindano hili, ‘Mkali wa mwezi’ leo tunashuka na majina kumi ya mastaa mbalimbali wa Kibongo waliotajwa kuwania nafasi moja ya ushindi.

Kwa mujibu wa kura za wasomaji na wapenzi wa mpambano huu, mastaa hao ni Kanumba, Ngwea, Yusuph Mlela, Marlaw, Chid Benz, Ray C, Madee, Mrisho Ngassa, TID na Mrisho Mpoto.

Mpira unarudi kwako ‘jaji’ ambaye ni wewe msomaji, unadhani kati ya hawa nani anastahili kuwa mkali wa mwezi huu wa Julai? Tutumie ujumbe mfupi kupitia simu namba 0787-110 173, e-mail:mcgeorge2008@gmail.com.
***********
compiled by mc george

Wednesday, July 15, 2009

Je ni kweli Muziki wa Bongo Fleva Unakaribia Kupoteza Utamu Wake?


KUANZIA mwanzoni mwa miaka ya 2000, ubongo wa wa vijana wengi wa Tanzania ulikuwa umejaa muziki wa Bongo Fleva. Unapowaona wamekaa vijana zaidi ya mmoja, basi mazungumzo yao yalikuwa ni juu ya muziki huo. Hata mavazi yao, matamshi yao yalikuwa ni ya kibongo fleva. Suruali kubwa inayoacha makalio wazi, fulana kubwa na hereni kifuani. Hiyo ndiyo ilikuwa staili ya kukuonyesha kuwa wewe ni mwana BongoFleva. Lakini wakati muziki huo unachukua chati, mwanamuziki mkongwe na kiongozi wa bendi ya Msondo Ngoma, Muhidin Gurumo 'Mjomba' alisema kuwa muziki huo ni sawa na Big G itafika kipindi utaanza kupoteza utamu.

Katika miaka ya hivi karibuni maneno hayo ya Gurumo kama yanaanza kutoa mwanga, kwani hali iliyouwa awali katika muziki huo inaanza kupotea. Muziki huo umeanza kupoteza umaarufu wake kwenye vinywa vya vijana. Wengi waliokuwa na ndoto ya kuwa wasanii wa Bongo Fleva wameanza kurudi nyuma, huku wengi wao walioingia wanatoka. Mavazi ya kibongofleva na swing (miondoko) ya kibongofleva yamepotea na wale ambao waliyatoa mawazo yao shuleni, sasa wameanza kuyarudisha. Je ni kweli Muziki wa Bongo Fleva Unakaribia Kupoteza Utamu Wake? Joseph Haule 'Profesa Jay' na Ambwene Yesaya 'AY' wanajibu swali hilo.

Gonga link hii kupata jibu la swali hilo: nifahamishe.com

Monday, July 13, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!



La-Toya: Dada’ake Michael Jackson, Amewahi kupiga picha kibao za utupu na kujiachia na midume minne
Ebwana dah! Leo inamcheki dada’ke King of Pop duniani, Michael Jackson aliyefariki dunia hivi karibuni, huyu si mwingine bali ni mwanamuziki, mwanamitindo na mcheza filamu La-Toya Jackson aliyetupambia safu hii kwa picha za ukweli.
Baada ya kifo cha kaka yake, mashabiki wengi Bongo wamekuwa wakitamani kujua mengi kuhusu ndugu zake waliobaki, na ndiyo sababu iliyotufanya sisi Abby Cool & MC George over the weekend kuzama mtandaoni na kuibua ishu kibao kuhusu Latoya wakikiwemo mastaa wa kiume aliowahi kujihusiaha nao kimapenzi.

Kwa mujibu wa mtandao unaodili na ishu za uhusiano, kwa nyakati tofauti La-Toya amewahi kujiachia na wanaume wanne ambao ni mwanamuziki mkongwe Chuck Berry ambaye nyota yake ni Punda, David Gest, Jack Gordon na Prince, mwanamuziki ambaye aliwahi kudondoshewa skendo ya ushoga.

Kama ulikuwa haufahamu, La-Toya ambaye hivi sasa ameenda eji, akiwa anamiliki umri wa miaka 53 aliwahi kupiga picha kibao za utupu kwa ajili ya kupamba jarida maarufu la Marekani, Playboy la 1989 (kama anavyoonekana katika hizo ndogo hapo juu), wakati huo akiwa ni mrembo mwenye umri wa miaka 33 tu.

Katika game ya muziki, La-Toya aliweza kukamata chati mbalimbali na ngoma zake kadhaa ukiwemo ‘If You Feel the Funk’ ambao ulifunika katika Billborad kwenye miaka ya 1980, huku akidondoka na albamu kadhaa. Hadi hii leo bado anaendelea kupiga shoo za hapa na pale japokuwa siyo kivile.

Akiwa na macho na nywele zenye rangi ya Dark Brown, msanii huyo alizaliwa kwa jina la LaToya Yvonne Jackson katika eneo la Gary, Indiana, Marekani.
**************************
Papii Kocha akabidhi mikoba ya albamu yake kwa Shigongo
Aliyekuwa rapa namba moja wa Bendi ya FM Academia, Francis Nguza a.k.a Papii Kocha mtoto wa mfalme ambaye sasa anatumikia kifungo cha maisha katika Gereza la Ukonga, Dar es Salaam, amemwomba Mkurugenzi wa Global Publishers & General Enterprises Ltd, Eric Shigongo kuwa msimamizi wa albumu yake ya Salima.

Msanii huyo ambaye alihukumiwa baada ya kukutwa na hatia ya kushirikiana na baba yake pamoja na ndugu wawili kuwalawiti watoto, amefikia hatua hiyo baada ya kuona hapati faida ya kazi yake hiyo kutokana na kukosa mawasiliano mazuri na msimamizi wake wa awali.

Kwa mujibu wa barua aliyoandika Papii na kupigwa mhuri wa Mkuu wa Gereza la Ukonga, msanii huyo anasema kwamba amelazimika kumwomba Shigongo asimamie kazi yake hiyo kwasababu anaamini kuwa haki yake itapatikana hasa baada ya albamu hiyo kufanya vizuri sokoni.

Mbali na ombi hilo kwa Shigongo, msanii huyo pia ameomba kupewa fedha za mauzo ya wimbo wake “Seya” ambao ulitangazwa kushika namba moja kati ya nyimbo 50 za kituo cha Radio Clouds FM.

Alimalizia kwa kumuomba msimamizi wake wa awali kumpa ushirikiano wote Shigongo ili afanikiwe kupata haki yake ambayo ameifanyia kazi.

Album ya Salima ilitoka kati ya mwaka 2003/2004 ikiwa na ngoma zilizotamba kama Salima wenyewe, Fanta, Seya na nyinginezo kibao.
******************

20%: life ya mashindano kwangu no!
Staa wa Bongo Flava asiyependa makuu, Hamisi Kinzasa a.k.a 20% amesema na safu hii kwamba baada ya kuhamishia makazi yake town (Dar es Salaam) akitokea Kimanzichana, Pwani iliko familia yake alidondoka pande za Keinyama, lakini baada ya kugundua mitaa hiyo mastaa wengi wanaishi kwa mashindano ameamua kuhamia Kigamboni.

“Kwa upande wangu maisha ya kushindano no, huwa napenda niishi nitakavyo siyo kama walivyo wengine, akimuona fulani ana staleti naye anataka awe nayo au akiona huyu ana kile naye pia anataka awe nacho,” alisema staa huyo wa Money Money, Mama Neema na ngoma nyingine kali.
******************

Hostel ya Mr. Chuzi, Aunt Ezekiel kitaani
Kutoka ndani ya indastri ya muvi za Kibongo, safu hii ilidondoshewa ishu kwamba, ile filamu ya Hostel iliyogongwa na mastaa mbalimbali wanaofanya vyema katika game hiyo tayari imedondoka kitaani kupitia Kampuni ya Tuesday Entertainment.

Ndani ya safu hii, mwandaaji wa muvi hiyo, Tuesday Kihangala ‘Mr. Chuzi’ alisema kwamba, filamu hiyo ambayo ilikuwa inasubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa fani hiyo nchini imeingia kitaani ikiwa katika DVD, VCD na VHS.

“Baadhi ya wasanii walioshiriki kwenye filamu hiyo ni pamoja na Mohamed Mwikongi ‘Frank’, Aunt Ezekiel, Ahmed Olutu ‘Mzee Chilo’, Mariam Jolwa ‘Jini Kabula na wengine wengi,” alisema Chuzi.
***************

Tollywood: Usaili mikoani baadaye
Kutoka ndani ya Kampuni ya Tollywood Movies waliyosimama vyema kuitetea sanaa ya filamu za Kibongo, safu hii imeambiwa kwamba, kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao wameamua kusitisha zoezi la usaili kwa wasanii wa mikoa ya Morogoro, Tanga, Arusha, Mwanza na Visiwani Zanzibar waliyojaza fomu kwa ajili ya kushiriki kwenye muvi mpya zinazotarajiwa kuandaliwa na kampuni hiyo ikiwemo ‘Tears On Valentine Day’.

Ndani ya safu hii Mkurugenzi wa Filamu ndani ya kampuni hiyo, Hamie Rajabu alisema kwamba kutokana na hilo wanawaomba radhi wasanii wote kwa usumbufu waliyoupata wakati wa zoezi la kujaza fomu kwa ajili ya kushiriki kwenye filamu hizo.

“Sisi kama Tollywood tumesikitishwa na hilo, tunawaomba radhi wale wote waliyopoteza muda wao kwa kwenda kwenye vituo vyetu kwa ajili ya kujaza fomu za ushiriki. Lakini pamoja na yote hayo tunawaahidi kwamba, tunajipanga vizuri kabla ya kuendelea na zoezi hilo kwa siku ambayo tutaitangaza kupitia vyombo vya habari yakiwemo magazeti yanayochapishwa na Kampuni ya Global Publishers,” alisema Hamie.

Aidha, mkurugenzi huyo alisema kwamba, katika filamu hizo mbili watawatumia wasanii zaidi ya 30 watakaofanikiwa kupita katika usaili uliyofanyika, Dar es Salaam hivi karibuni.
****************************
compiled by mc george

Sunday, July 12, 2009

VACANT APARTMENTS AT MBEZI



TWO APARTMENTS STILL VACANT, EACH WITH ONE MASTER BED ROOM, ONE BED ROOM, KITCHEN, TOILET, STORE AND A SITTING ROOM, AT MBEZI SALASALA DAR ES SALAAM. IF YOU ARE LOOKING FOR A NICER, QUITE AND SECURE PLACE, THEN JUST CALL:
+255 754 692 595

IRENE NA NDOA YAKE!

Irene anakuwa staa wa kwanza Bongo kufunga ndoa kwa staili hii na kujiwekea ka historia kake, cheki picha zaidi hapa: globalpublisherstz.com

Saturday, July 11, 2009

Ukipenda sana kompyuta...



Kila kitu kipende kwa wastani, ukizidisha unakuwa addicted kiasi hiki...
cheki zaidi hapa: NIFAHAMISHE.COM

Friday, July 10, 2009

IJUMAA SHOWBIZ!

TUNDA & SPARK WAUNGANA NA TMK FAMILY
Ishu mpya iliyotua ndani ya ShowBiz kutoka pande za Temeke na Manzese, Dar es Salaam inasema kwamba, makundi mawili yaliyopo kunako game ya muziki wa kizazi kipya, TMK Wanaume Family na Tip Top Connection yameungana na kuamua kupiga kazi pamoja huku wasanii Tundaman, Spark, Madee, Z-Anto, Kassim, Chegge, Temba, KR, Stiko na wengine wakionesha kufurahia ‘idea’ hiyo.

Baada ya kusikia uvumi huo, safu ilimtafuta kiongozi wa TMK, Said Fella ambaye alisema: “Yeah, ni kweli tumeungana na kuamua kupiga kazi pamoja kwa sababu tunaamini siku zote umoja ni nguvu, ukizingatia kwamba tangu zamani mimi na Abdul Bonge wa Tip Top ni kama mtu na mdogo wake.

“Tulichofanya baada ya kuungana ni kurekodi ngoma ya pamoja yenye jina la ‘Chama Kubwa’ ambayo inatambulisha muungano huo na siku chache zijazo tutaanza ziara katika mikoa mbalimbali kwa ajili ya kuutambulisha umoja wetu. Hatujaishia kwenye kazi hiyo tu, hivi sasa tupo kwenye hatua za mwisho kukamilisha albamu ya pamoja.”

Kwa upande wa uongozi wa Tip Top, safu hii ilipiga stori na Babu Tale ambaye alisema: “Sisi tumeupokea muungano huo kwa mikono miwili kwa kuwa tunaamini nguvu yake itakuwa kubwa, ili kukuhakikishia hilo ntakuletea kazi ya pamoja ‘Chama Kubwa’ ili usikie vijana walivyofanya kazi. Tunatarajia kuanza ziara ya pamoja Julai 24, mwaka huu Sumbawanga, Rukwa, baadaye Mbeya na Iringa itafuata.”
***********
USHER RAYMOND: KILICHOMLIZA MBELE YA JENEZA LA MICHAELJACKSON
Miongoni mwa mastaa wa Marekani waliotokwa na machozi wakati wa zoezo la kumuaga mfalme wa Pop, Michael Jackson ni pamoja na Usher Raymond ambaye kuna wakati alishindwa kuendelea kuimba kabla hajakumbatiwa na ndugu wa Michael ambao walimfariji.

Baada ya tukio hilo, ShowBiz ilifanya uchunguzi na kugundua kwamba ukaribu aliokuwa nao Usher kwa Michael ni mkubwa zaidi na kwamba hata staili ya kucheza anayotumia stejini aliikopi kwa nyota huyo ambaye alizimika ghafla wiki mbili zilizopita.

Kwa mujibu wa mtandao, Usher alikuwa akipata ushauri wa kutosha kuhusu muziki kutoka kwa Michael na hata katika baadhi ya shoo za mkali huyo wa Pop, mchizi alipanda stejini na kupiga kazi ambazo zilimfanya marehemu amkumbatie na kumpongeza huku akimpa moyo kwamba, baadae atakuwa mkali wa dunia katika kucheza.

Inawezekana hayo na mengine mengi ndiyo vitu vilivyomfanya Usher aibuke mafichoni alipokuwa amejichimbia na kuungana na umati wa watu na mastaa mbalimbali katika zoezi la kumuaga Michael Jackson lililofanyika katikati ya wiki hii, Los Angeles, Marekani, kabla hajapanda jukwaani na kumwaga machozi wakati akiimba.
**********

USAILI WASANII WA MUVI MIKOANI WASITISHWA
Kutoka ndani ya Kampuni ya Tollywood ambayo ni waandaaji wa filamu za ukweli nchini, ShowBiz imedondoshewa ishu kwamba kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao, wameshindwa kuendelea na zoezi la usaili kwa wasanii wa mikoa ya Morogoro, Tanga, Arusha, Mwanza na Kisiwa cha Zanzibar kwa ajili ya kupata wasanii watakaoshiriki kwenye muvi mpya zinazotarajiwa kuandaliwa ikiwemo ‘Tears On Valentine Day’.

Akipiga stori na ShowBiz, Mkurugenzi wa Filamu ndani ya kampuni hiyo, Hamie Rajabu alisema kwamba, kutokana na hilo wanawaomba radhi wasanii wote waliojitokeza kujaza fomu kwa usumbufu walioupata, lakini wakaahidi kurudia zoezi hilo baada ya kurekebisha tatizo lililojitokeza.

“Sisi kama Tollywood tunawaomba radhi wasanii wote waliojitokeza kujaza fomu, kinachoendelea kufanyika kwa sasa tunawapigia simu wahusika wote na kuwaita katika vituo walivyochukulia fomu kisha kuwarudishia pesa zao, hata wale ambao simu zao hazipatikani kama watapata nafasi ya kusoma gazetini waende walipojazia fomu ili warudishiwe pesa zao,” alisema Hamie Rajab.

Aidha, mkurugenzi huyo alisema kwamba, wanatarajia kuwapata vijana zaidi ya 30 ambao walishiriki katika zoezo hilo Dar es Salaam na siku kadhaa zijazo watawapigia simu mmoja baada ya mwingine, hususan wale waliofanya vizuri kwenye usaili ambao ulifanyika katika ofisi za Tollywood wiki mbili zilizopita.
********
MKALI WA MWEZI (MONTHLY BEST PERFORMER
Majina 10 ya mastaa wa Bongo yanaoyoendelea kutajwa kuwania ushindi wa mwezi (Mkali wa mwezi) kunako mpambano huu yatatajwa wiki ijayo, kisha wewe msomaji utapata fursa nyingi ya kudondosha kura yako ukimtaja mmoja ambaye unadhani anastahili kuwa mshindi wa mwezi huu wa Julai.

Kabla ya kuyataja majina hayo, ShowBiz inakupa nafasi ya mwisho wiki hii kutuma jina la staa ambaye unadhani anastaili kuwa bingwa. Tutumie SMS kupitia simu namba 0787-110 173. E-mail:mcgeorge@gmail.com.
***********

Ijumaa Sexiest Barchelor inakuja
Shindano la ukweli lililowahi kuwavutia mashabiki wengi, Ijumaa Sexiest Barchelor linaloandaliwa na gazeti hili linakuja tena kwa kasi ya ajabu. Ili kuwapata mastaa wa kiume ambao watashiriki kwenye mpambano huo wewe msomaji na mpenzi wa shindano hilo unahusika.

Unachotakiwa kufanya ni kututumia jina la staa wa kiume ambaye unadhani anastahili kuingia kwenye mpambano huo utakaoanza hivi karibuni. Andika ujumbe mfupi (SMS) ukilitaja jina hilo kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173.
_____
Compiled by mc george

Wednesday, July 8, 2009

BAADA YA KIFO MENGI HUSEMWA!




Mtu anapokufa mengi husemwa, kama ilivyo kwa Michael hivi sasa, anatafutwa 'mchawi' kama lilivyoripoti jarida la Life & style la Marekani kuwa kuna mtu alimpa dawa za sumu Michael ili afe na kuchukua mamilioni yake..pia aliyekuwa mtaalamu wake wa ngozi Dr. Anold klein amenyooshewa kidole na familia ya Michael kuwa ndiyo chanzo kwa kumpa madawa bila mpangilio na inadaiwa kuwa Michael alikuwa anakula kiasi cha vidoge 50 kwa siku!!! Hata hivyo katika cheti chake cha kifo kilichotolewa hakijaonesha sababu halisi ya kifo chake...inasubiriwa ripoti kamili ili kujua chanzo cha kifo chake hasa..!!