Tuesday, December 2, 2008
NGOJA NIWAPE HAI WADAU!
BAADA YA KULA USIFANYE MAMBO HAYA SABA!
Mwili ni kama gari au chombo chochote cha moto, ambacho ili kifanye kazi kama kilivyokusudiwa, lazima mtumiaji afuate maelezo ya kukitumia chombo hicho. Katika makala ya leo tutaangalia mambo saba ambayo mtu hatakiwi kuyafanya mara baada ya kula chakula. Katika makala haya tutayajua mambo hayo na kuona sababu za kukatazwa kwake.USIVUTE SIGARA
Ni dhahiri kuwa sigara ina madhara kiafya, kwa ujumla wake watu wanashauriwa kuacha kutumia. Lakini inaelezwa kuwa madhara yake huongezeka mara kumi iwapo mvutaji atavuta mara baada ya kula chakula. Utafiti wa kimaabara unaonesha kuwa ukivuta sigara moja baada ya kula ni sawa na mtu aliyevuta sigara 10, hivyo hatari ya kupata saratani (kansa) huongezeka.
USILE MATUNDA
Katika makala zetu zilizopita kuhusu ulaji sahihi wa matunda, suala hili tuliliongea kwa upana zaidi na leo tunalirudia. Usile matunda baada ya mlo kwani ulaji huo hulifanya tumbo kujaa hewa na matokeo yake kusababisha gesi tumboni. Usahihi ni kula matunda saa moja au mbili kabla au baada ya kula chakula chako. Kula matunda mara baada ya kula chakula ni kosa ambalo linafanywa na watu wengi na huonekana ni sawa.
USINYWE CHAI
Mara baada ya kula chakula, iwe mchana au usiku, usimwe chai. Kwa mujibu wa utafiti, majani ya chai yana kiwango kikubwa cha tindikali (acid), hivyo unapokunywa chai tindikali hiyo hufanya protini iliyo kwenye chakula ulichokula kuwa ngumu na hivyo kutosagika tumboni haraka, matokeo yake ni mtu kukosa choo kwa siku kadhaa.
USILEGEZE MKANDA
Unaweza usilichukulie ‘serious’ jambo hili, lakini ni jambo la hatari kwa mustakabali wa afya ya mtu. Mara baada ya kula, usilegeze mkanda wa suruali yako, uache kama ulivyokuwa hapo awali kwani kwa kufanya hivyo kunaweza kusababisha utumbo kujikunja na kuziba.
USIOGE
Usioge baada ya kula, bali oga kabla ya kula. Inaelezwa kuwa unapooga baada ya kula, mtiririko wa damu huongezeka zaidi sehemu za mikono, miguu na mwili na kusababisha damu kupungua sehemu za tumboni. Damu inapopungua tumboni maana yake ni kudhoofika kwa mfumo wa usagaji chakula tumboni (digestive system).
USIRANDERANDE
Kuna madai kuwa mtu ukila unashauriwa utembee kiasi cha hatua 100 na utaishi miaka 99, lakini kwa maana halisi, dhana hiyo si ya kweli. Utafiti unaonesha kuwa kurandaranda au kutembea tembea mara baada ya kula husababisha mfumo wa usagaji chakula kukosa uwezo wa kunyonya virutubisho vilivyomo kwenye chakula tunavyokula.
USILALE
Usilale muda mfupi tu mara baada ya kula, kwani chakula ulichokula hakitaweza kusagwa sawaswa na huweza kusababisha vidonda vya tumbo na magonjwa mengine ya kuambukiza kwenye utumbo mdogo.
Hayo ni mambo 7 muhimu ya kuzingatia ambayo yapo ndani ya uwezo wa kila mtu anayejali afya yake, hivyo tafadhali tusaidiane kuelimishana masuala haya kwa faida yetu.
Tuonane tena wiki ijayo panapo majaaliwa.
Monday, December 1, 2008
WIKIENDA SHOWBIZ!

Tamasha kubwa la Ukimwi leo
Tamasha kubwa la Ukimwi lililoandaliwa na Kamati ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi ya Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) linafanyika leo ndani ya Uwanja wa Maji Maji mjini Songea huku mgeni rasmi akiwa ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi ‘CCM’, Luteni Yusuph Makamba.
Mratibu wa tamsha hilo, Dk. Ringo Moses alisema na safu hii kwamba maelfu ya wakazi wa Songea, hasa vijana watakaofurika katika tamasha hilo watapata burudani ya kutosha kutoka kwa wasanii kibao wakiwemo Maunda Zorro, Joseph Haule ‘Prof. Jay’, Ruta Bushoke ‘Bushoke’, Herry Samir ‘Mr. Blue’ na wengine kibao wakiwemo wa mjini humo.
“Hili litakuwa ni tamasha la tatu la Ukimwi tangu tulipoanza mwaka 2006, kadri siku zinavyozidi kwenda tunaboresha zaidi, mtu aliyekuwepo kwenye tamasha la kwanza lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club 2006, akija Songea atagundua mabadiliko makubwa, kwani tumeboresha karibu kila sekta,” alisema Dk. Ringo.
Aidha, mratibu huyo alisema kwamba mbali na kupiga shoo ya nguvu, wasanii hao na wadau wengine wanaojihusisha na masuala ya Ukimwi watatoa mada mbalimbali kuhusiana na gonjwa hilo hatari. “Tunawaomba wananchi wa Songea, hasa vijana wajitokeze kwa wingi ndani ya Uwanja wa Maji Maji ili waweze kubadilishana mawazo na wasanii pamoja na viongozi mbalimbali wa kitaifa, hilo nadhani linawezekana kwasababu kiingilio ni bure,” alisema Dk. Ringo.
***************************
Likizo Tyme: Shoo kubwa wiki hiiIle shoo kubwa ya Likizo Tyme iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa na wapenda burudani nchini itaangushwa Ijumaa ya wiki hii ndani ya viwanja vya Leaders Club, Dar es Salaam na mastaa kibao wa muziki kutoka pande za Marekani na Jamaika.
Mashabiki wa Bongo watapata fursa ya kuwashuhudia lauvu na kujirusha na mastaa wa muziki kutoka Marekani kama Joe Thomas na kundi zima la Boyz II Men, huku Tanto Metro & Devonte na Tanya Stephens kutoka Jamaika wakiangusha ma-dancehall ya kutosha.
Waandaaji wa tamasha hilo, Kampuni ya Entertainment Masters (EM), wamesema katika taarifa yao kuwa maandalizi yote yako sawa ikiwemo wasanii hao kutamka kupitia luninga kuwa ni kweli wako njiani kudondoka ‘Tzee’. Kwa upande mwingine steji zitaanza kuvamiwa majira ya saa moja usiku, huku mashabiki wakizama ndani kwa viingilio vya shilingi lakini moja (VIP A), elfu hamsini (VIP B) na elfu ishirini sehemu ya kawaida.
“Hiyo ni kwa wale watakaokata tiketi zao mapema, watakaokatia getini siku ya tamasha watalipa shilingi lakini moja na elfu ishirini (VIP A), Elfu sitini (VIP B) na elfu thelathini, kawaida. Niimani yetu kwamba wewe mpenda burudani na shabiki utakuwa wakati wako wa kujiachia na mastaa hao”, walisema waandaaji.
*************************************
Naomi Campbell: Hii ni too much, midume zaidi ya 40!Ebwana Dah! Kutoka kunako mtandao wa ‘intaneti’ unaodili na uhusiano wa kimapenzi wa mastaa mbaliombali wa kiwanja tunaambiwa kwamba, mwanamitindo maarufu dunia, Naomi Campbell amewahi kujiachia na mastaa wa kiume zaidi ya 40, hii sasa ‘tu machi’.
Kwa mujibu wa mtandao huo, akiwa na umri wa miaka 38 hivi sasa Naomi amewahi kuwa na uhusiano na David Evans, Enrique Palacio, Francesco Carrozzini, Gabriel Byrne, Guy Laliberte, Johnny Depp, Kermit Nasser, Kevin Costner, Lewis Hamilton, Luca Orlandini, Marcus Elias na Muhammad Al Habtoor.
Wengine ni Pedro Diniz, Robert Goode, Sean Kanan, Sean Penn, Sergio Marone, Sylvester Stallone (Rambo), Joaquin Cortes, Mike Tyson mwaka 1987 - 88, Robert De Niro (1991 - 92), Eric Clapton (1993), Adam Clayton
(1993 - 94), Prince Albert II (1994 - 97), Chris Paciello (1995), Leonardo DiCaprio (1995) na Max Biaggi (1997).
Naomi hakuishia hapo, aliendelea kukandamiza raha na mastaa kama Joaquin Cortez (1997 - 98), Marcus Schenkenberg (1998), Flavio Briatore (1998 - 03), Joseph Fiennes (2000 - 01), Robbie Williams (2001),
Damon Dash (2001), Doug Band (2002), Puff Daddy (2002 - 03), Colin Farrell (2002), Matteo Marzotto (2003 - 05), Tommy Lee (2004), Usher Raymond (2004), Badr Jafar (2005 - 06) na Rolando Pintos (2007),
Pia Naomi alijiachia na Terrence Howard (2007), Gerard Butler (2007), Andre Balazs (2007), Hugo Chavez (2007),
Vladislav Doronin ambaye ndiyo yuko naye hivi sasa. Je, akitoka hapo atadondokea kwa dume gani? Ebwana Dah! Naomi anatisha.
Sunday, November 30, 2008
WIKI YA MRAMBA ILIVYOISHA!
Wiki hii ilikuwa ni ya Basil Mramb na Daniel Yona kutamba mahakamani kwa ubadhirifu..na wakati huo huo Mramba kutawala zaidi kwenye media baada ya kuwepo kwa harusi ya binti yake aliyeolewa Jumamosi hii katika kanisa la Mt. Petro (St. Peter) Oysterbay jijini Dar es salaam...alikuwa ahudhurie harusi hiyo lakini ikashindikana baada ya dhamana yake kukwama hivyo kulazimika kuendelea kunyea debe Keko kwa wikiendi nzima!!!
Saturday, November 29, 2008
Aliyekatika mikono akamatwa akinyonga usukani kwa miguu

Polisi mjini Beijing China, walipigwa na butwaa baada ya kukuta dereva waliyemsimamisha hana mikono na alikuwa akinyonga usukani kwa kutumia miguu...kwa full news nenda NIFAHAMISHE.COM
Friday, November 28, 2008
SHAMBULIO LA MUMBAI NI BALAA
Hali ilivyokuwa mara baada ya milipuko iliyofanywa na magaidi mjini Mumbai katika hoteli ya kitalii ya Taj
Asakari polisi akimsindikiza babu kupita katikati ya kituo cha reli baada ya shambulio la kigaidi liliofanyika mjini Mumbai, India. hadi sasa zaidi ya watu 120 wameripotiwa kuuawa.
IJUMAA SHOWBIZ!
Blue
Prof JayTamasha la Ukimwi 2008: Songea kaeni tayari kwa shoo
Kamati ya Taifa ya kudhibiti Ukimwi ya Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) inawaletea bonge la tamasha ambalo litawashirikisha wasanii maarufu wa muziki wa kizazi kipya, Joseph haule Prof. Jay’, Ruta Bushoke ‘Bushoke’, Herry Samir ‘Mr. Blue’ na wengine kibao, litakalopigwa Desemba 1, mwaka huu ndani ya Uwanja wa Maji Maji mjini Songea.
Mratibu wa shughuli hiyo, Dk. Ringo Moses alisema kwamba tamasha hilo ambalo hufanyika kila mwaka katika mikoa tofauti, mwaka huu litakuwa la aina yake kutokana na maandalizi kuwa makubwa zaidi tofauti na miaka iliyopita.
“Tunataka kila mwaka liwe tofauti kwa kuongeza vitu vipya, mbali na wasanii hao wa muziki wa kizazi kipya pia tutakuwa na wasanii wengine wengi wakiwemo wa sanaa za maigizo na nyimbo za injili ambao mbali na kutoa burudani pia wataongea na maelfu ya vijana watakaofurika siku hiyo kuhusiana na gonjwa hatari la Ukimwi,”.
Aidha mtaribu huyo alisema kwamba, Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi ‘CCM’, Luteni Yusuph Makamba ndiyo amepewa heshima ya kuwa mgeni rasmi siku hiyo. Mbali na Makamba viongozi wengine wengi wa Serikani watakuwepo kwa ajili ya kuongea na wananchi wa Songea.
“Tunawaomba wananchi wa Songea, hasa vijana wajitokeze kwa wingi ndani ya Uwanja wa Maji Maji ili waweze kubadilishana mawazo na wasanii pamoja na viongozi mbalimbali wa kitaifa, hilo nadhani linawezekana kwasababu kiingilio ni bure,” alisema Dk. Ringo.
***************************************************88
Mshindi kutajwa wiki ijayo
Tukiwa tunaelekea ukingoni mwa mpambano wa kumtafuta Ijumaa King Of Hip Hop, wasomaji na mashabiki wengi wanashahuku ya kutaka kufahamu kati ya mastaa hawa watatu, Prof. Jay, Johmakini na Fid Q waliyoingia kwenye tatu bora nani ataibuka na ushindi.
Kauli kutoka kwa mratibu wa shindano hilo, Charles Mateso, mshindi atatangazwa wiki ijayo kupitia safu hii baada ya zoezi kubwa la kuhesabu kura kukamilika. Unafikiri ni nani atalamba U-King huo? Cheki na sisi wiki ijayo.
********************************************************8
TMK Family: Kumpongeza Obama KenyaBaada ya kukamilisha ziara katika Mikoa ya Kusini mwishoni mwa wiki iliyopita kundi la muziki wa kizazi kipya, TMK Wanaume Family linatarajia kuungana na maelfu ya wananchi wa Kenya kunako tamasha kubwa la Kumpongeza Rais mteule wa Marekani, Barack Obama, Hawa Mkombozi anadondoka nayo.
Akipiga stori na safu hii, kiongozi wa kundi hilo Said Fella alitamka kwamba, tamasha hilo litafanyika Desemba 6, mwaka huu jijini Nairobi na kwamba wamepata dili hiyo baada ya kazi zao nyingi kufanya vyema karibu Afrika mashariki nzima.
“Sijafahamu vizuri tutakuwa na wasanii gani wengine, lakini tumeambiwa ni tamasha la kumpongeza Rais wa Marekani, Barack Obama ambalo litafanyika uwanjani. Ubora wa kazi zetu ndiyo umetufanya tupate mwaliko huo maalum,” alisema Fella.
Wakiwa katika Mikoa ya Kusini, TMK Family walifanikiwa kupiga shoo sehemu mbalimbali kama Newala, Masasi, Nachingwea, Liwale, Mtwara na Lindi ambako pia walitoa misaada kama chandalua, nepi za watoto na unga wa ulezi kwenye wodi ya wazazi katika Hospitali ya Sokoine. Safu hii inatoa pongezi kwa kundi hilo, ni mfano wa kuigwa na wasanii wengine.
Thursday, November 27, 2008
MR. AWORI CEO MPYA STANDARD CHARTER
Tuesday, November 25, 2008
JIKINGE NA MARADHI KWA KULA NANASI

Mzimu wa mananasi umeshawadia katika ukanda wote wa pwani. Katika msimu huu bei ya nanasi nalo hushuka na kuwa katika bei ambayo mtu yeyote anaweza kuimudu bila shaka. Hivyo asiyekula mananasi ya kutosha mpaka msimu unaisha, huyo ana hasara kubwa katika afya yake. Ukiacha ukweli huo, tunda hili lina faida ambazo linashawishi kila mtu kulitumia.
Faida zinazoweza kupatikana kwenye nanasi ni nyingi ambazo zinaweza kuwa kama kinga na tiba kwa baadhi ya matatizo ya kiafya ambayo pengine yangehitaji mtu kwenda hospitali kupatiwa dawa, tena kwa gharama kubwa. Miongoni mwa faida hizo ni hizi zifuatazo:
USAGAJI WA CHAKULA
Nanasi lina virutubisho vinavyouwezesha mfumo wa usagaji chakula tumboni kufanya kazi yake ipasavyo, pindi mfumo huu unapowezeshwa kufanyakazi yake vizuri, mtu huweza kupata choo laini na kwa wakati kama inavyotakiwa. Hivyo wenye kula tunda hili kwa wingi hawawezi kusumbuliwa na taizo la ukosefu wa choo. Aidha, kwa mujibu wa tafiti nyingine, nanasi pia lina virutubisho vyenye uwezo wa kupunguza au kuzuia uvimbe tumboni.
KINGA YA MWILI
Nanasi linaaminika kuwa miongoni mwa matunda yenye chanzo kizuri cha vitamin C ambayo kazi yake mwilini ni kuupa mwili kinga dhidi ya ‘wavamizi’ mbalimbali (free radicals), ambao wanapoingia mwilini, kazi yao hua ni kuharibu chembembe hai za mwili. Vile vile ‘wavamizi’ hao wanapoweka makazi mwilini, huziba mishipa ya damu na hivyo kusababisha magonjwa ya moyo na mengine mengi, ikiwomo kansa ya tumbo.
Kwa kuongezea, vitamini C inaaminika kuwa na uwezo mkubwa wa kuimarisha mfumo wa kinga ya mwili, hivyo kuifanya kuwa kinga ya magonjwa madogo madogo kama vile mafua, kikohozi, homa na maambukizi mengine. Unapokuwa na kiwango cha kutosha cha vitamin hiyo, bila shaka kinga yako ya mwili itakuwa imeimarika na hivyo utakuwa umejiepusha na maambukizi mbalimbali.
CHANZO CHA MADINI
Mbali ya kuwa ni chanzo kizuri cha vitamin C, nanasi pia ni chanzo kizuri cha madini aina ya ‘manganese’ ambayo yanaaminika kuwa na uwezo wa kuboresha ufanisi wa vimeng’enyo mbalimbali vya mwili, vikiwemo vya kuzalisha nishati na kinga ya mwili. Halikadhalika tunda hili lina kiwango cha kutosha cha vitamin B1 (thiamin).
KUIMARISHA NURU YA MACHO
Inawezekana karoti ikawa ndiyo inayojulikana na watu wengi kuwa na uwezo wa kuimarisha nuru ya macho, lakini nanasi nalo lina uwezo mkubwa wa kuimarisha nuru ya macho. Utafiti unaonesha kuwa ulaji wa tunda hili na matunda mengine, kiasi cha milo mitatu kwa siku, kunaondoa hatari ya kupungua kwa nuru ya macho kwa asilimia 36 kwa watu wazima.
NANASI LILILO BORA
Nanasi lililo bora ni lile kubwa na lililoiva vizuri. Wakati ni kweli kwamba nanasi kubwa lina nyama nyingi kuliko nanasi dogo, lakini hakuna tofauti ya ubora wa virutubisho kati ya nanasi dogo na kubwa, ili-mradi lisiwe limeoza au lenye michubuko mingi. Hivyo chagua nanasi lilioiva vizuri na lenye kunukia.
Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa hivi karibuni na Chuo Kikuu cha Innsbruck, nchini Austria, unasema kuwa tunda linapokuwa limeiva zaidi ndivyo ambavyo virutubisho vyake vinapokuwa bora. Kwa kula nanasi ambalo halijaiva vizuri, huenda ukajikosesha faida zanazopatikana kwenye tunda hilo kama inavyoelezwa.
Mara baada ya nanasi kumenywa na kukatwa vipande, linatakiwa kuliwa mara moja, iwapo litahifadhiwa kwenye jokofu kwa ajili ya kuliwa baadaye, njia sahihi ya kuhifadhi ni kuliweka kwenye chombo chenye mfuniko (container) ili kuhifadhi virutubisho vyake kwa kipindi hadi cha siku tano bila kupoteza ubora wake, ikiwa pamoja na ladha.
Mwisho, unapokula tunda lolote, zingatia usafi. Osha tunda hadi litakate, nawa mikono yako kwa sabuni au maji moto, kisha shika tunda lako, vinginevyo unaweza kujikuta unakula tunda na vijidudu vya maradhi ya kuharisha na hata kipindupindu.
RAIS KARUME
RAIS WA ZANZIBAR NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI MHE DK AMANI ABEID KARUME,AKIMKABIDHI KIKOMBE NAHODHA WA TIMU YA STONE TOWN HAMZA MBWANA JOZI YA JEZI MARA BAADA YA KUIBUKA WASHINDI WA KOMBE LA KARUME KWA KUWASHINDA POLISI VIKAPU 60-47 MASHINDANO YA KARUME CUP YALIYODHAMINIWA NA KAMPUNI YA SIMU ZA MKONONI TIGO
Subscribe to:
Posts (Atom)








