Monday, April 4, 2016

ATU WASIOJULIKANA WATUMIA NAMBA YA SIMU YA MBUNGE

TANGAZO KWA UMMA.

Mbunge wa Jimbo  la Moshi mjini Jafary Michael (Chadema) anatoa tahadhari kwa umma ya kuwa
kuna baadhi ya watu wenye nia mbaya wanatumia namba yake ya simu ya mkononi  ya mtandao wa Vodacom kufanya utapeli .

Watu hao wamekuwa wakituma ujumbe mfupi (SMS) kwa watu mbalimbali kwa lengo la kutapeli wakiomba kutumiwa fedha .

Wakati akishughulikia suala hilo katika vyombo vya dola ametoa ombi kwa yeyote atakayepata ujumbe huo kuupuza na kutoa taarifa kwa yeyote atakaye fikwa na kadhia hiyo.

Ukipata ujumbe huu mfahamishe na mwenzako.

Imetolewa na :
Japhary Michael
Mbunge wa Moshi mjini

No comments: