


Ni huzuni na ni jambo la kujiuliza, kwa nini maisha ya wanamuziki maarufu wa Reggae duniani huzimika ghafla? Yu wapi Bob Marle, yu wapi Peter Tosh?
Waziri Mkuu,Edward Lowassa akizungumza na mmoja wa watoto (jina halikupatikana) waliojitokeza katika mapokezi yake wakati alipowasili katika mji mdogo wa Rujewa wilayani Mbarali akiwa katika ziara ya mkoa wa Mbeya jana.(Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Meneja wa Idara ya Masoko wa Kampuni ya simu ya tiGO, Bw. Kelvin Twissa (kushoto) akimkabidhi shilingi milioni tatu Bw. Salum Adam mara baada ya kushinda Bahati Nasibu ya Matajiri wa tiGO inayoendelea kila wiki.
Mshindi wa kwanza wa Bahati Nasibu hiyo Bw. Salum Adam akiwa katika picha ya pamoja na mshindi wa tatu, Margareth Mandari (kushoto) aliyejishindia sh. 330,000 na mshindi wa nne Fakia Said aliyejishindia 290,000. Washindi hao walikabidhiwa zawadi hizo katika Makao Makuu ya kampuni ya tiGO yaliyopo mtaa wa Lugoda jijini Dar es Salaam .
Bw. Salum Adam (katikati) akihesabiwa pesa zake na Mkurugenzi wa Idara ya Masoko, anaeshuhudia (kulia) ni Afisa wa Value Added Services Technical Assistant wa kampuni hiyo, Bw. Salim Madati
VIDONDA VYA TUMBO:
Husababishwa na unavyokula!
Kitabibu au kitaalamu, vidonda vya tumbo vinaelezewa
DALILI KWAMBA UNA VIDONDA VYA TUMBO
Dalili kwamba una vidonda vya tumbo ni nyingi, lakini zinazojulikana zaidi ni kusikia maumivu makali sehemu ya juu ya tumbo kwa wenye vidonda kwenye utumbo mfupi. Maumivu ya vidonda kwenye utumbo mrefu, mara nyingi huja saa moja baada ya mlo na mara chache huja usiku.
Maumivu ya vidonda vya kwenye utumbo mfupi, mara nyingi huja kabla ya mlo, pale tumbo linapokuwa tupu, yaani mtu anaposikia njaa. Maumivu hayo huondolewa kwa chakula, hasa maziwa ambayo yameonekana kuwasaidia watu wengi kupoza maumivu yake.
Vidonda vinapoendelea kuwepo kwa muda mrefu, maumivu huwa makali zaidi na husababisha mwili kudhoofika na kukosa nguvu. Vile vile hali inapoendelea kuwa mbaya zaidi, kinyesi cha mwathirika hutoka na damu.
KITU GANI KINACHANGIA VIDONDA HIVI?
Kitu kinachochangia mtu kupata vidonda vya tumbo ni chakula tu. Aina ya chakula na jinsi unavyokila ndiyo 'mama' wa tatizo hili, matatizo mengine ya kimaisha na msongo wa mawazo au baadhi ya madawa ni miongoni mwa vitu vinavyofanya tatizo kuwa gumu zaidi lakini siyo chanzo. Stali yako ya ulaji inapokuwa nzuri, matatizo mengine hudhibitiwa kwa lishe tu.
Vidonda vya tumbo ni matokeo ya tumbo kuwa na gesi nyingi ambayo husababishwa na ulaji mbovu, kama vile kula na kushiba kupita kiasi, kula vyakula vyenye viungo vingi vikali kama pilipili, unywaji sana wa kahawa, pombe na uvutaji sigara. Ukiwa na staili ya maisha kama hii, lazima utapata vidonda vya tumbo na hakuna dawa ya kuponya ila kufuata kanuni za ulaji sahihi.
Wakati tukikueleza hapa baadhi ya vyakula vitakavyoweza kukupa nafuu ya vidonda, lazima staili yako ya ulaji pia nayo ibadilike.
NDIZI MBIVU KAMA TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO
Inaelezwa na wataalamu wetu wa tiba mbadala kuwa ndizi mbivu ni moja kati ya tiba za nyumbani zenye nguvu sana katika kutibu tatizo la vidonda vya tumbo. Tunda hili, ambalo upatikanaji wake hauna shida wala msimu kwa kila mtu, linaaminika kuwa na virutubisho vya ajabu visivyojulikana, ambavyo kiutani wamevipachika jina la Vitamini U (against ulcers)!
Ndizi inapoliwa na ikifika tumboni, ina uwezo wa kutuliza makali ya gesi na kupunguza kuuma kwa vidonda kwa kuuwekea kinga utumbo mzima. Ili upate faida za ndizi kama tiba, hasa kwa wale ambao wako katika hatua za mwanzo za kuumwa vidonda, kula ndizi mbivu mbili pamoja na maziwa mara tatu au nne kwa siku. Fanya hivyo kama sehemu ya mlo wako kila siku.
KABICHI KAMA TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO
Kama ilivyo kwa ndizi, kabichi nayo inaaminika kuwa tiba nzuri ya nyumbani ya kudhibiti vidonda vya tumbo. Chukua robo kilo ya kabichi, ichemshe na maji ya nusu lita hadi yabaki robo. Kisha yachuje na uyaache yapoe. Yakisha poa, kunywa mara mbili kwa siku.
Aidha, mbali ya kuchemsha na kunywa maji ya kabichi, pia unaweza kutengeneza juisi yake ambayo nayo ni bora kwa matatizo ya vidonda vya tumbo. Kwa kuwa juisi ya kabichi ina nguvu sana, itapendeza ikichanganywa na juisi ya karoti kwa kipimo cha nusu kwa nusu na kisha kunywa mara mbili kwa siku.
MAZIWA YA MBUZI KAMA TIBA YA VIDONDA VYA TUMBO.
Mbali ya kula ndizi mbivu pamoja na maziwa ya ng'ombe, kunywa maziwa ya mbuzi peke yake nayo ni dawa kubwa ya vidonda vya tumbo. Ili kupata matokeo mazuri na kwa muda mfupi, kunywa glasi moja ya maziwa ya mbuzi ambayo hayajachanganywa na kitu kingine, mara tatu kwa siku.
MLO WA MTU MWENYE VIDONDA VYA TUMBO
Mlo wa mtu mwenye vidonda vya tumbo unapaswa kupangiliwa kwa makini zaidi ili kutoa lishe inayotakiwa mwilini na wakati huo huo kutoa kinga kwa utumbo ulioathirika na vidonda. Maziwa, krimu, siagi, matunda, mboga mboga, vyakula vingine vya asili vyenye vitamini mbalimbali, ndiyo mlo wa kila siku anaopaswa kula mtu mwenye vidonda.
Masaji (massage) ya mwili mzima pamoja na mazoezi ya kuvuta na kutoa pumzi ni miongoni mwa vitu vinavyosaidia kutuliza au kudhibiti vidonda vya tumbo. Mbali na yote hayo, mgonjwa anapaswa kuachana na mawazo na badala yake awe mwenye furaha, hivyo hana budi kutengeneza mazingira ya kuwa mbali na vitu vinavyomkasirisha na kumletea mawazo.
Elvan Stambuli na Makongoro Oging’ (Gazeti la Uwazi - Okt 16)
Mufti wa
Habari zilizolifikia gazeti hili siku ya tukio zinasema wakati wa kwenda Ikulu jijini Dar es Salaam, Naibu Mufti Sheikh Zuberi alifuatana na viongozi wa ngazi ya juu wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) akiwemo Katibu wa Baraza la Ulamaa na Kamishna wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS), Sheikh Hassani Chizenga na Mjumbe wa Baraza la Ulamaa, Sheikh Abdallah Nyasi.
Wengine ni Katibu wa Hija, Sheikh Sued Sued, Mkuu wa Idara ya Mambo ya Nje wa BAKWATA, Sheikh Iddi Hussein, Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Ally Nguruko na Katibu wake Alhaji Suleiman Magubika.
Mara baada ya kupata habari hizo waandishi wetu walikwenda Makao Makuu ya BAKWATA na kuwakuta viongozi wote waliotimuliwa Ikulu wakiwa wanatafakari hali hiyo chini ya mwembe ambapo baada ya kuulizwa kuhusu habari hizo walikiri kutokea.
Hata hivyo, Naibu Mufti alimruhusu Sheikh Mkuu wa Mkoa wa
Akifafanua zaidi Sheikh Nguruko alisema Rais Kikwete aliswali swala ya Iddi katika Msikiti wa Al Farouk, Makao Makuu ya BAKWATA na akaagiza Naibu Mufti na viongozi wenzake waende Ikulu katika karamu aliyoiandaa bila kukosa.
"Kwanza wale watu tuliowakuta getini walipaswa kujua kwamba Naibu Mufti ana heshima yake kitaifa na pia alikuwa akimuwakilisha Mufti wa
Naye Katibu wa Ulamaa, Sheikh Chizenga alisema kwamba hii ni mara ya kwanza kwa viongozi wakuu wa BAKWATA kukataliwa kuingia Ikulu katika sherehe ya Iddi kwani viongozi wa awamu zote tatu za serikali zilizopita walikuwa hawafanyi hivyo, hivyo kuwatupia lawama watendaji wa Ikulu na sio Rais Kikwete.