Saturday, March 3, 2018

WAFADHILI WARIDHISHWA NA MRADI


 Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi kulia akiwaonyesha mmoja ya sehemu zinazotunzwa tablets ambazo zinatumiwa kufundishia wanafunzi akiwa na wafadhili wa mradi huo




Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi akiwaongoza wafadhili wa mradi huo kutembelea maeneo mbalimbali unapotekelezwa wilayani Pangani
  Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi kushoto akiwa na wafadhili wa mradi huo wakiangalia namna wanafunzi wanavyojifunza kutumia teknolojia ya Tablets
Katibui Tawala wa Mkoa wa Tanga,Mhandisi Zena Saidi kulia akiteta jambo na wafadhili wa mradi huo
Wadau wa mradi  wa  miaka mitano wenye lengo la kutumia  teknolojia ya kisasa kuwawezesha watoto waliona fursa ndogo ya kupata elimu katika umri wa miaka tisa hadi kumi na mmoja, kujifunza wenyewe stadi za msingi za Kusoma, Kuandika na Kuhesabu (KKK) wameeleza kuridhishwa kwao na maendeleo ya majaribio hayo.
Wadau ambao walikuwa na ziara ya siku moja kutembelea vijiji mbalimbali vya nradi huo katika wilaya za Muheza na Pangani wadau aho ambao walikuwa pamoja na Mwakilishi wa Mpango wa Chakula Duniani (WFP) nchini Tanzania, Michael Dunford, Mkurugenzi wa Ofisi ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) ya Kanda ya Afrika Mashariki, Anne Ndong-Jatta wakiambatana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga, Mhandisi Zena Said.
Wakitoa maoni wakati wakipewa maelezo walisema ni wazi mradi umeanza kuonyesha uwezo wa teknolojia kuamsha ari ya kujifunza na kusoma.
Taarufa za awali za mradi na ushuhuda tuliouona inaonyesha kuwa mpango huu wa kiteknolojia una uwezo wa kuwasha mwamko wa elimu miongoni mwa watoto na wazazi na unapaswa kutiliwa maanani, alieleza  Mhandisi Said wakat wa ziara hiyo.
Pia Mhandisi Said alisema kuwa ni wazi pia kuwa kuwatambulisha wananchi katika teknolojia ya kisasa wakiwa na umtri mdogo kunawahakikishia  watoto hao kuwa hawawezi kunyanyaswa hapo baadaye wakiwa wakubwa.
Naye Ndong-Jatta alisema kuwa mradi unaonyesha haja ya kuangalia uwezekano wa kupunguza tatizo la kutojua kusoma na kuandika kwa wazazi kama njia mojawapo ya kuamsha mwamko wa elimu miongoni mwao na kuwawezesha kuwasukuma watoto kwenda shule.
Zaidi ya watoto 2,500 kutoka katika vituo 142 vilvyopo katika wilaya za Handeni, Korogwe, Lushoto, Mkinga, Muheza na Pangani walipewa tablet mpya aina ya Google Pixel C, zilizotolewa kwa hisani ya Google. Tableti hizo zimewekewa mifumo ya elimu kutoka kwa washindi watano wa mwisho wa Global Learning XPRIZE. Washindi hawa walichaguliwa kutoka katika timu 198 napaneli ya majaji 11 wa kujitegemea na walio wataalamu na kutangazwa mwezi September, 2017 wakati wa wiki ya BarazaKuu la Umoja wa Mataifa
Mradi huo wa miaka mitano uliotokana na mashindano duniani yenye thamani ya Dola za Mareka ni milioni 15. Mradihuu wa dunia unatoa changamoto kwa timu za wa bunifu kubuni na kuandaa zana za kusaidia kuondoa ujinga duniani na kuwasaidia watoto ambao hawajapata fursa ya kwenda shule kujifunza wakiwa nyumbani (Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha)

No comments: