Monday, October 6, 2008

WIKIENDA SHOWBIZ!


Fella: Siyo umeneja tu, hata stejini nimo
Kiongozi wa kundi la muziki wa kizazi kipya la TMK Wanaume Family kutoka pande za Temeke, Said Fella a.k.a Mkubwa hivi karibuni aliwaonesha mashabiki wa kundi hilo kuwa yeye siyo kiongozi wa maneno tu, hata stejini anakamua pia.

‘Mkubwa’ alijitosa stejini na kushambulia jukwaa na ‘wanae’ (kama anavyoonekana pichani katikati) huku akishangiliwa na mashabiki kibao waliofurika ndani ya Ukumbi wa Dar West Park Tabata, Dar es Salaam wakati kundi hilo lilipokuwa linasababisha bonge la shoo kwaajili ya kusheherekea Sikukuu ya Idd.

‘Mara nyingi huwa napanda stejini kuwahamasisha ‘wanangu’, siunajua muziki ndiyo ajira yetu? Huwa wanafurahi sana ninapofanya hivyo, wanajikuta wakiongeza kasi ya kutosha,” alisema Fella.
'3 bila Rimiksi' bila Inspector, Kalama, Why?
Uvumi wa wasanii wawili, Haruna Kahena ‘Inspector Haroun’ na Kalama Salum Jongo ‘Luteni Kalama’ kujitoa ndani ya kundi la TMK Halisi ulianza kuenea taratibu, baadae ukafikia hatua kwa wasanii hao kutamka hadharani kupitia baadhi ya vyombo vya habari, Rebeka Benard anadondoka nayo.

Lakini kwa upande wa kiongozi wa kundi hilo, Juma Kassim Kiroboto ‘Nature’ bado hakubaliani na hilo kwa kukanusha kuondoka kwa wasanii hao au kukataa kulizungumzia, kitu ambacho kinaonekana kuwachanganya wapenzi wengi wa kundi hilo.

Sisi kama wadau wa mradi huo tunauliza, mbona kunako rimiksi ya ngoma yenu, Tatu bila sauti za Inspector na Kalama hazimo, badala yake tumesikia sauti mpya ya msanii anayejiita Baba Levo. Why?
******************************************************************************

No comments: