Monday, October 6, 2008

EE BWANA DAH Mariah Carey!!



Unaweza usiamini, lakini huu ndiyo ukweli kwamba staa wa muziki wa R&B, Maria Carey kabla hajafunga ndoa na kijana Nick Cannon hivi karibuni, aliwahi ‘kujilamba’ (kutoka faragha) na midume zaidi ya kumi kwa nyakati tofauti.

Kwa mujibu wa mtandao wa ‘intaneti’ kati ya wanaume wote aliowahi kufanya nao mapenzi, ni wawili tu ndiyo aliyofanikiwa kufunga nao ndoa, Tommy Mottola (1990) na Nick Cannon aliyejitwisha mzigo mapema mwaka huu.

Kila kukicha baadhi ya mashabiki na watu wa karibu wa mastaa hao wanazidi kuitabiria ndoa yao kifo kutokana na tabia ya Mariah kutopenda kutulia na mwanaume mmoja ambapo siku kadhaa zilizopita watu wengi walishangaa baada ya kuwaona wawili hao wakiwa pamoja, kwani walitegemea kusikia kwamba, siku chache baada ya ndoa yao, Mariah Carey na Nick Cannon wameachana.

Kupitia safu hii ‘Ebwana dah!’ itakuwa inakudondoshea ishu za mastaa mbalimbali wa kiwanja kuhusiana na maisha yao ya uhusiano. Unachotakiwa kufanya wewe msomaji ni kutuambia unapenda kujua nani aliwahi kuwa na uhusiano na nani? Tutumie ujumbe mfupi kupitia simu namba +255 715-110 173 au Wikienda@globalpublisherstz.com **************************************************

No comments: