Friday, January 2, 2009

Ijumaa Sexiest girl: Top 5

Wema Sepetu
Irene Uwoya
Rose Ndauka
Jokate Mwegelo
Hadija Sure
Hatimaye shindano hili la kumtafuta mrembo mwenye mvuto wa kimapenzi ‘Ijumaa Sexiest Girl’ limeingia kunako hatua ya fainali baada ya mshiriki wa kumi na saba, Neema Chande kutolewa leo.

Neema ambaye ameambulia kura chache za kumtaka aendelee kuwepo katika shindano hili kutoka kwa wasomaji ambao ndiyo Majaji, ameuacha mpambano ukiendelea na warembo Irene Uwoya, Hadija Sure, Jokate Mwegelo, Wema Sepetu na Rose Ndauka ambao kwa pamoja wanakamilisha Top 5 hiyo.

Kauli kutoka kwa mratibu wa mpambano huo, Oscar, kinachofuata hivi sasa ni kuzitafuta zile chati tatu za juu, yaani Top 3 kabla ya kumpata mshindi mmoja. Amewaomba wasomaji na wapenzi wa shindano hili waendelee kutuma kura zao kwa kuandika ujumbe mfupi wakimtaja mshiriki ambaye anastahili kuibuka na ushindi, kisha watume kwenda simu namba 0784-275 714.

“Tunawashukuru na kuwapongeza washiriki wote waliyotolewa katika shindano hili, bila kuwasahau nyinyi wasomaji na wapenzi wa mpambano huu kwa kupiga kura zenu. Tunawaomba muendelee kuchangia mpaka pale mshindi mmoja, yaani ‘Ijumaa Sexioest Girl’ atakapopatikana,” alisema Oscar.

3 comments:

Mzee wa Changamoto said...

Dah!! Kaazi kwelikweli maana hata hatujui vigezo vya uchaguzi huo. Lol. Haya, i hope wana mvuto kwa wengi. Hivi mnafikiria kufanya kura za mtu mwenye "positive impact" kwa jamii yetu? Iwe kwa ujumla ama kwa celebrities tuu. Pengine itakuwa njema kutambua mchango wa wale wanaoendelea kujitolea muda na vitu vyao pamoja na vipaji vyao kuwajali wale wenye uhitaji. Nina hakika wapo wenye kufanya hivyo toka mioyoni mwao na ni wakati wa kuendzi na kutambua mchango wao.
Kazi nzuri sana Kaka na TUKO PAMOJA

Anonymous said...

Katika mademu wote hapo, aliyekwenda shule kama sexiest girl ni Jokate Mwegelo tuu.

Hii ni opinion yangu!

Anonymous said...

howdy !
dont you have conflict of interest with the Ndauka girl?