Monday, August 6, 2007

UCHAFU, USAGAJI!

Na Waandishi Maalum
Pamoja na Serikali kuongeza mkazo kwenye mapambano dhidi ya ugonjwa hatari wa Ukimwi, inaonekana baadhi ya Watanzania bado hawajali, kwani hivi karibuni kamera yetu iliwabamba warembo wawili wakifanya vitendo vya usagaji chooni.

Warembo hao waliofahamika kwa majina moja moja, Khanifa na Mwaija (pichani kushoto), walibambwa Agosti 2, mwaka huu ndani ya choo kilichopo kwenye Ukumbi wa Baa ya Mango Garden, Kinondoni jijini Dar es Salaam wakifanya uchafu.

Kamera yetu iliyokuwepo ukumbini humo kushuhudia burudani kutoka kwa Kundi la Jahazi Modern Taarab, ilitonywa na chanzo chetu kimoja kuhusu uwepo wa ‘kamchazo kachafu ka' warembo hao chooni.

Chanzo hicho, jinsia ya kike ambacho kilionesha kukerwa na uchafu wa warembo hao, kilitupasha kuwa, Khanifa na Mwaija walikuwa kero kwa watu wengine kwa sababu waligeuza choo kuwa chumba cha kufanyia mapenzi.

Kiliendelea kutanabahisha kwamba, warembo hao walikuwa wameingia chooni muda mrefu, lakini cha ajabu badala ya kutimiza kilichowapeleka, waliamua kufanya vitendo vya kusagana.
“Wanatia kinyaa, tunaomba mtusaidie, yaani wamevuana nguo, mmoja matiti yako nje, sisi wengine tukienda chooni ni kero tupu,” kilisema chanzo hicho.

Baadaye, katika kupata ukweli wa mambo, ‘paparazi’ wetu wa kike aliingia kwenye choo hicho ambapo aliwakuta warembo hao na kufanikiwa kuwapiga picha wakiwa katika pozi la kimahaba huku wakitomasana.

Hata hivyo, kutokana na kile kilichotafsiriwa kama ni kutokujali, warembo hao waliendelea na mchezo wao bila wasiwasi licha ya kushuhudia wakipigwa picha huku baadhi wateja wakiwataka waondoke chooni.

Aidha, baada ya paparazi wetu kufanikiwa kuwapiga picha wasagaji hao, chanzo chetu kingine kilichodai kinawafahamu warembo hao, kiliwataja majina yao kuwa ni Mwaija na Khanifa ingawa hakikuwatofautisha.

Kilisema, warembo hao wameshakubuhu kwa vitendo vya usagaji na mara wanapozidiwa na kilevi, hushindwa kujizuia na kufanya mapenzi sehemu yoyote.

Chanzo hicho kiliongeza kwamba kwa sasa wasagaji hao wanaishi kama mke na mume nyumbani kwao, ingawa hakikusema ni sehemu gani ya Jiji la Dar es Salaam.

Gazeti linalaani vikali vitendo vya aina hiyo, kwani siyo tu kwamba vinakwenda kinyume na maadili ya Mtanzania bali pia vinachochea kasi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi. Tunaiomba serikali idhamirie kukomesha hali hiyo. MHARIRI

The Big Brother Guy - Mwisho Mwampamba.

Mwisho Mwampamba kafika MWISHO!
Na mwandishi wetu Morogoro

Mshiriki wa Tanzania katika Shindano la Big Brother Africa (BBA) mwaka 2003, Mwisho Mwampamba a.k.a Mr. Morogoro, amedaiwa kuwa muuza chips baada ya kufilisika kimaisha.

Mwisho anadaiwa ‘kuchoka’, wakati shindano hilo lililompatia umaarufu na mafanikio kiasi baada ya kushika nafasi ya pili, likizinduliwa tena jana nchini Afrika Kusini, baada ya kusitishwa kwa muda ambapo mshindi wa mwaka huu anatarajia kujipatia Dola za Kimarekani laki moja (shilingi mil. 130).

Ndugu wa karibu na Mwisho, alilipasha gazeti hili kuwa 'staa' huyo ambaye alishika nafasi ya pili BBA, anafanyia biashara hiyo ya kuuza chips katika eneo la Forest, mjini Morogoro.

Mtoa habari huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake gazetini aliongeza kuwa Mr. Morogoro anafanya biashara hiyo katika banda ambalo anachangia na kaka yake aitwaye Isambe Mwampamba.

“Mambo yamebadilika, kila kitu kimemuendea mrama, hivi sasa maisha yake ni ya kubahatisha kwa sababu hata hilo banda la chips halimuingizii pesa kama alizokuwa akizipata na kutumia hovyo kipindi alichotoka BBA," alisema ndugu huyo.

Mtoa habari huyo aliongeza: "Wakati mwingine anategemea michango ya ndugu, hivi karibuni ndugu yetu mmoja baada ya kuona kero zimezidi za kila mara Mwisho kumuomba hela, aliamua kumpa daladala ili awe anaendesha usiku.

"Kwahiyo kuna wakati usiku huwa anaendesha daladala ili kuganga njaa, lakini hapendi kuonekana, si unajua ni 'supastaa', kwa kweli tunamhurumia, Mwisho hakuwa mtu wa kupigika kiasi hicho, kwa sababu alikuwa ameshatoka kimaisha".

Jitihada za gazeti hili kumpata Mwisho azungumzie madai hayo ziligonga ukuta, kwakuwa lilielezwa kwamba yupo safarini Dar es Salaam, pia lilipojaribu kumsaka kwa njia ya simu ya mkononi halikufanikiwa kwani namba yake ilikuwa haipatikani.

Alipopatikana kaka yake Mwisho, Isambe Mwampamba alisema kuwa banda la chips ni mali yake, lakini watu wanavumisha ni la Mwisho kwa sababu huwa wanashirikiana, pia huwa anakwenda bandani hapo mara kwa mara.

"Banda ni langu na kwa kuwa Mwisho ni ndugu yangu kuna wakati tulikuwa tunashinda naye pale bandani, sasa watu wanadhani ni lake, ukitaka kuamini hivi sasa nimelifunga kwa sababu nimepata kazi Kiwanda cha Tumbaku," alisema Isambe.

Baada ya tetesi kuzagaa kwamba Mwisho 'ameishiwa', watu mbalimbali wamekuwa wakitoa maoni tofauti, kuhusiana na mabadiliko ya kimaisha ya Mr. Morogoro huyo.

Wakiongea na gazeti hili mjini hapa, wananchi kadhaa walisema, Mwisho amekumbwa na balaa hilo kwa sababu alikuwa mfujaji wa pesa.

"Aliposhinda BBA alipata mikataba mingi, ikiwemo kurekodi filamu Nigeria, lakini jamaa alikuwa mtu wa matanuzi," alisema Kulwa Ibrahimu wakati Happy Kushamu alieleza: "Mwisho alitaka kuishi kizungu ndiyo maana amewahi kuishiwa.”

Hata hivyo, Chris Kabala alisema, anaamini matatizo ya Mwisho yametokana na laana aliyoachiwa na aliyekuwa mchumba wake, Elpy Zembatakis ambaye anadai alimtosa baada ya kupata mafanikio BBA.

"Laana siyo mpaka itoke kwa wazazi, kitendo cha Mwisho 'kumwaga' Elpy hakikuwa kizuri kabisa, fikiria alikuwa ndiye mchumba wake kabla hajaenda BBA, lakini aliporudi 'alimtosa', hiyo ilikuwa ni laana kwa sababu yule dada aliumia sana.

"Mwisho hakujali alitaka 'masupastaa' wenzake, kama Ray C (Rehema Chalamila) ambaye walitesa na tukasikia walifunga ndoa, lakini haikudumu, mara Rah P (Fredinah Payton), wakatangaza wanaona lakini ndoa yenyewe ikawa hewa tu," alisema Chris.

2 comments:

Unknown said...

Kuuza chips sio vibaya, mwanamume anatafuta hivyo. Leo anauza chips, keshokutwa anafungua restaurant etc etc. Tuache kuwakatisha tamaa watu kutafuta, kazi kazi tu, au mnataka atafute AK 47 awe jambazi? Maendeleo yanaletwa na jitihada za watu kama hivyo. Keep it up Brother Morogoro!

Anonymous said...

hawa madada wanalana tena hawana haya ningewakuta mimi wote ninge waponyeza kizenji