Wednesday, February 3, 2010

Ana Miaka 13 Lakini Anaonekana Kama Bibi wa Miaka 50



Siku moja Zara Hartshorn alipanda basi la abiria na kutaka kukata tiketi ya watoto lakini dereva wa basi hilo alimuangalia kwa mshangao na kumwambia kuwa asifanye masihara alipe pesa kamili.

Zara aliposema kuwa yeye ni mtoto na ana umri wa miaka 13, dereva huyo ambaye alikuwa ni mzee wa makamo, alicheka sana na kumwambia kama ndio hivyo basi na mimi nina umri wa miaka 21.

Abiria nao waliingia kwenye mjadala huo na kumuunga mkono dereva kuwa Zara anawachezea watu akili kwani anaonekana wazi kuwa yeye ni kikongwe mwenye wajukuu.

Zara kwa aibu alishuka toka kwenye basi hilo na kusubiria basi jingine kwa imani dereva wa basi lifuatalo angeweza kumuelewa kuwa yeye ni mtoto.

Kusoma zaidi stori ya Zara linki ni hii

http://www.nifahamishe.com/NewsDetails.aspx?NewsID=4017954&&Cat=7

No comments: