Ndugu zangu,
Kwa
mwanadamu, hakupaswi kuwapo na ukomo wa kujitahidi kufanya yalo mema kwa jamii
yako.
Na
katika kujitahidi kuyafanya yalo mema, basi, mwanadamu uwe tayari kukumbana na
changamoto nyingi. Na kama ilivyo kwa maji
ya mto, yanapokutana na mwamba, basi, kasi yake huongezeka maradufu.
Leo
blogu yako hii ya Mjengwablog imetimiza miaka saba. Miaka saba si haba. Ni umri
wa mtoto kuanza shule.
Kwa
niaba ya timu nzima ya Mjengwablog nachukua fursa hii kuwashukuru kwa dhati ’
WanaFamilia’ wote wa Mjengwablog kwa kuwa nasi katika hali zote. Hivyo basi,
kutuunga mkono.
Naam,
ni miaka saba ya kuwa mtandaoni karibu katika kila siku inayotujia na kupita.
Ni miaka saba ya mapambano magumu ya kuitumikia jamii na kuhakikisha kuwa
tunabaki hai.
Maana,
unapoamua kuitumikia jamii bila kuegemea upande, basi, ina maana pia ya kujiweka katika mazingira ya hatari sana. Yumkini kuna maua mengi ya upendo yanaweza
kurushwa kwako, lakini, kuna mishale michache ya sumu ambayo pia itarushwa
kwako. Kwamba kuna maadui pia.
Na
ukimwona nyani ametimiza miaka saba , basi, ujue kuna mishale kadhaa ameikwepa. Lakini, na anavyozidi
kuendelea kuishi, yumkini kuna mishale mingine inaandaliwa. Na nyani hatakiwi
kuishi kwa kuogopa mishale ya wanadamu. Vinginevyo, ajitundike mtini, afe.
Lililo
jema na kutia faraja ni kutambua, kuwa kuna walio wengi wenye kufaidika na kazi
hii ya kijamii ambayo Mjengwablog inaifanya.
Ni hawa ndio wenye kututia nguvu ya kuendelea kuifanya kazi hii pamoja
na changamoto zake nyingi.
Ndugu
zangu,
Ilikuwa
ni Jumanne, Septemba 19, 2006. Ni siku hiyo ndipo kwa mara ya kwanza niliingiza
picha ya kwanza kwenye mjengwablog na kuashiria uzinduzi wa
blogu. Ni picha hiyo inayoonekana hapo juu. Niliipiga eneo la Kinondoni Shamba.
Tangu siku ya kwanza, niliweka wazi kwenye fikra zangu, kuwa Mjengwablog iwe
jukwaa litakalomtanguliza mtu wa kawaida. Iwe sauti ya wale ambao sauti zao
hazisikiki.
Na
Mjengwablog ikawa chachu ya kuanzishwa kwa gazeti la michezo na burudani la ’
Gozi Spoti’, ikawa chachu pia ya kuanzishwa gazeti la ’ Kwanza Jamii’.
Na
kuna miongoni mwetu wenye kufikiri, kuwa mwenye kumiliki gazeti ni lazima awe
Mhindi au Mtanzania ’ mweusi’ Mfanyabiashara tajiri. Nakumbuka kuna hata ambao
hawakuwa tayari kuchangia kiuandishi kwenye ’ Gozi Spoti’ na ’ Kwanza Jamii’
kwa vile linamilikiwa na ’ Mswahili mwenzao!’Na
hata kupata matangazo kukawa na ugumu mkubwa. Gozi Spoti lilisimama kuchapwa baada
ya mwaka mmoja mitaani. Kwanza Jamii, nalo likasimama kuchapwa. Likarudi tena
baada ya kuingia ubia na Shirika la
Daraja. Baada ya miaka miwili na baada ya aliyepelekea kuingia ubia kuondoka nchini na kurudi kwao Uingereza,
basi, Kwanza Jamii nalo ’ likaandaliwa’ mazingira ya kuondoka mitaani.
Hata
hivyo, Kwanza Jamii, gazeti dogo, ambalo naamini ni muhimu kwa jamii, limerudi tena
kupitia mtandaoni. Mipango iko mbioni kuliimarisha zaidi katika siku zijazo.
Ndugu
zangu,
Changamoto
zipo ili tukabiliane nazo, na si kukata tamaa. Mjengwablog inatimiza miaka saba
leo kwa vile tulishaamua, kuwa tutapambana hadi risasi ya mwisho. Hivyo pia,
tutapambana hadi pumzi ya mwisho.
Maana,
tunaamini kuwa kazi tuifanyayo ni yenye manufaa kwa jamii pana. Na tuna haki ya
kuifanya. Tunavumilia sauti zenye kutushutumu na kutukosoa. Kuna tunayojifunza
kutoka kwa wakosoaji wetu. Tunawashukuru sana na tunawaomba waendelee kutukosoa
kila wanapoziona kasoro.
Lakini,
kuna wachache pia wenye kuonyesha zaidi chuki kuliko kukosoa. Hawaipendi kazi tuifanyao wala kuithamini, ni
kawaida. Lakini, faraja ni kutambua kuna wenye kuipenda na kuithamini kazi yetu.
Hapa
chini ni mmoja wa watu hao;
Maggid,
Iringa.
Iringa.
Wow. Siamini kama ni miaka
saba tu. Mjengwa Blog was the first TZ blog that really hooked me. And it is
still hooking me. In a blogging world fixated with celebrity, gossip and
slander, Mjengwa Blog is a rare and fresh piece of sanity with a window onto
the real Tanzania. Bravo Mwenye Kiti, umefanya kazi kubwa hadi hapo ulipo. Na
wala usipate wazo lolote lile la kustaafu. Wanakijiji wenzako bado tunakuhitaji
na kukutegemea uendelee hivyo hivyo. Aluta continua...
Jimmy Innes ( UK)
Ahsanteni
sana.
Maggid
Mjengwa.
Mwenyekiti
Mtendaji.
Mjengwablog.com
No comments:
Post a Comment