Makamu
Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam, (Anayeshughulikia masuala ya Utawala),
Profesa David Mfinanga, (Watatu kushoto), akipeana mikono na Afisa Uhusiano
Mwandamizi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (watatu kulia), wakati
akipokea msaada wa magodoro 118 yaliyotolea wan Mfuko huo kwenye hafla fupi
iliyofanyika chuon I hapo, Agosti 24, 2015. Magodoro hayo ni kwa ajili ya
wanafunzi walioathiriwa na mogto uliozuka kwenye bweni kitalu B kule hosteli za
Mabibo, Aprili mwaka huu 2015.
Profesa
mfinanga (wapili kushoto), akitoa shukrani kwa niaba ya chuo mbele ya maafisa
wa PSPF, viongozi wa wanachuo na
wafanyakazi wa chuo hicho wakati wa hafla hiyo
Afisa
Uhusiano wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF, Abdul Njaidi, (kushoto), akizungumza na
baadhi ya wafanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, baada ya kukabidhi
msaada huo, Agosti 24, 2015
Paulina Mabuga, mfanyakazi wa Chuo Kikuu Cha Dar
es Salaa, (wapili kulia), akizungumza kwenye hafla hiyo. Wakwanza kushoto ni
Rais wa Serikali ya Wanafunzi, Denis Bashulula
Profesa
Mfinanga na Njaidi wakiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi wa
serikali ya wanafunzi UDSM
Mfanyakazi
wa UDSM, akipita jirani na magodoro hayo
NA K-VIS MEDIA
MFUKO wa Pensheni wa PSPF, leo Agosti 24, 2015, umekipatia Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, UDSM, magodoro 118 ili kusaidia huduma ya malazi kwa wanachuo walioathirika kutokana na bweni lao kuungua moto kwenye hosteli ya chuo hicho Mabibo jijini Dar es Salaam Aprili mwaka huu.
Akikabidhi msaada huo kwa Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, (Anayeshughulikia masuala ya Utawala), Profesa David A. Mfinanga, Afisa Uhusiano Mwandamizi wa PSPF, Abdul Njaidi, amesema, PSPF, iliguswa na ajali hiyo ya moto ambayo iliyotokea kwenye bweni kitalu namba B na kusababisha mamia ya wanachuo kupoteza mali zao.
“Kwa kutambua kuwa wanachuo ni sehemu ya jamii ya Watanzania, na pia ni wanachama watarajiwa wa Mfuko, tumeona tuchangia sehemu ya vifaa ili wanafunzi waweze kurejean katika hali yao ya kawaida.” Alisema Njaidi.
Akitoa shukrani zake, kwa niaba ya Chuo, Profesa Mfinanga aliishukuru PSPF, kwa msaada huo ambao kwa hakika umesaidia pakubwa, kwani magodoro hayo yatapelekwa kwa walengwa na hivyo kusaidia kuwapunguzia machungu waliyoyapata kutokana na kuunguliwa vifaa vyao.
Kwa mujibu wa viongozi wa Chuo hicho, jingo hilo lilikuwa ,linakaliwa na wanachuo 788, wakati linawaka moto.
No comments:
Post a Comment