Thursday, December 14, 2017

KHERI APOKELEWA KWA KISHINDO MKOANI DODOMA.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Ndg:Kheri D James (katikati) akiwasili Ofisi za Makao makuu ya Chama Cha Mapinduzi Taifa kushoto kwake ni Ndg
Kaimu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Shaka Hamdu Shaka.
Ndg:Rodrick Mpogolo Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi akimpokea Mwenyekit wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi alipowasili Makao makuu ya chama cha mapinduzi.
Mwenyekiti wa umoja wa vijana mkoa wa Dodoma akiwasilisha salamu za vijana wa mkoa wake kwa mwenyekiti wa umoja wa vijana Taifa.
Kaimu katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi ndg:Shaka Hamdu Shaka akizungumza.
Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha mapinduzi ndg:Thabia Mwita akizungumza na vijana wa Umoja wa Vijana wa chama cha mapinduzi katika viwanja vya makao makuu ya ccm dodoma.
Kikundi cha chipukizi kikitoa burudani
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi ndg:Kheri D James akipokea wanachama wapya 200 toka vyama mbalimbali vya upinzani pichani ni alie kuwa katibu wa chama cha ACT WAZALENDO mkoa wa Mwanza ndg:gwanchele.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ndg:Kheri D James akizungumza na Vijana wa mkoa wa dodoma katika hafla ya kumkaribisha iliofanyika makao makuu ya CCM DODOMA.

 Meza kuu
Vijana wakisikiliza kwa umakini hotuba ya mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ndg:Kheri D James.
PICHA ZOTE NA FAHADI SIRAJI




No comments: