Monday, September 29, 2008

WIKIENDA SHOWBIZ

Matumaini:sitoki faragha na Kiwewe
Kutoka ndani ya Kundi la Sanaa za Maigizo, Kaole, ‘Hot Corner’ ilipata kupiga stori na mkali wa ‘komedi’, Tumaini Mwakibibi a.k.a Matumaini ambaye aliongea ishu kibao ambazo wewe msomaji utazinyaka kutoka hapa, zaidi tucheki na Rebeka Bernard kwa ‘intavyuu’ zaidi.

Hot Corner: Mambo vipi Matumaini?
Matumaini: Yapo fresh tu.
Hot Corner: Unajisikiaje kuwa staa wa Bongo?
Matumaini: Najisikia vizuri kwasababu ndiyo ilikuwa ndoto yangu haswa.
Hot Corner: Unadhani utakuwa hujakamiliki bila kuwa na nini?
Matumaini: Bila sanaa ya maigizo.
Hot Corner: Kuna tetesi kuwa unatoka faragha na masanii mwenzako, Kiwewe, hiyo ikoje?
Matumaini: Hakuna kitu kama hicho, yule ni msanii mwenzangu.
Hot Corner: Starehe yako kubwa ni ipi?
Matumaini: Kucheki muvi.
Hot Corner: Msanii gani Bongo anayekuvutia?
Matumaini: Marlaw ananikosha sana.
Hot Corner: Kipi kinachokukera nje ya sanaa?
Matumaini: Watu wazima wanaofanya mambo ya kitoto.
Hot Corner: Msanii gani alikuvutia ukaingia kwenye sanaa?
Matumaini: Kemmy.
Hot Corner: Unapenda mume wa aina gani ?
Matumaini: Atakayekubaliana na matakwa yangu.
Hot Corner: Poa, aksante sana kwa ushirikiano wako.
Matumaini: Nawe pia, karibu tena.
***************************************
Cellulant yagawa shavu kwa wasanii wa Bongo
Kampuni mpya ya milio ya simu Bongo, Cellulant imezindua rasmi mradi wa kununua nyimbo za wasanii na kuziuza kisha wasanii hao kufaidika kwa kiasi cha mkwanja kitakachopatikana, ishu ambayo tunaweza kusema ni shavu au dili kwa wasanii hao, cheki na Richard Bukos.

Akisema na safu hii katika uzinduzi huo uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Hoteli ya Southern Sun, Dar es Salaam, Afisa Mwandamizi wa kampuni hiyo, Jide Harrison alitamka kwamba katika mpango huo kampuni yake itachukua nyimbo za wasanii na kuziuza kwa watumiaji wa simu za mkononi kwa shilingi 600.

“Katika kiasi hicho, msanii atapata shilingi mia moja kila wimbo wake utakaponunuliwa pesa ambayo atakuja kuchukua kwenye kampuni yetu kila mwezi tofauti na walanguzi ambao wanahamisha kienyeji nyimbo za wasanii na kunufaika wao peke yao,” alifafanua Jide.
************************************

TMK Family:..wajidhamini wenyewe
Tofauti na ilivyozoeleka na watu wengi kwamba, wasanii huwa hawana uwezo wa kujiandalia shoo wenyewe zaidi ya kualikwa na mapromota, usemi ambao kundi la TMK Wanaume Family limeufuta kwa kujiandalia shoo lenyewe, huku wakijidhamini kupitia maduka yao ya nguo, la Mbagala na lile la Temeke, Dar es Salaam, cheki na Issa Mnally.

Meneja wa kundi hilo, Said Fella alisema na safu hii kwamba, shoo ya kwanza itagongwa siku ya Idd ndani ya Ukumbi wa Basiaya Camp uliopo Boko, nje kidogo ya jiji la Dar es Salaam, huku ya pili ikifanyika siku ya Idd pili kunako ukumbi wa Dar West Park Tabata.

“Katika shoo hizo maalum kwa ajili ya kusherehekea sikukuu hiyo, tutatambulisha kazi kibao ukiwemo wimbo mpya wa Mh. Temba ambao unaoitwa ‘Kiulaini,” alisema Fella.
******************************


Sostenes alipokuwa Hon Kong!
Picha mbili za juu ni Bw. Sostenes Raphael akiwa Hon Kong mapema wiki iliyopita alikokwenda baada ya kushinda Bahati Nasibu ya Jishindie Safari ya Hon Kong 2008 iliyokuwa ikiendeshwa na gazeti la Ijumaa Wikienda. Sosteness amerejea Dar jana saa nane mchana.

1 comment:

Anonymous said...

🌹 Ushuhuda Wangu Kuhusu Dkt. Dawn – Mtu Aliyerejesha Nyumba Yangu na Furaha Yangu

Nataka kushiriki ushuhuda wangu wa dhati kuhusu jinsi Dkt. Dawn alivyobadilisha maisha yangu kabisa.

Kwa karibu mwaka mmoja, mume wangu aliniacha mimi na watoto wetu wawili. Aliacha kujali, akaacha kupiga simu, na alikuwa ameenda kabisa. Nilikuwa nimevunjika moyo, nimechanganyikiwa, na karibu kupoteza tumaini. Kisha siku moja, rafiki aliniambia kuhusu Dkt. Dawn, mtu wa kiroho aliyepewa kipawa na ulimwengu kuwasaidia watu kurejesha upendo na amani.

Mwanzoni, nilikuwa na shaka, lakini kitu kuhusu maneno yake kilinipa amani. Aliniambia haswa kilichokuwa kibaya na kwamba mtu alikuwa ametupa uchawi mkali kututenganisha. Aliandaa kazi maalum ya kiroho na uchawi wa kuungana tena kwangu — na ndani ya siku chache, mume wangu alinipigia simu ghafla, akilia na kuomba msamaha.

Tangu wakati huo, maisha yangu hayajawahi kuwa sawa. Ndoa yetu sasa ni tamu na yenye furaha zaidi duniani. Tunapendana zaidi kuliko hapo awali, na nyumba yetu imejaa vicheko na baraka.

Lakini si hayo tu — Dkt. Dawn pia alisaidia kuondoa bahati mbaya na nishati hasi iliyokuwa ikizunguka familia yetu. Tangu wakati huo, kila kitu kimekuwa laini: amani nyumbani kwetu, maendeleo ya kifedha, afya njema, na furaha safi.

Ninashukuru ulimwengu kila siku kwa kuniongoza kwa Dkt. Dawn. Kwa kweli ni mtu mwenye nguvu na mwanga wa kimungu. Ikiwa unapitia hali yoyote — huzuni, bahati mbaya, au mkanganyiko — usikate tamaa. Mfikie na uache ulimwengu ufanye kazi kupitia yeye ili kubadilisha hadithi yako, kama vile alivyobadilisha yangu.

Wasiliana naye kwenye WhatsApp: +2349046229159
Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com