Saturday, October 25, 2008

ULIMWENGU WA KANUMBA

Lile tatizo la kiufundi lililoweka kiwingu kwenye mtandao wa muigizaji mahiri nchini Tanzania, Steven kanumba, sasa limeondoka na mtandao huo uko makini. Mashabiki na wapenzi wanakaribishwa kwenye ulimwengu wa Kanumba, ambako anaelezea alikotoka, alipo na nini amefanya kama msanii wa kibongo. Pengine ungetaka kutangaza biashara yako kupitia mtandao wake, basi hebu cheki hapa upate 'data' na 'contact' zake zote: www.kanumba.com.

Friday, October 24, 2008

IJUMAA SEXIEST GIRL: Wanne wafungua dimba la kuaga

Rose Ndauka
Queen David
Maunda Zoro
Winta

Violeth Timoth
Siku chache baada ya kuanza kwa shindano la ‘Ijumaa Sexiest Girl’ wasomaji na wapenzi wengi wameonesha kulipokea kwa shangwe, jambo linalowafanya waendelee kutuma meseji za kumwaga, wakiwapigia kura wale ambao wanadhani wanastahili kuendelea kuwepo shindanoni. Kama tulivyowahabarisha wiki iliyopita kuwa, shindano linatakiwa lianze rasmi na warembo 12 kati ya 20 waliyopo pichani, lakini kutokana na wengi kufungana katika kura zao, leo wanatolewa wanne, Nakaaya, Queen David, Violeth na Latoya ambao wameambulia kura chache. Bado tunaendelea kuwatafuta 12, unachotakiwa kufanya msomaji ni kuendelea kututumia ujumbe mfupi (SMS) kupitia simu zile zile +255 784-275 714, +255 787-110 173, utuambie nani anastahili kuingia rasmi katika mpambano huo.

Big Brother Africa: TK and Ricco Go Head-to-Head!

Ricco
Takondwa 'TK'
The housemates of M-Nets Big Brother Africa 3 have nominated and after Mondays (October 20) Nomination Show, Zambias TK and Angolas Ricco are up for eviction this week.

This week Tawana followed Morris decision last week in deciding to not use her power as Head of House to influence the nominations, meaning that the housemates nomination stands.

Ricco and TK received 3 nominations apiece and will go head-to-head in the battle of the Lucky Housemates! TK has been nominated five times, saved himself twice and was saved by Morris once. Ricco has been nominated twice, and swapped in twice, by Heads of House Morris and TK. This will be his fourth trip to the glass house!

Heres how TK and Ricco found themselves on the nomination list this week:

- Thami voted for Ricco “because hes been up so many times and it would be a disaster if another girl went,” and for Morris, because he has not tasted nomination since the fake nominations in week one.

- Ricco voted for Thami to see if he could stand the nomination pressure again. He also voted for Morris because he hadnt been nominated in a while.

- Hazel nominated Ricco and TK, because she sees them as strong contenders.

- TK voted for Thami - again as punishment for his pranks and for new Head of House Tawana, to “see if she will change herself”.

- Tawana voted for TK because of his constant snoozing and Ricco, because “he has lost all his girlfriends,” and she thinks he is lonely.

- Morris nominated Tawana because she was Head of House and wouldn't be eliminated and TK because he's “been there, done that” and “won't be a problem.”


Now its up to viewers to decide the fate of the nominated twosome and remember, youre voting for the person youd like to see evicted! There are three ways to vote - by sending an SMS, making a call or by voting for free on the website (www.mnetafrica.com/bigbrother).

Tuesday, October 21, 2008

Ubunifu!


Author/photographer Saxton Freymann has made his living sculpting food, and publishing the results in a delightful series of children’s books with titles like How Are You Peeling? Above are a few of his favorite Freymanns!

UZITO UNAPOKUZIDIA..!

..na mara nyingi wenye vitambi kama huyu wanapenda sana kula kulaa, hii inakuwaje?

UZITO UNAPOKUZIDIA..!

?
..na mara nyingi wenye vitambi kama huyu wanapenda sana kula kulaa, hii inakuwaje

Matatizo ya kibofu cha mkojo kwa wanaume


Ni safari ndefu kwa mwanaume kufikisha umri wa miaka 50, lakini katika umri huo pia ndiyo matatizo mengi ya kiafya huanza kujitokeza, likiwemo tatizo la kibofu cha mkojo.

Kwa mujibu wa takwimu zilizopo, watu wanne kati ya watano hupatwa na matatizo ya kibofu cha mkojo wanapofikisha umri wa miaka 50. Inaelezwa pia kuwa karibu asilimia 80 ya watu wenye umri wa miaka 60 hupatwa na tatizo la kibofu.

Kuna aina nyingi za matatizo ya kibofu cha mkojo ambayo mtu anaweza kuyapata, mengi ya matatizo hayo yanaweza yasiwe na maumivu sana lakini hutoa usumbufu wakati wa kutoa haja ndogo ambayo mwanzoni hutoka kwa shida.

Tatizo la kibofu linapoanza kukomaa kwa mgonjwa, huweza kusababisha maumivu fulani hata kwa viungo vingine kama vile mgongo na ‘hips’, miguu na kwenye nyayo ikiwa ni dalili ya kuanza kukomaa kwa ugonjwa.

SABABU
Zinaweza zikawepo sababu nyingine, lakini sababu zinazojulikana zaidi kusababisha matatizo ya kibofu cha mkojo kwa wanaume wengi ni kama ifutavyo:

Kukaa sehemu kwa muda mrefu mkao wa aina moja. Hali hii huweza kuwapata baadhi ya watu maofisini wenye kazi za kukaa kwa muda mrefu na ambao hawapendi kufanya mazoezi mara kwa mara. Hivyo jiepushe na kazi za kukaa mkao mmoja kwa muda mrefu, ni hatari kwa afya yako ya uzeeni.

Matatizo sugu ya kibofu cha mkojo wakati mwingine husababishwa na hali ya hewa, hasa mtu anapopigwa baridi kali kwa muda mrefu. Aidha mtu pia anaweza kupatwa na matatizo haya kutokana na kuugua magonjwa ya kuambukiza.

Vile vile inaelezwa kwamba kadri umri unavyosonga mbele, ndivyo mtu anavyoongezeka uzito na hupoteza ulaini wa viungo, hivyo kufanya sehemu za nyonga kuelemewa na mzigo wote kuangukia kwenye kibofu.

Sababu nyingine inayoweza kusababisha mtu kupatwa na matatizo ya kibofu uzeeni, ni kuwa na tatizo la kukosa choo kwa siku kadhaa mara kwa mara.

KINGA
Jiepushe na unywaji wa ‘kafeni’ kwa wingi ambayo hupatikana zaidi kwenye chai, kahawa na chokoleti. Japo chai ina faida nyingine nyingi mwilini, lakini ikizidi sana huchangia kubana njia ya mkojo hivyo kuifanya hali ya mtu mwenye tatizo hili kusikia maumivu zaidi wakati wa kukojoa.

Aidha, inaelezwa pia kuwa unyaji wa kilevi uepukwe kwani huchangia kuziba kwa njia ya mkojo, ingawa hoja hii inapingwa na baadhi ya watu, hasa wale wanaotetea kilevi, wanasema kuwa watu wengi wanaokunywa bia huwa hawasumbuliwi na matatizo ya kibofu cha mkojo.

Vile vile, ili kujiepusha na uwezekano wa kupatwa na matatizo ya kibofu cha mkojo uzeeni, jiepushe na ulaji wa viungo vingi (spices), hasa pilipili, kupitia vyakula unavyokula kila siku.

Jiepushe na kuishi maisha yenye mawazo, hasira na ghadhabu, kwani hali hii huongeza uvimbe kwenye kibofu kutoka na kuzalishwa kwa wingi kwa homoni za kibofu pale mtu anapokuwa kwenye mfadhaiko wa akili, hii ni kwa mujibu wa wanasayansi wetu.

Penda kujisaidia haja ndogo kabla ya kwenda kulala ili kusafisha kibofu chako na inalezwa pia kuwa njia bora zaidi ya kusafisha kibofu cha mkojo ni kufanya tendo la ndoa kwani manii huondoa vizuizi vinavyozuia mkojo kupita kwenye kibofu.

Mwisho, inashauriwa kuwahi hospitali mapema pale unapoona dalili za kusumbuliwa na kibofu ili kupata tiba mapema kabla ya hali kuwa mbaya. Asanteni.

Monday, October 20, 2008

WIKIENDA SHOWBIZ


Whitnes hajaambulia ziro Channel O
Msanii wa kike anayekomaa kunako game ya muziki wa Hip Hop, Whitness Kaijage hajaambulia ziro kama ulivyo wimbo wake, badala yake amedondoka Bongo na tuzo ya Channel O, kupitia video ya ngoma yake, ‘Ziro’ iliyomshirikisha Fareed Kubanda ‘Fid Q’ na kusema kuwa hafanyi muziki kwa ajili ya Tanzania tu, bali anataka Afrika nzima na baadhi ya nchi za mbali zaidi wamtambue.

Akipiga stori na Kituo cha Televisheni cha Channel Ten mwishoni mwa wiki iliyopita msanii huyo ambaye pia ni ‘muhanga’ wa kundi la Wakilisha alisema kwamba anaamini ipo siku ndoto zake hizo zitatimia, kwani dalili za mafanikio tayari zimeshaanza kuonekana kupitia tuzo hiyo ambayo hutolewa na Kituo cha TV cha Channel O cha Afrika Kusini kila mwaka.

Hiyo inaonesha ni jinsi gani game ya muziki wa Bongo flava inavyozidi kubamba Afrika, kwani mwaka jana mchizi kutoka TMK Halisi, Juma Kassim ‘Nature’ alirudi kutoka Afrika Kusini na tuzo ya Channel O baada ya video ya wimbo wake, Mugambo kufanya vyema. Sisi kama Abby Cool & MC George Over The Weekend tunatoa Big Up za kumwaga kwa Whitness, aendelee kukomaa zaidi katika game.

MTV Africa Awards:PROF. JAY YUKO FULL KUJIAMINI
Wakati siku za utoaji Tuzo za MTV Afrika (MTV Africa Music Awards) zitakazofanyika nchini Ghana hivi karibuni zikiwa zinazidi kusogea kwa kasi, muhusika wa shughuli hiyo anayeiwakilisha Bongo, Joseph Haule ‘Prof. Jay’ anazidi kuonesha ‘komfidensi’ za kutosha kwa kutamka kwamba mwaka huu ni wake, Rebeka Bernard anashuka nayo.

Akiwa anawania tuzo moja na wakali wa Marekani, Lil Wayne na The Game, Jay alisema kuwa watu wasishangae pale atakapoibuka ‘Best Hip Hop’ na kuwamwaga wasanii hao kwasababu ngona anazofanya zina ujumbe na mafunzo ya kutosha kwa jamii kitu ambacho kinamfanya asiwe na wasi wasi kwa hilo.

“Nafahamu kwamba wasanii ninaopambana nao katika tuzo hiyo ya mwana Hip Hop bora ni wakali, lakini naamini mashabiki wangu na wapenzi wa Hip Hop Bongo hawataniangusha kwasababu ushindi wangu ni wa nchi nzima,” alisema Jay.

Mbali na Lil Wayne na The Game, ndani ya kategori hiyo, Jay pia atakutana na wasanii wengine kama 9ice kutoka Nigeria na HHP wa Afrika Kusini. Ishu zaidi kuhusiana na tuzo hizo za MTV endelea kufuatilia katika magazeti yanayotolewa na Kampuni ya Global Publisher na kusikiliza Radio Clouds FM, bila kusahau Kituo cha Runinga cha TBC 1.
Street Version

MASANJAa.k.a Mkoboaji
Hivi karibuni msanii wa Kundi la Comedy Original, Masanja (pichani juu) ambaye sasa anajiita Mkoboaji, alijichanganya kinyemela ndani ya Viwanja vya Mnazi mmoja, Dar es Salaam ulipokuwa ukifanyika mkutano wa Chama cha Wananchi, CUF. kamera ya Street Version ilimbamba laivu.
*********************************************************
SHAKIRA: Alijiachia na wanaume watatu tu!
Inakuwaje wapenzi wa safu hii, ‘Ebwana Dah!’, wale wasomaji waliotutumia sms wakitaka kufahamu mwanamuziki Shakira aliwahi kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanaume gani, leo ndiyo siku yao ya ‘kujilamba’.

Ishu ni kwamba, binti huyo Shakira Isabel Mebarak Ripolli a.k.a Shakira mwenye umri wa miaka 31 sasa anaonekana kuwa bonge la mjanja, kwani tangu alipoukaribisha ustaa amewahi kujiachia na wanaume watatu tu ambao ni Osvaldo Rios, Wyclef Jean aliyefanya naye kolabo ya wimbo ‘Hips Dont Lie’ na Antonio de la Rua ambaye anatanua naye hadi hii leo.

Kwa Osvaldo Rios na Antonio de la Rua inaweza isiwe ishu sana kwa mashabiki wa mrembo huyo aliyezaliwa February 2, 1977, Barranquilla, Colombia, lakini kwa Wyclef inaweza ikawashangaza mashabiki wengi na huenda wasiamini kama kweli mchizi aliwahi kujiachia na mtoto huyo, bingwa wa mauno awapo stejini kwani walidhani urafiki wao uliishia kwenye kolabo ya Hips Dont Lie tu.