Saturday, March 1, 2014

AUDIO: Maongezi kati yangu nawe kuhusu Katiba Mpya

SIKINDE YAANZA KUIPUA NYIMBO MPYA…

Inline image 1

Hatimaye bendi kongwe, bendi pekee ambayo imepata kuwa mabingwa wa muziki nchini mara zote mbili ambazo mashindano hayo yamepata kufanyika, bendi ya  Mlimani Park Orchestra “Sikinde Ngoma ya Ukae” imeanza kuipua nyimbo zake mpya zitakazokuwa katika album mpya ya “Jinamizi la Talaka” itakayozinduliwa mwaka huu 2014.
Album hiyo itakuwa na jumla ya nyimbo 7.
Mpaka sasa Sikinde wameishazitoa nyimbo tatu za 1. Jinamizi la Talaka, 2. Za Mkwezi Mbili na 3. Nikipata Nitalipa.
Nyimbo hizi unaweza kuzisikiliza online au ku-download kwenye mtandao wa https://www.hulkshare.com/sikinde
Nyimbo 4 zilizobakia ambazo nazo zitatolewa muda wowote kuanzia hivi sasa ni 1. Kibogoyo, 2. Dole Gumba, 3. Ng'ombe Haelemewi na Nundu na 4. Tabasamu
Hii ni album ya kwanza kutolewa tokea mwaka 2009 iliporekodiwa album ya “Supu Umeitia Nazi” album iliyomfanya mwimbaji wake Karama Regesu kuchukua zawadi katika Kili Music Award ya mwaka 2009 kwenye category ya “Mtunzi Bora wa Muziki”.

HALMASHAURI YA JIJI : JE HAWA NI SAHIHI KUWEPO KATIKA ENEO HILI?

Hili ni eneo la Ubungo ambapo Kumekuwa na kero kubwa ya wafanya bishara wadogo wadogo kuegesha biashara zao za kila aina pembezoni mwa njia za wapita kwa miguu jambo ambalo linasababisha usumbufu mkubwa kwa watumiaji hao wa barabara hiyo.

Licha ya usumbufu huo  na kero hiyo, eneo hilo kutokana na msongamano wa watu wengi sana, limekuwa ndio maskani kwa vibaka ambao hujipatia kipato chao bila hata ya jasho kwa kujichanganya humo kama raia wa kawaida na kufanya wizi.

Wakizungumza watumiaji mbalimbali wa barabara hiyo wamelilalamikia Jiji na Manispaa husika kwa kushindwa kuwataftia eneo husika wafanyabiashara hao wadogo wadogo na kwamba kutokana na uzembe huo mkubwa wakuto wazuia nao wameamua kuendelea kuleta kero

"Eneo hili kwa kweli linatia Aibu sana kwa sababu hapa ndipo Lango kuu la kuingia jijini na mara watu wanapo ingia wanakutana na kero hii ambayo mimi binafsi naita ni uchafu, nasikitika sana kuona Jiji na Halmashari husika wameshindwa kabisa kudhibiti na kuwataftia eneo husika hii ni aibu" 

Alizungumza mmoja wa watumiaji wa barabara hiyo ambaye hupita mara kwa mara.

Hizi ni Picha zilizopigwa moja kwa moja katika eneo hilo...   

  
 Hawa nao wanauza Viatu pande hizi kwa bei nafuu...
 Wengine wanauza samaki katika eneo ambalo kiafya sio sahihi
 Wenye kuuza Nguo za ndani katika eneo kama hili nao wapo ingawa napo kiafya sio nzuri yaweza sababisha magonjwa ya ngozi kwa sababu watu wengi wanaonunua huishia kuvaa moja kwa moja bila hata kufua
 Hawa wametundika Suluali pembezoni mwa Barabara
 Eneo hili lina vumbi na huku wakiwa wameanika T-Shirt zao na kuuza kitendo kinacho sababisha kupatwa vumbi na kuhatarisha afya za watumiaji.
 Wengine wanauza Urembo pamoja na makasha ya simu
 Hii kali sana hawa Jamaa wanauza DVD kwa Tsh 500 hadi 1,000 bei ya juu sasa swali linakuja hapa kuna kazi za Nje na ndani ya Tanzania Je Haki miliki Mpo? na watu wa mapato hili mnalionaje?
 Wauza Radio kwa Bei nafuu sana nao wapo
 Huu ni uzibe wa Barabara kuu na wapita kwa miguu lakini vya kuzibia vimejaa nguo mbalimbali je Hiyo ni sehemu halali ya kufanyia Biashara?
 Katika eneo hili la Ubungo sio pembezoni mwa barabara pekee lakini hadi mabondeni biashara zinaendelea kwa kasi.
 Hawa nao wapo wanauza Vioo vya kujitazamia pamoja na vifaa vya kuegeshea nguo
 Mikanda ya nguo mbalimbali nayo inauzwa katika eneo hili
 Miwani ya wakubwa na watoto nayo ipo kwa bei poa
 Ma bukta yakutosha yanauzwa eneo hili , yakiwa yamepigwa vumbi la kutosha
 Hii ndiyo hali Halisi ya eneo kutoka Ubungo Darajani karibia na mitambo ya Gesi hadi eneo la watu wanaopandia magari ya kwenda Mwenge? Je Halmashauri ya Jiji hamlioni hili? Je Manispaa husikia nanyie hamlioni hili? Au hili ni eneo halali limepitishwa kwa ajili ya kufanya biashara hizi?



 Picha na Dar es salaam yetu

DTBi - COSTECH WATILIANA SAINI YA USHIRIKIANO NA SILION VALLEY YA MAREKANI

Mr Carl Davis Jr, President of the Silicon Valley Black Chamber of Commerce and Eng. George Mulamula, CEO of DTBi sign MOU copy
Bw.Carl Davis Jr, Rais wa Silicon Valley Black Chamber of Commerce na Eng. George Mulamula, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi (kulia) wakisaini MOU.
Na Mwandishi Wetu, MOblog Tanzania
KAMPUNI tanzu ya Tume ya sayansi na teknolojia ya DTBi-COSTECH na Silicon Valley Black Chamber of Commerce’s Center for Entrepreneurial Development (SVCED) wametiliana saini ya Mkataba wa Makubaliano (MoU) ambapo pande zote mbili zitashirikiana kwa njia mbalimbali kwa ajili ya ukuaji wa wajasiriamali.
Mkataba huo, kati ya DTBi na SVCED utawezesha pande hizo mbili kukuza ujasiriamali na kujenga uwezo katika Habari, Teknolojia na Mawasiliano kwenye sekta zote za kiuchumi.
Mkataba huo wa MoU utawafanya wadau kufanya shughuli za biashara kwa kuanza na mfumo wa teknolojia ya habari na mawasiliano kwa kupitia njia ya mtandao na kusaidia wale walio na ubunifu katika nyanja mbalimbali za biashara.
Mr Carl Davis Jr, President of the Silicon Valley Black Chamber of Commerce and Eng. George Mulamula, CEO of DTBi shake hands after signing MOU copy
Bw. Carl Davis Jr, Rais wa Silicon Valley Black Chamber of Commerce na Eng. George Mulamula, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi kupeana mikono baada ya kusaini MOU.
Mkataba huo pia utasaidia wajasiriamali kuweza kukua na kufanya biashara kwa kutumia mifumo habari, teknolojia na mawasiliano katika kukuza ujasiriamali na kuanzisha mfumo wa kubadilishana uzoefu katika kuendeleza biashara na ukuaji wa ujasiriamali.
Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa DTBi, Injinia. George Mulamula amesema mkataba MOU utatoa ushirikishiano ambao utaruhusu wajasiriamali wa Tanzania kufaidika na ujuzi, maarifa ya Silicon Valley ya ujasiriamali.
Amesema hii itasaidia nchi ya Tanzania kuruhusu uanzishwaji wa biashara kupitia njia ya mtandao na mifumo ya Habari, teknolojia na mawasiliano katika kukuza ajira na kuchangia pato la taifa.
Mr Mulamula explains the partnership to the press copy
Eng.George Mulamula akielezea ushirikiano kwa vyombo vya habari.
Baada ya kutiliana saini ya MOU, Bw Carl Davis Jr, alikuwa na semina kwa wajasiriamali yenye jina la “The Mindset of the Silicon Valley Entrepreneur: Lessons for the Tanzania Entrepreneur/Innovator”.
Mr Davis Jr amesema anaweza kuwasaidia “wajasiriamali kuelewa jukumu la uzinduzi na ujasiriamali na jinsi Wajasiriamali hapa nchini jinsi wanavyoweza kujiinua katika kufikiri chanya kwenye maeneo ya biashara.
Mr Carl Davis Jr,  gives a talk to Tanzanian entreprenuers at DTBi copy
Bw. Carl Davis Jr, akitoa majadiliano DTBi kwa wajasiriamali wa Tanzania juu ya jinsi ya kuwa mwekezaji mwenye mafanikio.
Attendee contributing to the discussion copy
Mshiriki akichangia mjadala.

Thursday, February 27, 2014

TASWIRA KUTOKA SOKO KUU LA SANYA JUU MKOANI KILIMANJARO

Sanya Juu ni mji mdogo ndani ya wilaya Siha Mkoani Kilimanjaro ikiwa ni Km 25 toka Bomang'ombe  na KM 50 toka Moshi Mjini, weekend hii nilifanikiwa kuutembelea Mji wa Sanya Juu ambapo siku ya Jumamosi  mji huu huwa umechangamka kwa shamrashamra za kibiashara. katika pita pita zangu nilifanikiwa kulitembelea soko ila nilishangazwa na hali niliyo ikuta ya miundombinu isiyo kidhi na kulifanya soko kuonekana hatarishi kwawafanya biashara na wateja wao kiafya.
Huu ni msimu wa mvua kwa sehemu kubwa ya mkoa wa Kilimanjaro, hatua za haraka zinatakiwa kuchukuliwa kuimarisha miundombinu ya soko la Sanya Juu kuimarisha afya za wafanyabiashara na wateja wao. 

Hii ni njia ya kuelekea soko hili ikiwa imejaa matope kutokana na kuwa katika kiwango cha changarawe

Baadhi ya wachuuzi wakiwa sokoni hapo kununua mahitaji yao lakini mazingira ya soko hayaridhishi kutokana na uchafu uliokithiri hapo na kuhatatrisha afya za walaji wa bidhaa

hali halisi inavyonekana sokoni hapo baada ya mvua kunyesha

Msimu huu wa mvua unasababisha kero hii kwa baadhi ya wateja hata wafanyabiashara sokoni 

hali hii pia ni kero kwa watembea kwa miguuu  sokoni hapo 

Picha zote na mdau Wito Msafiri wa Mwanaharakati Mzalendo Blog

Top Golden Globe Award Winners 2014

The hottest stars of Hollywood came out to party at the 71st Annual 2014 Golden Globe Awards ceremony on Sunday, Jan. 12, 2014 at the Beverly Hilton hotel. Tina Fey and Amy Poehler returned as co-hosts and kept the party going with their witty SNL style zingers and hilarious digs at everyone from George Clooney to Leonardo DiCaprio. The Fey-Poehler performance alone made the 71st Golden Globes worth watching, even before the first award was handed out.
tina-amy-golden-globe-hosts

Here are the top ten big wins of the 71st Annual 2014 Golden Globe Awards:


1. Best Motion Picture – Drama: "12 Years A Slave"
12 Years a Slave, a 2013 British-American epic historical drama film is an adaptation of the 1853 memoir of the same name by Solomon Northup, a New York State-born free negro who was kidnapped and sold into slavery. Solomon worked on plantations in the state of Louisiana for twelve years before his release.

Best-Picture-Drama-12-Years-a-Slave
During its marketing campaign, 12 Years a Slave received unpaid endorsements by celebrities such as Kanye West and Sean Combs. It has received universal acclaim by critics and audiences and has been named as one of the best films of 2013 by various ongoing critics. Compared to critically acclaimed movies such as Schindler's List, 12 years of slave is considered to be a front runner for the 2014 Oscars.
12-Year-a-Slave-Cast-at-the-Golden-Globes-2

2. Best Motion Picture - Comedy Or Musical: "American Hustle"
American Hustle is a 2013 American crime comedy-drama film directed by David O. Russell and is loosely based on the FBI ABSCAM operation of the late 1970s and early '80s. It stars Christian Bale and Amy Adams as two con artists who are forced by an FBI agent to set up an elaborate sting operation on corrupt politicians, including the mayor of Camden, New Jersey.
Best-motion-picture-comedy-American Hustle
American Hustle received seven Golden Globe Award nominations; it won for Best Motion Picture – Musical or Comedy, with Amy Adams and Jennifer Lawrence winning Best Actress – Motion Picture Musical or Comedy and Best Supporting Actress – Motion Picture respectively.

3. Best Performance by an Actress in a Motion Picture – Drama: Cate Blanchett - "Blue Jasmine"
Cate Blanchett won her second Golden Globe award for her portrayal of Jeanette 'Jasmine' Francis in Woody Allen's Blue Jasmine.
best-actress-drama-cate-blanchett
4. Best Performance by an Actor in a Motion Picture – Drama: Matthew McConaughey - "Dallas Buyers Club"
This marks the first Golden Globe nomination & win for McConaughey, who lost 50 pounds for 'Dallas Buyers Club."
best-actor-drama-matthew-mcconaughey
McConaughey plays an HIV-positive patient named Ron Woodroof who smuggles anti-viral medications that are not approved in the U.S. in order to survive.
best-actor-dallas-buyers-club-
5. Best Performance by an Actress in a Motion Picture - Comedy Or Musical: Amy Adams - "American Hustle"
best-actress-comedy-or-musical-amy-adams-2
Amy Adams won for Best Performance by an Actress in a Motion Picture - Comedy or Musical for her role in "American Hustle," marking her first win and fifth nomination.
Best-actress-Amy-Adams

6. Best Performance by an Actor in a Motion Picture - Comedy Or Musical: Leonardo DiCaprio - "The Wolf of Wall Street"
This is the second Golden Globe win and 10th nomination for actor Leonardo DiCaprio.
best-actor-comedy-or-musical-Leonardo-DiCaprio

7. Best Director - Motion Picture: - "Gravity"
It was a big night for Gravity director Alfonso Cuaron, who won best director. The Mexican filmmaker joked about his thick accent when he went onstage to accept his award.
Best-director-Alfonso-Cuaron
TELEVISION
8. Best Television Series – Drama: "Breaking Bad"
A Golden Globe send off for "Breaking Bad". The gripping drama about a teacher turned meth kingpin, "Breaking Bad," capped its celebrated final season with a win for best TV drama the 71st Golden Globes in Beverly Hills. The series was nominated last year but had never won the Globe before. The show wrapped up its run in September with a finale seen by more than 10 million total viewers.
Best-television-series-drama-Breaking-Bad
9. Best Television Series - Comedy Or Musical: "Brooklyn Nine-Nine"
Andy Samberg's little-seen police sitcom Brooklyn Nine-Nine was a double winner at the Golden Globes with a best actor in a comedy win for Samberg.
Brooklyn Nine-Nine is an American action comedy television series that follows an immature detective and his relationship with his strict new captain.
Best-television-series-comedy-Brooklyn-Nine-Nine
10. Best Performance by an Actor In A Television Series – Drama: Bryan Cranston - "Breaking Bad"
best-actor-drama-Bryan-Cranston

MBUNGE MASELE AWAJENGEA UWEZO WAKINA MAMA LISHE SHINYANGA

 Mbunge wa Shinyanga mjini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Madini Ndugu Stephen Masele akizungumza kwenye mkutano na wakina Mama na Baba Lishe wa Shinyanga mjini ambapo aliwasaidia kufungua SACCOS na kuwaongezea mtaji wa biashara yao.
 Wakina Mama Lishe ambao wengi ni Wajane na Yatima wa Shinyanga mjini wakishangilia jambo wakati wa hotuba ya Mbunge wao Ndugu Stephen Masele,kwenye ukumbi wa NSSF CCM mkoa wa Shinyanga uliofanyika jana tarehe 26 Februari 2014.
 Wakina Mama Lishe ambao wengi ni Wajane na Yatima wa Shinyanga mjini wakishangilia baada ya kuwezeshwa pesa kwenye mitaji ya biashara yao Mbunge wao Ndugu Stephen Masele,kwenye ukumbi wa NSSF CCM mkoa wa Shinyanga uliofanyika jana tarehe 26 Februari 2014.
Wakina Mama Lishe ambao wengi ni Wajane na Yatima wa Shinyanga mjini wakipeana mikono na  Mbunge wao Ndugu Stephen Masele baada ya kuwawezesha kuwa na SACCOSS pia kuwasaidia mtaji wa zaidi ya shilingi milioni nane,kwenye ukumbi wa NSSF CCM mkoa wa Shinyanga uliofanyika jana tarehe 26 Februari 2014.

NAPE AUNGURUMA SHINYANGA AWAZOA WAWILI KUTOKA CHADEMA

 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akiangalia matembezi ya mshikamano wakati yakiingia uwanjani kabla hajaanza kuhutubia wakazi wa Shinyanga mjini.
 Wakazi wa Shinyanga mjini wakiwa na Furaha ya kuwakaribisha wanachama wapya ambao walikuwa madiwani kwa kupitia Chadema ambao tarehe 25 walijiuzuru na tarehe 26 Februari 2014 kujiunga na CCM.
 Zakaria Martin Mfuko aliyekuwa Diwani wa Chadema Kata ya Masekelo akihutubia wakazi wa Shinyanga mjini kwenye viwanja vya Mahakama ya Mwanzo na kuwaambia wananchi hao ameamua kurudi CCM kutokana na ufisadi na ukiukwaji ya maadili ya Uongozi ndani ya Chadema.
Sebastian Peter maarufu kama Obama aliyekuwa Diwani wa Chadema kata ya Ingokole akihutubia wananchi kwenye viwanja vya Mahakama ya Mwanzo mjini Shinyanga.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimsaidia kufunga vifungo vya shati Ndugu Sebastian Peter aliyekuwa Diwani wa Kata ya Ingokole ambaye amerudisha Kadi yake ya Chadema na kupokelewa rasmi CCM kwenye viwanja vya Mahakama ya Mwanzo mjni Shinyanga.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akihutubia maelfu ya wakazi wa Shinyanga mjini na kuwaambia Huu ndio Mwanzo tu,aliwaambia CCM imejengwa kwa misingi imara hivyo itaendelea kuwepo kwa muda mrefu zaidi.
Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akimpa ushauri Mbunge wa Shinyanga Mjini Ndugu  Stephen Masele juu ya VETA mkoani hapo kutoa kozi zinazoendana na mahitaji ya Soko la Viwanda vya Shinyanga kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya mahakama ya mwanzo Shinyanga mjni tarehe 26 Februari 2014.