
Na Elvan Stambuli
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa amesema ametishiwa kuuawa kwa kupigwa risasi. Dk. Slaa aliyasema hayo Jumamosi iliyopita katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam wakati wa mapokezi maalum ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliyesimamishwa kuhudhuria vikao vya bunge mpaka mwakani kutokana na hoja yake ya kuhoji mkataba wa madini uliotiwa saini nchini Uingereza na Waziri wa Madini na Nishati, Nizar Karamagi.
Akifafanua zaidi Dk. Slaa alisema ujumbe huo wa vitisho ulimfikia kwa njia ya simu yake ya kiganjani.
"Sikwenda kuripoti polisi kwa sababu aliyenitishia kuniua simu yake ilikuwa imeandika 'private', hivyo kutomjua mtu aliyenitolea vitisho hivyo wala namba yake". alisema Dk. Slaa.
Aliongeza kuwa anaamini amepewa vitisho hivyo kutokana na kugundua kwake kuwa kuna makampuni (majina tunayahifadhi) yamepoteza fedha za serikali alizodai kufikia shilingi bilioni 131.
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Wilbrod Slaa amesema ametishiwa kuuawa kwa kupigwa risasi. Dk. Slaa aliyasema hayo Jumamosi iliyopita katika viwanja vya Jangwani jijini Dar es Salaam wakati wa mapokezi maalum ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe aliyesimamishwa kuhudhuria vikao vya bunge mpaka mwakani kutokana na hoja yake ya kuhoji mkataba wa madini uliotiwa saini nchini Uingereza na Waziri wa Madini na Nishati, Nizar Karamagi.
Akifafanua zaidi Dk. Slaa alisema ujumbe huo wa vitisho ulimfikia kwa njia ya simu yake ya kiganjani.
"Sikwenda kuripoti polisi kwa sababu aliyenitishia kuniua simu yake ilikuwa imeandika 'private', hivyo kutomjua mtu aliyenitolea vitisho hivyo wala namba yake". alisema Dk. Slaa.
Aliongeza kuwa anaamini amepewa vitisho hivyo kutokana na kugundua kwake kuwa kuna makampuni (majina tunayahifadhi) yamepoteza fedha za serikali alizodai kufikia shilingi bilioni 131.
"Nchi hii haina wenyewe, ndege ya uchumi inayopaa aliyoisema Waziri Mkuu ni yao sio yetu," alisema Dk Slaa na kushangiliwa na wananchi waliokuwa hawajali kunyeshewa mvua iliyokuwa ikinyesha kwa nguvu.

Alisema alimuandikia barua Spika wa Bunge, Samueli Sitta na kumtaarifu kuwa anaondoa hoja yake lakini atatafuta njia mbadala wa kushughulikia ubadhirifu wa Benki Kuu ya Tanzania.




1 comment:
Naupongeza sana ujasiri alionao kijana mwenzetu Zito kabwe ni dalili tosha kuwa sasa vijana tunaweza kishika madaraka na hilo ni wajibu wazee aliokuwa vilaza kipindi cha ujana wao mpaka leo ni vilaza tu tuamke vijana tutajibu nini mbele za mungu tumeutumiaje ujane wetu? tabia za starehe na ngono tuwaachie wazee walishamiliza deni lao
sisi kwa mbinu yeyote tuitoe tanzania katika umaskini uliopindukia
wabunge wetu hawana hekima sina ushahidi likini ni wangapi walifahamu swala la alilodokeza Mh. kabwe kabla?
lakini hawaoni ushupavu huo bado wakapigakura asurubiwe huo ni unafiki.
watanzania tuamke tuache ushabiki wa kijinga lazima tuongeze nguvu ya upande wa upinzani tuinyooshe serikali bila hivyo tutalia kilio cha samaki
Post a Comment