Monday, November 16, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!

Omarion ajikunja na Rihanna!
Ebwana Dah! Ipo hewani tena na leo tunaye memba wa zamani wa Kundi la B2K, Omarion ambaye listi yake si ndefu lakini mtu mmoja ambaye ameweza kutokana naye ni mshangao.

Kwa mujibu wa tovuti ambayo ime-specialize katika eneo la staa gani katoka na nani, mrembo Debra ndiye anayetajwa nambari moja kutoka na ‘bwa mdogo’ huyo mwenye uwezo mkubwa wa kumiliki jukwaa. Mrembo wa pili anayetajwa ni Robyn Rihanna Fenty ambaye alitoka naye mwaka 2007, lakini haitajwi ni lini waliachana.

Kumbukumbu zinaonesha pia kuwa ni mwaka huo huo (2007) Rihanna alianza kutoka na dogo wa R&B na Pop mwenye kismati, Chris Brown a.k.a Ngumi Jiwe. Hii inamaana kuwa kwa mwaka mmoja, Rihanna alikuwa na Omarion, pia Chris Brown, ingawa haijulikani ni nani alianza au pengine alikuwa anawachanganya.

Omarion jina lake kamili ni Omari Ishmael Grandberry, ana umri wa miaka 25, alizaliwa Novemba 12, 1984, Inglewood, California, Marekani. Urefu wake ni futi 5.7, dini yake ni Mkristo.
****************************

Busta Rhymes live ndani ya Fiesta J’mosi
Mkali wa vocal za kigumu nchini Marekani, Busta Rhymes atakuwa live kwenye Viwanja vya Posta, Barabara ya Ali Hassan Miwinyi, Mikocheni, Dar es Salaam na kugonga shoo ya kiwango.

Awali, Busta alikuwa afanye makamuzi hayo wiki mbili zilizopita, lakini iliahirishwa baada ya Kampuni ya Clouds Entertainment Company Ltd inayoratibu shoo hiyo, kupatwa na msiba mzito. Clouds, ilifiwa na Mwenyekiti wake, marehemu Alex Mkama Kusaga, hivyo kusababisha Fiesta 2009 kuahirishwa kwa wiki mbili mbele.

Kwa mujibu wa waratibu, wasanii wote waliokuwa wamepangwa kutumbuiza siku hiyo, watakuwa ndani ya nyumba kwa ajili ya kufanya kile ambacho kinatakiwa na wengi. Hey, hii si ya kukosa, ni pale pale viwanja vya posta ambavyo vinatazamana na Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama, Dar.
*******************

R. Kelly ndani ya Kampala very soon!
Mfalme wa R&B asiyepingika, Robert Kelly ameridhia mwaliko wa kutua nchi jirani ya Uganda na kufanya shoo ya kiutu uzima.

Habari kutoka mtandaoni zinasema kuwa, R Kelly atatia maguu Kampala, Uganda na kufanya kweli katika viwanja vya Lugogo Cricket Oval , Januari mwakani. Imewekwa kweupe kwamba ujio wa R Kelly umefanikishwa kwa kiasi kikubwa kwa udhamini wa Kampuni ya Simu za Mkononi ya Zain.
***********************

Kuwapa featuring mastaa ni kuharibu kazi
Hili haliwezi kupita, Abby Cool & MC George over the weekend ni lazima itoe salamu kuhusiana tabia ya baadhi ya mastaa kupenda kuharibu nyimbo za underground bila huruma. Yeah, hii imebainika kuwa wengi hufanya hivyo ili kuwabania watoto wasiamke.

Iko hivi, inaelezwa kuwa mastaa wengi wanaposhirikishwa na underground kwenye kazi fulani fulani, hufanya chini ya kiwango kwenye audio na hata video ili kuwabania vijana wasitambulike katika level za wajanja.

Yap, mastaa huboronga na kufanyakazi chini ya kiwango ili kuharibu kazi ya msanii, lengo ni kwamba ikitoka ionekane takataka, na kuwafanya madogo wasijulikane kwa sababu viwango vyao vinaonekana ni vidogo wakati kumbe wamesalitiwa. Mfano ni huu, singo inayokwenda kwa jina la Mariam ambayo ni mali ya wasanii mapacha, Johnson na Jackson a.k.a P. Square wa Bongo, imeharibiwa na mkali wa swaga, Rashid Makwilo ‘Chid Benz’.

Safu hii, iliiangalia traki hiyo kideoni, pia ikaifutilia katika audio na kubaini kuwa Chid alifanyakazi chini ya kiwango. Vocal ni kama kalazimishwa, kwenye video ndiyo kabisa, swaga hazionekani kabisa.

Hiyo siyo fresh, haipendezi kuharibiana kazi, huko mbele wajanja wakishirikishwa huwa wanagonga standard kama vile ni kazi yake, lakini huku duh! Kuharibiana ndiyo kama kazi. Unaona traki ya mwenzako ikisimama itafanyabiashara, kwahiyo unamharibia.

Mbaya zaidi washikaji wanakuchangia ela ya mafuta ya kwenda na kurudi home, ni vema kama hutaki ukakataa kuliko kuharibu. Ni mastaa wengi wenye tabia hiyo. Safu hii inawaonya kuwa makini, vinginevyo one day itadondoka na ripoti kamili na kutaja madudu yao yote.
****************

Nay agonga kolabo na aliowadisi
Mkali wa Hip Hop anayevuma na traki inayokwenda kwa jina la Itafahamika, Nay wa Mitego ameamua kuunda remix ya ngoma yake hiyo huku akiwa amefanya kolabo na baadhi ya artists aliowadisi.

Itafahamika traki ambayo inasumbua kitaani, huku ikishika chati mbalimbali ikiwemo Bamiza ya Magic FM, ni ngoma ambayo inawagonga live baadhi ya wakali waliovuma kitambo lakini sasa hivi wamefunikwa.

Wakali kama Joseph Rushahu ‘Bwana Misosi’, Haroun Kahena ‘Inspector’, Zainabu Lipangile ‘Zay B’, Paul Matthysse ‘P. Funk’ ni baadhi ya waliochanwa kwenye verse za wimbo huo. Hata hivyo, Nay akipiga stori na safu hii, amenena kuwa amewapa featuring baadhi ya artists aliowadisi ili kuonesha kuwa hakuwagonga kwa bifu, isipokuwa ni mtazamo wa kisanii tu. Katika remix ya Itafahamika, Sister P, Squezeer, O-Ten, Mansulee, Dalaza, Kimbuka na wengine wameingiza vocal.

****************

No comments: