Monday, November 16, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!




Eliza na Remtulla
Eliza Na ishuz za 5star party
Product ya Bongo iliyokuwa ndani ya mjengo wa Big Brother Revolution, Elizabeth Gupta ‘Queen’, wikiendi iliyiopita alifanya sherehe yenye level ya 5stars, ikiwajumuisha mastaa kibao nchini.

Party hiyo kiwango, ilichukua nafasi ndani ya Club Bilicanas kwenye Ukumbi wa Much Mo, usiku wa kuamkia Jumamosi, ikiwa ni maalum kwa kupongeza ushiriki wa Queen Eliza katika mjengo wa Big Brother na kumkaribisha nyumbani.

Mara tu alipodaka kinasa sauti, Eliza aliwashukuru Wabongo kwa kumkubali na kumpa sapoti ya kutosha kwa kipindi chote alichokaa mjengoni kabla ya kutolewa kwa zengwe. Aidha, Queen Eliza alionesha ufundi wa kucheza muziki, na kuuchangamsha ukumbi ambao sehemu kubwa ilikubali kwamba mtoto anaweza kumwaga swaga.

Jokate Mwegelo, Nasreen Karim, Mwanamitindo Ally Remtula, Ambwene Yesaye ‘AY’, Hamis Mandi ‘B12’ ni, baadhi ya mastaa waliokuwepo katika 5star party hiyo. *************************

compiled by mc george

No comments: