Friday, August 7, 2009

Ajali zilizotokea Kiajabu Ajabu!




IJUMAA SHOWBIZ!

Chameleone amjaza mimba nyingine mkewe
The wonderful vocalist from UG, Joseph Mayanja ‘Chameleone’ ameonesha uwezo katika sanaa ya kujaza watu duniani, baada ya kumpachika mimba nyingine mkewe, Daniela Atim.

Ijumaa Showbiz inakujulisha kuwa hivi sasa Chameleone anatarajia kupata mtoto wa tatu kutoka kwa Daniela ambaye mpaka sasa amekwisha give birth mara mbili watoto wa kiume, Abba na Alfa Mayanja.

Mbali na hilo, hivi karibuni Chameleone alizindua mfuko wa kusaidia watu wasiojiweza kwa kushirikiana na makampuni mawili ya vinywaji pande za UG, Nile na Crown Beverages.
*****************************************

Hii ni Dar mpaka Moro, Dom
Baada ya kuangusha shoo kadhaa za utambulisho wa albamu tatu kwa mpigo katika mikoa ya Rukwa, Mbeya na Iringa, makundi mawili ya muziki wa kizazi kipya, TMK Wanaume Family na Tip Top Connection yaliyoungana na kupiga kazi pamoja sasa yanageuzia mashambulizi Morogoro na Dodoma.

Akipiga stori na safu hii memba wa TMK, Said Juma ‘Chege’ alisema kuwa mizuka imeshapanda kwa ajili ya kusababisha Moro ambako zitatambulishwa albamu nne, Mtoto wa Kichaga ya Amani James Temba ‘Mh’, Pesa ya Hamad Ally ‘Madee’, Ripoti Kamili ya Tundaman na Spark bila kuiweka kando, Mkubwa na Wanawe ya Said Fella ‘Mkubwa’.

Chege ambaye amesimama vilivyo katika wimbo Running Roll ambao amepewa featuring na mwanadada Wahu, alisema kuwa katika ziara hiyo ambayo wameipa jina la Wanaume Family na Tip Top Kazini Tour, wakiwa Moro watakamua kwenye Ukumbi wa Bwalo la Umwema na baadaye Uwanja wa Jamhuri.

“Siku inayofuata tutadondoka Dom ambako nako tutasimamisha mizuka kwenye Uwanja wa Jamhuri,” alisema Chege ambaye katika wimbo huo aliofanya na Wahu, ameonesha kiwango cha kijanja.
*****************************************************

Exclusive: K-Sher avuta mkoko mpya
Hii ni exclusive, mwanadada wa Bongo Flava, Khadija Shaaban ‘Keisha’ hivi sasa atakuwa adimu kwenye vituo vya madereza tax kama ilivyokuwa zamani na kwenye daladala ndiyo kabisaaaa!

Iko hivi, Keisha ambaye ni mwanamuziki bora wa kike 2008-09, kwa mujibu wa Tuzo za Dandu, ametungua ndinga mpya aina ya Toyota Vitz na akikatiza nalo kitaani utalishuhudia likiwa na rangi nyekundu huku namba zake za usajili zikisomeka T 771 BBK.

“Nimeipenda sana plate no. yangu, ile BBK ni kirefu cha Baby Keisha,” alichonga Keisha kwa mapozi. Hey Baby Keisha, u deserve congratulation mama, ndo' ustaa wenyewe wa kibongo!
**************

Wasanii wanaotarajiwa kupiga kazi ndani ya muvi ya Tears On Valentine iliyoandaliwa na Kampuni ya Tollywood Movies wamemaliza mazoezi ya nguvu (kama wanavyoonekana pichani) na wanatarajiwa kuanza shooting wiki ijayo na wameahidi kutoa muvi kali kuliko zote.
*****************************

Ijumaa Sexiest Bachelor
Ni mchuano wa kijanja, guys wenye mguso wa kimahaba ndiyo wanaoshindanishwa hapa. Msanii Steven Kanumba, ambaye kwa sasa anatamba na sinema yake mpya ya The Director, ndiye anayeshikilia taji la Ijumaa Sexiest Bachelor na mwaka huu amependekezwa tena kuingia shindanoni.

Kazi yako ya awali uliyotakiwa kuifanya umeitekeleza ipasavyo. God bless u! Kupitia kura uliyoidondosha kwetu, tumeweza kupata orodha ya kukata na shoka ambayo inakuijia hapo chini.

Unachonatakiwa kufanya ni kupiga kura ili tubakize watu 12 wiki ijayo. Inawezekana Mtanzania. Angalia majina kwa makini kisha tuma kura yako kwenye simu namba 0787- 110173 ukimtaja mtu ambaye unadhani anastahili kuendelea kuwepo shindanoni.

Majina ni haya; Hemedi, Marlaw, Gwamaka Kaihula ‘Gk’, Steven Kanumba, Yusuf Mlela, Vincent Kigosi ‘Ray’, Adamu Mchomvu, Mwisho Mwampamba, Kalapina, Dudubaya, P. Funk, Shija, Black Rhino, Mb Dog, Tundaman, Benn Kinyaiya, Spark, Dully Sykes, Chid Benzi, Tino, Jumbe Yusuf, Jerry Tegete, Ally Mustafa, Chege, Makamua na Mr. Blue.
Wengine ni AY, MwanaFA, Ally Mustafa, Henry Joseph, Hessein Machozi, Fid Q, Niki wa 2, Hermy B, Jay Moe na Johmakini.
*************************

Monday, August 3, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!


Madhila no. 2: Itawaliza wengi
Nakala ya pili ya muvi inayokwenda kwa jina la Madhila (Part II) inaweza kuweka rekodi ya kuwaliza watazamaji wengi zaidi, Abby Cool & MC George imeichungulia na kujionea tofauti.

Ndani ya Madhila Part II, mateso kwa kijana Salim Mbwana ambaye anabeba uhusika wa jamii ya watu wenye ulemavu ni makubwa kuliko ilivyokuwa kwenye nakala ya kwanza, pia inaonesha jinsi walemavu wanavyoonekana si kitu ndani ya familia zao.

Hata hivyo, pamoja na mateso hayo baadaye Mbwana ambaye ni mlemavu katika hali halisi, anaonesha jinsi ambavyo mdharau mwiba, guu linaweza kuota tende, anafanya ‘wandaz’ kwa kudhihirisha kuwa kumbe inawezekana.

Hili ni dude lingine ambalo limekwenda kidato, na litaingizwa kitaani kwa ufanisi wa hali ya juu na kampuni mkombozi wa vipaji nchini ya Tollywood Movies.

Ndani ya filamu hiyo, pia yumo galacha Riyama Ali, staa wa tangazo la Haki Elimu, Nuru Njaidi (Huba) na wengine kibao wakiwemo Joyce Eliya (Bi. Mashavu), Subira Waziri (Kuluthum), Alfred Malima (Smart), Rahima Salim (Radia, Naima Salim (Nadia) na Jacob Daudi (Sam).
*******************************


The Director ya Kanumba kitaani J5,
Staa wa sanaa za maigizo nchini, Steven Kanumba, ameonesha umakini wa hali ya juu kazini na Jumatano anatarajia kudondosha mtaani muvi ambayo imesimama kwa jina la The Director.

Hii inakuwa ni sinema yake nyingine kucheza na Wanigeria kwa mafanikio makubwa, kama vile ilivyokuwa Dar to Lagos, Cross My Sin ambazo zilifanya vizuri sana katika soko la muvi za kibongo.
**********************************


Wasanii Tears on Valentine Day wakiwa mazoezini kambini

****************************************************8

Tuzo za Channel O
Piga kura kwa Black Rhino, FA
Once again, Mtanzania unaweza kuwa daraja la wasanii wawili nchini, kuibuka na tuzo ya kimataifa. Wanazungumziwa Nicolas Haule ‘Black Rhino’ na Hamis Mwinjuma ‘MwanaFA’.

Bila shaka unajua kilichopo kwamba Black na FA ni among the nominees kwenye tuzo za Channel O 2008-09, hivyo unatakiwa kudondosha kura yako kwa wanetu hao.

It easy to make them hero! Black kupitia wimbo wake Black Chata, ametajwa kwenye categories mbili, Video Bora Afrika Mashariki (Most Gifted East Afrika Video) na Video Bora ya Hip Hop (Most Gifted Hip Hop Video).

FA pia kupitia ngoma yake Naongea na Wewe ambayo amefanya kolabo na Ambwene Yesaya ‘AY’ ametajwa kwenye vipengele viwili, Video Bora Afrika Mashariki (Most Gifted East Afrika Video) na Wimbo Bora wa Kushirikiana (Most Gifted Group a.k.a Duo).

Utaona kwamba Black na FA wanakamuana pua kwenye category moja ambayo ni Video Bora Afrika Mashariki; lakini siyo ishu, muhimu hapa ni kuleta heshima home.
Unawezaje kupiga kura? Video Bora Afrika Mashariki, kwa Black tuma SMS yenye maneno 13E kwenda namba +27839208400 au FA, unaandika 13B unatuma kwenye nambari +27839208400.

Video Bora ya Hip Hop, unampigia kura Blak kwa kuandika SMS yenye maneno 10F na unaituma kwenda nambari +27839208400, wakati ili FA ashinde Wimbo Bora wa Kushirikiana, unaandika meseji yenye maneno 4E kisha unai-send namba +27839208400. Inawezekana!
*******************************

TMK family, Tip Top
Almanusura wauwe!
Ishu kibao zimesharipotiwa about muungano wa TMK Wanaume Family na Tip Top Connection, lakini hili linaweza likawashangaza wengi. Do u know which is ringing the bell? Guyz wamethibitisha kwamba Bong Flava is still alive.

Siku chache zilizopita jamaa almanusura wapoteze maisha ya baadhi ya mashabiki wao ambao walifurika kunako shoo yao kubwa iliyochukua nafasi pande za Iringa, wakati washkaji walipokuwa wakiutambulisha umoja wao kupitia pini linalosimama kwa jina la Chama Kubwa.

Mbali na ngoma hiyo, familia hizo mbili kongwe katika industry ya burudani Bongo, zilichukua nafasi kutambulisha albamu za wasanii wake watatu, Amani James Temba ‘Mheshimiwa’, Hamad Ali ‘Madee’ na Said Fella ‘Mkubwa’.

“Tulianza Sumbawanga, tukashuka Mbeya kisha tukamalizia Iringa. Kiukweli shoo zote zilikuwa na mafanikio makubwa lakini Iringa ilikuwa balaa zaidi.

“Mashabiki walifurika Uwanja wa Samora mpaka baadhi yao kuchungulia kifo kutokana na msongamano. Tunamshukuru Mungu ulinzi ulikuwa wa kutosha, askari walilazimika kuwachomoa wale waliokuwa wamebanwa ili kunusuru maisha yao,” alisema Fella.

Mkubwa pia aliongeza kuwa baada ya mafanikio hayo, hivi sasa wanajipanga kwa mashambulizi mengine kwa ajili ya Moro ambako watakita nyama chini kwenye Uwamnja wa Jamhuri na Bwalo kabla ya kutua Dom kwenye Dimba la Jamhuri.
******************************

Lil mama: Alivyochangia penzi la Chriss Brown na Rihanna
She is underage but kwenye malavidavi anaonekana kuyachangamkia kwa sana. Mtajwa hapo ni rapa, Niatia Jessica Kirkland a.k.a Lil Mama.

Oktoba 4, mwaka huu ndiyo atatimiza miaka 20, hivyo bado anajidai na 19, lakini inafunuliwa kuwa miaka miwili iliyopita (2007) akiwa na miaka 17 alikuwa akijikunja kimahaba na mwanamuziki handsome boy, Chris Brown.

Mshangao ni kwamba wakati huo Lil Mama akitoa urojo kwa Chris, dogo huyo ndiyo kwanza alikuwa analinogesha penzi kwa sweet-baby wake, Robyn Rihanna Fenty, kwa maana hiyo alikuwa anawachanganya.

Hata hivyo, Lil Mama hana listi ndefu, kwani katika tovuti inayodili na ishuz za mastaa wa kiwanja, inaonekana kwamba mbali na kuchangia penzi la Chris na Rihanna, pia kipindi cha mwaka 2007 hadi 2008 alijiweka kwa Soulja Boy.

Alizaliwa Harlem, Manhattan, New York Oktoba 4, 1989. Nyota yake Mzani, ana urefu wa futi 5.65, rangi ya macho yake ni Brown-Dark, dini yake ni Mkristo na alibukua Edward R. Murrow High School.

compiled by mc george