Thursday, July 7, 2011

FFU! Ngoma Africa Band kuvamia Internationals African Festival Tübingen,Germany


       Mabakuli ya "Supu ya Mawe" uwanjani kila moja na lake!
     "FFU kwa hasira wamerusha song  jipya "Supu ya Mawe" hewani "

Bendi maarufu ya mziki wa dansi barani ulaya "Ngoma Africa Band" aka FFU,kinatarajiwa kutumbuiza
 jukwaani tena katika onyesho kubwa la aina yake African Internationals Festival,mjini Tübingen,ujerumani siku ya jumamosi 16.julai 2011.
FFU hao wamziki pia wamepakua jikoni wimbo mpya uliobeba jina "SUPU YA MAWE" wimbi wenye ujumbe
mahusus kwa walimwengu ,ambao kwa sasa unasikia katika kambi ya FFU  at www.ngoma-africa.com, wimbo huo utunzi wake kamanda Ras Makunja akiimba kwa kushirikiana na Christian Bakotessa aka Chris-B aka "Mshenzi" wa gitaa la solo.Wimbo huo "Supu ya Mawe"
ujumbe uliomo katika wimbo huo unaonekana kuwa na nguvu na vitamin zote za maisha kuliko kikombe cha dawa.
kutokana na taarifa la gazeti moja la kimataifa hili http://www.africa-news.eu/entertainment/44-entertainment/2815-welcome-to-international-african-festival-in-tubingen-germany.html  bendi hiyo maarufu inazidi kupata umaarufu na kujizolea washabiki kiaina yake katika kila kona.
Usikose kuwasikiliza

1 comment:

Anonymous said...

Vichaa FFU,kazi yenu inakubalika kimataifa nyinyi ni mzimu wa mziki