Saturday, March 5, 2011

MBEYA YETU


JINA LA BLOG: MBEYA YETU
Tunapenda kulitambulisha wadau wote libeneke jipya la Mbeya Yetu ambapo nia na malengo ni kuwaletea habari mbali mbali kutoka Jijini Mbeya, Tanzania na Duniani kwa Ujumla ikiwa unatukio la aina lolote usisite kututumia kupitia mbeyayetu@yahoo.com . karibuni nyote na asanteni kwa kututembelea.

Kwa pamoja tunaweza.

Thursday, March 3, 2011

OCHU AJA NA 'Umechakachuwa'

POLENI KWA UJENZI WA TAIFA NA NAAMINI MU WAZIMA WA AFYA TELE

STUDIO MPYA YA SEDUCTIVE RECORDS INAPENDA KUWAPA NAFASI WADAU, MARAFIKI NA WAPENZI WOTE WA MUZIKI WA BONGO FLEVA KUSIKILIZAA SINGLE YA PILI YA MSANII OCHU EDDY SHEGGY AU KWA JINA LA KISANII OCHU

SINGLE HIYO INAITWA "UMECHAKACHUWA" IMEREKODIWA NA PRODUCER JILLY BABY WA SEDUCTIVE RECORDS NA PIA IMESHAFANYIWA MUSIC VIDEO YAKE CHINI YA KAMPUNI YA EMPTYSOULZ PRODUCTION AMBAYO IMESHAANZA SAMBAZWA KATIKA VITUO MBALIMBALI VYA TV.

NATUMAINI MTAENJOY KAZI HII NZURI NA PIA KUMPA SUPPORT MSANII HUYU AMBAYE ANAJARIBU KUENDEREZA SANAA HII ALIYOKUWA AKIIFANYA MAREHEMU BABA YAKE MSANII WA MUZIKI WA DANCE EDDY SHEGGY.

PIA USISITE KUANDIKA KUTOA USHAURI PALE UTAPOSIKILIZA SINGLE HII YA "UMECHAKACHUWA"

ASANTENI NA TUWE PAMOJA!

Regards:
Solomon Lamba

BONGO & BROOKLYN FLAVA

For those who missed the concert on the 9th of february here is another chance to see a great collaboration of artists. Initially we were brought together through MDGFive.com and UNFPA's efforts to raise awareness about maternal health through music. This is an independent event organised by Caravan Records to challenge, renew and fuse two powerful youth cultures. Please spread the word. The concert will take place at Triniti on FRIDAY the 4th of March. 8PM-00AM
--
Kind Regards,

Caravan Records
MANAGEMENT
Tel: +255 763 822 022
E-mail: kichaamusic@gmail.com

Wednesday, March 2, 2011

WADAU WA SANAA WAAPA KUPAMBANA NA RUSHWA, DHURUMA

Nyomi kwenye Jukwaa la Sanaa.Kwa sasa linakua kwa kasi na kuvuta watu kutoka pande mbalimbali za jiji la Dar es Salaam na vitongoji vyake.
Warembo wa miss utalii wakicheza moja ya ngoma ya asili kwenye Jukwaa la Sanaa.
Warembo wanaowania taji la Miss Utalii wakiungana na Katibu Mtendaji wa BASATA,Ghonche Materego (Katikati aliyevaa suti nyeusi) kusakata muziki uliokuwa unaporomoshwa jukwaani na msanii Vitali Maembe kwenye Jukwaa la Sanaa Jumatatu ya wiki hii.
Mkongwe wa dansi nchini Mzee Kassim Mapili (kulia) akimpa makabrasha msanii Vitali Maembe ili ayatumie kwenye mapambano dhidi ya dhuluma kwa wasanii na jamii kwa ujumla.
Baadhi ya wadau wa Jukwaa la Sanaa linalofanyika kila Jumatatu kwenye Ukumbi wa BASATA wakinyoosha mikono juu kama ishara ya kula kiapo cha kupambana na rushwa, uvivu na kutokuwajibika.Kiapo hicho kiliongozwa na Msanii maarufu wa muziki wa falsafa,Vitalii Maembe aka Sumu ya Teja.

Na Mwandishi Wetu
Wadau wa Jukwaa la Sanaa mapema wiki hii wamekula kiapo cha kupambana na rushwa pia dhuruma nchini huku wito ukitolewa kwa wasanii kuwa mstari wa mbele katika mapambano dhidi ya matatizo hayo ambayo kwa sasa yanatajwa kuwa kikwazo katika kuleta maendeleo ya mtanzania.

Akiwasilisha mada kwenye Jukwaa hilo linalofanyika kila Jumatatu kwenye Ukumbi wa Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Juu ya Wasanii na Ukombozi wa Jamii,Msanii Vitali Maembe maarufu kama Sumu ya Teja alisema kwamba,sanaa ni chombo kilichoshushwa na Mungu kwa ajili ya kuikomboa jamii dhidi ya makucha mbalimbali ikiwemo rushwa na ufisadi hivyo wadau wa sanaa hawana budi kuitumia katika kuikomboa jamii.

“Kama kuna watu watapewa adhabu na Mungu kwa kutotimiza wajibu wao ipasavyo basi ni wasanii.Mungu ametupa sanaa ambacho ni chombo chenye nguvu katika kuikomboa jamii lakini badala ya kuitumia kwa kazi hiyo,tumeigeuza chombo cha starehe, kujizolea umaarufu na kupatia wanawake” alilalamika Vitali Maembe.

Aliongeza kwamba,yeye katika kazi zake za sanaa hataacha kuimba ukweli na matatizo halisi yanayoigusa jamii ingawa kuna watu wanachukizwa na msimamo huo na kwamba anaamini ameingia kwenye tasnia hii kuikomboa jamii na wajibu wa suala hilo ni wa msanii yeyote.

“Kuna watu wanachukizwa sana na mimi kuimba ukweli na matatizo yanayoikumba jamii,mimi sitaacha kufanya hivyo hata nikitishiwa na nyimbo zangu kuzuiwa kupigwa.Sanaa imegeuzwa chombo cha starehe na kutukuza anasa wakati jamii inateketea” aliongea kwa uchungu Maembe huku akiimba nyimbo zenye ujumbe mzito kama Afrika shilingi tano,sumu ya teja na nyingine nyingi.

Katika kuhakikisha sanaa inatumika kupambana na rushwa,Vitali Maembe ameanza kampeni ya Chanjo dhidi ya rushwa, uvivu na kutowajibika ambayo kwa sasa imejikita mashuleni ambapo amekuwa akizunguka mikoa mbalimbali na kuhamasisha wanafunzi kujiepusha na vitendo hivyo ambayo vinalirudisha nyuma taifa.

Aidha,Maembe akiwa amewaomba wadau wa Jukwaa la Sanaa kunyosha mikono yao juu, aliwaongoza kutamka ahadi za Mwana TANU dhidi ya rushwa ambazo zilikuwa ni maarufu wakati Baba wa Taifa hayati Julius Kambarage Nyerere anaasisi azimio la Arusha mwaka 1967 ambapo pamoja mambo mengine lililenga kupinga dhuruma na rushwa ndani ya jamii.

Sambamba na Vitali Maembe ambaye alikonga vilivyo mioyo ya wadau wa Jukwaa, warembo wanaowania taji la Miss Utalii wanaotazamiwa kupanda jukwaani Jumamosi ya wiki hii walitoa burudani ya ngoma mbalimbali za asili na kuwa kivutio kwa wadau hao zaidi ya 200 waliohudhuria wiki hii.

Monday, February 28, 2011

HARAMBEE YA GONGO LA MBOTO LONDON ILIVYOFANA

WAKURUGENZI WA SERENGETI FREIGHT WAKITOA MCHANGO WAO
WADAU KUTOKA PANDE ZOTE ZA LONDON WAKIWA KATIKA HARAMBEE
MR & MRS KAMWANO SABUNI WAKIKABDHI MCHANGO WAO
MDAU FREDDY MACHA ALKUWA MSTARI WA MBELE KATIKA KUCHANGIA
MDAU ALI HAMISI NA RAFIKI YAKE WAKIKABIDHI MCHANGO WAO
MDAU ABUU FARAJI AKIPEWA MKONO WA ASANTE
LEMNA NA WATOTO WAKE WALIKUWA MSTARI WA MBELE KATIKA KUCHANGIA

Salaams,
Tunapenda kutoa shukrani zetu za Dhati kwa watanzania wote waishio LONDON UK walioweza kufika jana jioni AFRICAN VILLAGE BAR & RESTAURANT kuchangia waathirika wa Gongo la Mboto Tanzania. Kwa mda wa masaa mawilitumeweza kukusanya Jumla ya pesa taslim Pounds £600, pia tumekusanya Nguo nyingi kutoka kwa watu mbalimbali na vifaa vingine mbali mbali.

Ningependa kutoa shukrani za dhati kutoka URBAN PULSE,MISS JESTINA BLOG,AIL TV, LOCUS IMPEX SHIPPING CO, SHILLA FRISCH, NA Utawala wa AFRICAN VILLAGE BAR & RESTAURANT LONDON kwa kusaidia na kuwezesha kufanikiwa kwa zoezi la jana.

Mungu Ibariki AfriKa, Mungu Ibariki Tanzania
Asanteni

STREET DREAMZ

Sunday, February 27, 2011

ALFRED IS MARRIED!

Go check what went down on his wedding: harusini.blogspot.com

HARAMBEE YA GONGO LA MBOTO READING YAFANA

'Toa ndugu' ikiendela
Mtoto Chanele akimpa mchango wake Miss Jestina
Frank kutoka Urban Pulse akiwa na Tina kutoka Miss Jestina Blog baada ya harambee
Wadau wa Harambee; kutoka kushoto J J, Chisumo, Miss Jestina, Gardol na Frank

Salam,
Tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Watanzania wote waishio Reading UK walioweza kuja Leo mchana Vincent kuchangia wahangwa wa Gongo la Mboto Tanzania. Kwa mda wa saa moja tumekusanya Jumla ya pesa taslim Pounds £200. Pia tumekusanya nguo nyingi kutoka kwa watu mbalimbali. Tafadhali Kumbuka bado hujachelewa kwa wakazi wa Reading ambao hawakuweza kufika leo mnaweza kupeleka michango yenu Vincent siku ya mwisho ya kukusanya ni Jumanne ijayo tarehe 1.3.11.

Ningependa kutoa shukrani za dhati kutoka URBAN PULSE, MISS JESTINA BLOG, AIL TV, LOCUS IMPEX SHIPPING CO, SHILLA FRISCH, MRS NASIBU NA Utawala wa Vincent Restaurant Reading kwa kusaidia zoezi la leo.

Mungu Ibariki Afrika, Mungu Ibariki Tanzania
Asanteni

Falling In Love By D'Banj Feat. Genevieve


Falling In Love By D'Banj Feat. Genevieve