mwalimu(Hamza Kalala) akiwapa tafu kupiga gitaa la solo ndani ya dar live
Paul Mwanja mpiga drum wa academy akiwa mzigoni
Rapa wa Academy Rahim akifanya makamuzi
Wana Academia wakiimba wimbo wao mpya unaoitwa linda
sebene kwa kwenda mbele
Baada ya kufanikisha uundwaji wa Music Academy Tanzania chini ya usimamizi wa ASET na URBAN PULSE CREATIVE kwa mara ya kwanza wana academia walipata fursa ya kutumbuiza live stejini katika ukumbi mpya wa kisasa Dar Live uliopo mbagala siku ya jumamosi tarehe 17.3.2012
Hii ilikuwa ni mojawapo ya hatua waliopiga kuonyesha vipaji vyao na kuwajengea uzoefu kutumbuiza mbele za maelfu ya mashabiki waliojitokeza kupata burudani.
Music Academy inaendelea kutoa mafunzo na pia kutafuta vipaji vipya katika tasnia ya muziki ikiwepo kucheza, kuimba, kutunga, kurap, kupiga vyombo mbalimbali n.k na kutoa fursa ya kujiunga katika bendi, vikundi au kuanza kama solo career/ artist mara tu wanapofuzu ili kuimarisha mziki wa kitanzania na pia kuwapa vijana ajira. Mazoezi hayo yataendela kufanyika mara tatu kila wiki kwa wiki kadhaa ndani ya ukumbi wa Baobab Kinondoni Vijana.
Asanteni,
ASET na URBAN PULSE CREATIVE
No comments:
Post a Comment