Ndugu zangu,
Naitwa Maggid Mjengwa, mmiliki wa Mjengwablog na mtandao wa Kwanza Jamii. Baadhi yenu ni watembeleaji wa Mjengwablog, nawashukuru sana, na wengine ambao hamjawahi kuitembelea, basi, karibuni sana.
Nianze kwanza kwa kueleza jambo ambalo sijapata kulisema kabla. Mimi nina historia na chuo hiki.
Mwaka 2005 nilijiunga na Chuo hiki kwa minajili ya kujifunza kozi za Social na Cultural Anthropology. Nilifundishwa na marehemu Profesa Mshana.
Dhumuni la pili lilikuwa ni kujifunza juu ya mazingira wanakojifunza wasomi wa Kitanzania vijana kama nyinyi. Maana, mimi sikuwahi kusoma Chuo Kikuu hapa nchini. Nimegruduate nchini Sweden.
Nilimaliza kozi zile katika kipindi cha miezi minne na nilifaulu vema. Kisha nikaondoka. Sikuhitaji cheti.

Ndugu zangu,
Taaluma ya habari inahusiana kwa wanahabari kusema yalo ya ukweli kwa jamii. Na jambo hili lina changamoto zake katika jamii zetu hizi.
Maana, ukweli.... Soma zaidi...http://www.mjengwablog.com/habari-za-kijamii/item/2780-hotuba-yangu-chuo-kikuu-cha-tumaini-iringa-jana-mchana.html