Ndugu
zangu,
Leo
Taifa Stars yetu inashuka tena uwanjani kwenye moja ya mechi muhimu sana kuwahi
kuchezwa. Kimsingi, leo tunapigania safari mbili; ya Brazil na Morroco kwenye
Afcon. Ni kwa vile Morocco inatarajiwa kuwa mwenyeji wa mnichuano hiyo 2015.
Mshindi
wa pili kwenye safari ya kwenda Brazil anaingia moja kwa moja kwenye michuano
ya fainali za Mataifa ya Afrika. Mara ya mwisho Tanzania kushiriki fainali hizo
ilikuwa mwaka 1980.
Tafsiri
yake?Leo tunalazimika kushinda ili tuwe na matumaini ya kwenda Brazil na hata kushika nafasi ya pili na kwenda AFCON. Tukifungwa leo ina maana ya hata safari yetu ya AFCON 2015 kuwa ngumu pia.
Kama ninavyosema mara nyingi, kuwa kandanda ina miujiza yake na imetokea zaidi ya mara elfu moja. Leo tikiwafunga Ivory Coast . Kisha Ivory Ciast wakafungwa na Morocco, na sisi tukawafunga Gambia kwao, basi, ina maana tunakwenda Brazil.
Cha
kujiadhari?
Tuukubali
ukweli, kuwa Ivory Coast ni timu kubwa na ina wachezaji wakubwa na wenye
uzoefu. Kimsingi ina wachezaji ambao, wanaweza kufanya lolote lile na wakati
wowote ule wakiwa uwanjani. Hivyo, ni timu ya kuiheshimu lakini si kuigopa.
Ivory Coast wanafungika, lakini lazima wachezaji wetu wajitume kwa dakika zote
za mchezo.
Kila
la Heri Taifa Stars Yetu!
Maggid,
Iringa.
0754
678 252
http://mjengwablog.com
No comments:
Post a Comment