By Willliam Kaijage
UTANGULIZI (PREAMBLE)
•Mwanzoni mwa mwezi wa 7 ndio nusu ya mwaka. Zinakuwa
zimepita siku 182 (au 183 kwa mwaka mrefu) na kubaki siku 182.
•Yafuatayo ni matukio makubwa ya muziki wa dansi kwa nusu
ya kwanza ya mwaka huu wa 2015
BENDI MPYA
•Tarehe 31-Jan-2015, BMM Classic Band, ilizinduliwa katika
ukumbi wa BMM Mwenge, opposite TRA.
•Tarehe 21-Feb-2015,
JJ Band yazinduliwa katika ukumbi wa. JJ Band ni bendi dada ya Skylight
Band itakayokuwa inatumbuiza mjini Mwanza katika hotel ya Jembe ni Jembe Resort.
•Tarehe
06-Mar-2015 (Ijumaa), Ruby Band ilitambulishwa rasmi katika ukumbi wa Coco
Beach Pub ambapo pia ilizindua video ya wimbo mpya wa “Noma”.
•Tarehe 18-Jul-2015 (Jumamosi), Stars Band yazinduliwa
katika ukumbi wa Mzalendo Pub. Bendi hiyo inaongozwa na mwanamuziki Aneth
Kushaba aka “AK47” aliyekuwa Skylight Band. Meneja wa bendi ni mpiga drums
James Kibosho.
UZINDUZI WA ALBUM MPYA
•Mpaka sasa (zaidi ya nusu mwaka) hakuna album yoyote
mpya hata moja iliyozinduliwa.
KILI MUSIC AWARD
•Tarehe 23-Mar-2015, Kililimanjaro Music Award 2015
yazinduliwa rasmi
•Tarehe 25-Apr-2015, Academy
ya Kili Music Award yakutana kuchagua majina ya washiriki wa kila kipengele.
•Tarehe 29-Apr-2015, majina
ya washiriki wa kila kipengele yatangazwa rasmi
•Tarehe 13-Jun-2015 (Jumamosi), sherehe za washindi wa Kili
Music Award 2015 zilifanyika katika ukumbi wa Mlimani City. Kulikuwa na jumla
ya vipengele (categories) 6 vya muziki
wa dansi. Washindi walikuwa kama ifuatavyo;
1. Bendi Bora ya Mwaka- FM Academia
1. Bendi Bora ya Mwaka- FM Academia
2. Mtunzi Bora wa Mwaka Bendi-Jose Mara (Mapacha Watatu)
3. Rapa Bora wa Mwaka Bendi- Fergusson (Mashujaa Band)
4. Wimbo wa Kiswahili Bendi- ”Wale Wale” (Vijana Ngwasuma)
5. Mwimbaji Bora wa Kiume Bendi- Jose Mara (Mapacha Watatu)
6. Mtayarishaji Bora wa Nyimbo Bendi-Amoroso Sound
NB: Mwaka huu hakukuwa na Mwimbaji Bora wa Kike Bendi
WANAMUZIKI WALIOFARIKI
•Tarehe 04-Jan-2015 (Jumapili), mwanamuziki wa Flowin aka
“Kachumbari” aliyekuwa mpiga drums na tumba wa Chuchu Sound afariki dunia.
•Tarehe 30-Jan-2015, mwanamuziki Peter Kanuti afariki
dunia kwa ajali ya gari akiwa Zanzibar. Huyu anatokea familia ya wanamuziki
Gaspar Kanuti, Fred Kanuti na Joseph Kanuti.
•Tarehe 28-Feb-2015, mwanamuziki, mwanasiasa, mwanajeshi
mstaafu, mbunge wa jimbo la Mbinga Magharibi, Mkurugenzi wa kundi la sanaa za
maonesho la Tanzania One Theatre (TOT Plus) Captain John Damian Komba afariki
dunia
•Tarehe 16-Apr-2015, mwanamuziki Joseph Chigwele “Che”
Mundugwao afarikia dunia.
•Mwanamuziki Mutombo Lufungula “Audax” mmoja ya
waanzilishi na wamiliki wa bendi ya Maquis du Zaire (ambayo baadaye ikaitwa
Maquis Original) afariki dunia alfajiri ya alhamis tarehe 23-Apr-2015 na
kuzikwa Jumapili ya tarehe 26-Apr-2015 katika makaburi ya Kinondoni.
•Tarehe 17-Jul-2015 (Ijumaa), mwanamuziki Ramadhan Ally
Masanja aka “Banza Stone” afariki dunia siku ya mwisho ya mwezi mtukufu wa
Ramadhan. Azikwa Jumamosi tarehe 18-Jul-2015 sikuu kuu ya Idd Mosi (Eid al
Fitr) katika makaburi ya Sinza.
MATUKIO MENGINE MAKUBWA
•Tarehe 18-Jan-2015 (Jumapili), Ali Choki apanda jukwaa
la Twanga Pepeta siku Twanga walipokuwa wakitumbuiza Leaders Club na kusalimia
kisanii. Tukio hili halijawahi kutokea tangu Ali Choki alipohama Twanga Pepeta
mwaka 2008 na kwenda kujiunga na TOT Plus.
•Ndani ya siku 3 kuanzia 24-26 January 2015, Wadau wa
Muziki wa dansi chini ya uratibu wa admin wa BONGO DANSI Deo Mutta Mwanatanga
wafanikisha harambee na zoezi la kumrudisha Dar-es-Salaam mwanamuziki Banza
Stone aliyekuwa amekwama mjini Tunduma huku akiwa anaumwa baada ya matatizo
yaliyoitokea bendi ya Rungwe aliyoenda nayo huko.
•Tarehe 24-Jan-2015 (Jumamosi), tamasha linaloitwa TIGO
KIBOKO YAO Concert lafanyika Leaders Club. Bendi za muziki wa dansi
zilizoshiriki ni Msondo Ngoma, Mlimani Park Orchestra, Christian Bella &
Malaika Music Band, Yamoto Band. Kila bendi ilipiga kwa dakika 45.
•Tarehe 25-Jan-2015 (Jumapili), tamasha la miaka 10 ya
CDS lafanyika TCC Chang’ombe na kushirikisha bendi za muziki wa dansi za Msondo
Ngoma, Mapacha Watatu, Malaika Music Band na FM Academia. Kuna uwezekano
tamasha hili likawa linafanyika kila mwaka.
•Tarehe 30-Jan-2015, Ali Choki na Mama Asha Baraka
wapatanishwa rasmi chini ya usuluhishi uliofanywa na Global Publisher.
•Tarehe 07-Feb-2015 (Jumamosi), tukio la “Miaka 16 ya
Luizer Mbutu” ndani ya Twanga Pepeta lafanyika Mango Garden.
•Tarehe 28-Mar-2015 (Jumamosi), wafanyika mpambano kati
ya FM Academia na Twanga Pepeta katika ukumbi wa Escape One.
•Tarehe 08-Apr-2015, Ally Choki na Super Nyamwela
watangazwa rasmi kujiunga (kurejea) Twanga.
•Tarehe 18-Apr-2015 (Jumamosi), Christian Bella afanya
tukio la “Usiku wa Masauti” ndani ya ukumbi wa Escape One. Christian Bella atumia
tukio hilo kutambulisha/kuzindua audio na video ya wimbo wake mpya wa
“Nashindwa”.
•Tarehe 25-Apr-2015 (Jumamosi), show ya kwanza ya Ally
Choki na Super Nyamwela baada ya kurejea Twanga Pepeta yafanyika Mango Garden.
•Tarehe 25-Apr-2015 (Jumamosi), kundi la Les Wanyika
kutoka Kenya latumbuiza katika kiwanja cha Escape One.
•Tarehe 26-Apr-2015, Bendi ya Cuban Marimba watunukiwa
nishani ya Muungano kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya
Mrisho Kikwete katika sherehe zilizofanyika katika viwanja vya ikulu.
Waliopokea nishani kwa niaba ya bendi ni Waziri Nyange (mpiga solo) na Mzee
Juma Sangura (mpiga bass).
•Tarehe 08-May-2015 (Ijumaa), Mashujaa Group wazindua
ukumbi wao wa Mashujaa Lounge ambao zamani ulikuwa unaitwa Business Park uliopo
maeneo ya Victoria, Dar-es-Salaam. Katika tukio hilo, Mashujaa Band imetumia
nafasi hiyo pia kutambulisha wanamuziki wawili wapya Roggart Hegga Katapila na
Dady Dipirone “Rais wa Masauti ya Chini”. Pia Mashujaa Band walitambulisha
nyimbo 2 mpya. Ikumbukwe pia kuwa Mashujaa Group mwaka huu wamefanikiwa
kuanzisha radio ya Mashujaa FM mkoani Lindi.
•Tarehe 24-Jun-2015, mwanamuziki Ramadhan Masanja aka
“Banza Stone” alizushiwa kifo baada ya kuumwa muda mrefu. Hii ni moja ya mara
nyingi sana mwanamuziki huyo kuzushiwa kifo.
•Tarehe 18-Jul-2015 (Jumamosi), mpambano wa
Msondo na Sikinde wafanyika siku ya Idd Mosi (Eid al Fitr) katika ukumbi wa TCC
Chang’ombe kwa kuandaliwa na Fred Ogot na kampuni yake ya Bob Entertainment.
No comments:
Post a Comment