Tuesday, December 8, 2015

PANAFRICAN ENERGY YATOA YAFADHILI UJENZI WA WODI YA ‘MAMA NGONJEA’ HOSPITALI YA WILAYA KINYONGA KILWA KIVINJE NA KUKARABATI WODI ZA UZAZI NA CHUMBA MAALUM CHA UANGALIZI WA AKINA MAMA

Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni ya PanAfrican Energy Andrew  Kangashaki  (kushoto ) na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa Twalib Mbasha wakikabidhiana mkataba wa miradi  ya ujenzi wa nyumba ya mama ngojea  katika hospital ya Kinyonga  na ukarabati wa wodi  ya uzazi  mara baada ya kumaliza kusaini mikataba hiyo katika hafla fupi iliyofanyika jana Kilwa Kivinje.
Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni ya PanAfrican Energy Andrew  Kangashaki(wa tatu kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa Twalib Mbasha (wa tatu kulia) wakisaini makubaliano ya miradi miwili ya ujenzi wa mama ngojea ‘maternity waiting home’ yaani nyumba maalum kwa kina mama wajawazito watakaokua wakisubiri kujifungua itakayojengwa katika hospitali ya Kinyonga – Kilwa Kivinje na kukarabati wodi ya uzazi na chumba maalum cha uangalizi wa akina mama mara tu baada ya kujifungua katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko.
Huku wakishuhudiwa na Mwanasheria wa Wilaya Mh. Godfrey Makary (wapili kutoka kulia), Mkuu wa Wilaya ya Kilwa Juma Abdalah Njwayo(wa pili kushoto), Mbunge wa jimbo la Kilwa Kaskazini kupitia chama cha CUF Mh. Vedasto Edgar Ngombale(wakwanza kushoto) pamoja na Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia chama cha CUF Selemani Bungawa a.k.a Bwege(wakwanza kulia).

Mbunge wa Kilwa Kusini kupitia chama cha CUF Selemani Bungawa a.k.a Bwege(wapili kulia) akitoa neno la shukrani kwa Kampuni ya PanAfrican Energy kwa niaba ya wananchi wa Kilwa Kusini mara baada ya makabidhiano ya mkataba wa miradi itakayowanufaisha wananchi wa kilwa.
Wafadhili wa mradi wa ujenzi wa wodi ya wazazi Kampuni ya PanAfrican Energy pamoja wakiwaonesha wanahabari chumba cha uzazi katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko ambacho kipo katika mradi uliosainiwa kati ya wilaya ya Kilwa na kampuni hiyo. Hii ni katika kuunga jitihada za serikali za kuboresha huduma za afya.
Hali halisi ya mazingira ya wodi ya wagonjwa katika kituo cha afya cha Kilwa Masoko, hii ni wodi ya wanaume. Kiyuo hichi cha afya  kilijengwa mwaka 1952 enzi za ukoloni mpaka sasa hakijawahi kukarabatiwa.
Wakisaini makubaliano ya miradi ya ujenzi wa mama ngojea na ukarabati wa chumba cha uzazi na wodi maalum ya uangalizi wa kina mama mara tu baada ya kujifungua wilayani Kilwa ni Meneja Uwajibikaji kwa jamii kutoka Kampuni ya PanAfrican Energy Andrew Kangashaki(wa pili kushoto) pamoja na Mkurugenzi wa Wilaya ya Kilwa Twalib Mbasha (wa pili kulia) wanaowashuhudiwa ni Mwanasheria wa Wilaya ya Kilwa Mh. Godfrey Makary ( kulia), Mkuu wa Wilaya ya hiyo Juma Abdalah Njwayo (kushoto) jana katika hafla fupi iliyofanyika jana katika hospitali ya Kinyonga Kilwa Kivinje.

<!--[if gte mso 9]>

No comments: