Sunday, October 22, 2017

NIHF ARUSHA YAANZA KUTOA ELIMU YA BIMA YA AFYA MTAA KWA MTAA


 Afisa Metekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Arusha,Miraji Kisile akiwahamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo ili kuweza kunufaika na huduma zinazotolewa ikiwemo za matibabu
  Afisa Metekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Arusha,Miraji Kisile akiwahamasisha wananchi kujiunga na mfuko huo ili kuweza kunufaika na huduma
zinazotolewa ikiwemo za matibabu
 ELIMU ikiendelea kwenye moja ya masoko Jijini Arusha kuhusu umuhimu wa wajasiriamali kujiunga na mfuko huo ili kuweza kunufaika na huduma mbalimbali ikiwemo za matibabu
MFUKO wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Arusha (NHIF) umeanza kutoa elimu ya bima ya afya mtaa kwa mtaa kwa wakazi wa mkoa huo ili waweze kujiunga nao ili kuweza kunufaika na huduma mbalimbali ikiwemo za matibabu.
 
Hayo yalibainishwa na Afisa Matekelezo wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya Mkoani Arusha ,Miraji Kisile  ambapo alisema lengo ni kuhamasisha wazazi na walezi kuwaandikisha watoto wao na mpango wa toto afya kadi kwa chini ya miaka 18.

Alisema mfuko huo umeamua kushiriki katika zoezi hilo kikamilifu kwa kupita katika masoko na magulio ambayo asilimia kubwa ya wananchi wamekuwa wakipatikana huko.

Aidha alisema sambamba na hilo lakini pia uongozi wa mfuko huo wamedhamiria kuwahamasisha wajasiriamali mbalimbali kujiunga na mfuko huo kupitia mpango wa kikoa ili kulinda mitaji yao kwa kuwa na uhakika wa huduma za afya na matibabu kupitia NHIF kwa gharama nafuu.

“Zoezi hilo limeanza Octoba 18 mwaka huu na litafanyika kikamilifu kwa muda wa miezi miwili lengo ni kuwafikia wakazi wengi wa mkoa wa Arusha na viunga vyake “Alisema.

Alisema kwa sasa mfuko huo unatoa kipaumbele kusajili watoto kupitia mpango wa Toto Afya Kadi kwa gharama za kitanzania 50400 kwa mwaka  ambapo ataweza kuhudumiwa kwa vituo 7000 vilivyosajiliwa na bima ya afya vikiwemo hospitali zote za serikali,Hospitali zinazomilikiwa na Madhehebu ya dini,Hospitali za watu binafsi, maduka ya dawa pamoja na vituo maalumu vya uchunguzi.

Zoezi hilo limefanyika na kutarajiwa kuendelea kufanyika kwenye maeneo mbalimbali ikiwemo soko la Tengeru,Soko la Ngaramtoni,Soko Kuu,Soko la Kilombero,Soko la Mbauda,Soko la Namanga, Mnadani Monduli,Loliondo,Digodigo Ngorongoro na Waso Ngorongoro.
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments: