Thursday, November 16, 2017

WAANDISHI WA HABARI MKOANI TANGA WAFANYA ZIARA YA MAFUNZO HIFADHI YA MAMLAKA YA NGORONGORO

Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali mkoani Tanga wakiingia kwenye hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro tayari kuanza ziara ya siku kumi ya mafunzo
 Waandishi wa Habari Mkoani Tanga wakiwa kwenye hifadhi ya mamlaka ya Ngorongoro mkoani Arusha wakati wa ziara ya siku tano kwa ajili ya ziara ya mafunzo kutembelea vivutio vya utalii kulia ni Mwandishi wa Shirika la Utangazaji la TBC
,Bertha Mwambela ambaye ni mratibu wa ziara hiyo kushoto ni Mbonea Herman wa Kituo cha Star TV kulia ni 
 Mratibu wa ziara ya waandishi wa habari mkoani Tanga waliotembelea hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro,Bertha Mwambele kutoka Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) wakiingia ndani ya mamlaka hiyo kulia ni Sussan Uhinga mwandishi wa gazeti la Mtanzania mkoan Tanga  kushoto ni Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka
 Mratibu wa ziara ya Waandishi wa Habari mkoani Tanga ambaye ni Mwandishi wa Shirika la Utangazaji la TBC Bertha Mwambele akiwa kwenye picha eneo la Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro mara baada ya kuwasili kwa ajili ya mafunzo ya siku kumi ikiwemo kutembelea hifadhi hiyo.
Waandishi wa habari wakipiga picha kwenye bango la mamlaka hiyo kabla ya kuanza ziara ya siku kumi kutoka kulia ni Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka,Lilian Lucas wa Mwananchi,Nestory Ngwega wa gazeti la Daily News,Bertha Mwambela wa TBC,Alex wa TATV,Pamela Chaula wa Tanga One Blog
Afisa Uhusiano wa Mamlaka ya Ngorongoro,Walter Mairo akitoa ufafanuzi kwa waandishi wa habari kabla ya kuanza ziara ya kutembelea maeneo mbalimbali ya hifadhi wakati wa ziara yao ya siku kumi
 Waandishi wa habari wakipata kifungua kinywa kabla ya kuanza ziara ya mafunzo ya siku kumi
 Mwandishi wa Kituo cha Tanga TV cha Jijini Tanga,Abraham Alex akiwa kwenye eneo la mchanga ambalo umekuwa ukihama mara kwa mara
 Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kutembelea eneo la mchanga ambalo limekuwa likihama mara kwa mara
 Waandishi wa habari,Mbaruku Yusuph wa gazeti la Tanzania Daima na Mbonea Hermani wa Star TV wakiangalia eneo la ambalo limegunduliwa fuvu la binadamu wa kwanza wakati wa ziara hiyo
 Jumba la Makumbusho ya Mambo ya Kale ambalo lipo eneo la Mamlaka ya Ngorongoro Mkoani Arusha
Afisa Uhusiano wa Mamlaka hiyo,Samweli Nsyuka kulia akitoa maelekezo kwa waandishi wa habari mara baada ya kutembelea Jumba hilo la Makumbusho 
Habari kwa Hisani ya Blog ya Kijamii ya Tanga Raha

No comments: