Tuesday, May 13, 2008

MAMA YAKE LLOYD BANKS ANUSURIKA AJALINI.

Ukisikia utu uzima kazi ndio hivi bwana. Wakati rapa mahiri wa kundi la maarufu la rapa za kigumu, G-Unit, Lloyd Banks akiwa katika ziara nzito iliyomleta mpaka bongo na kundi hilo, imeripotiwa kuwa mama yake alipatwa na bonge la ajali wikendi mbili zilizopita.

Kwa mujibu wa mtandao Media take Out wa mambo ya masupastaa, umemnukuu msomaji wake mmoja akisema kuwa gari alilokuwa akiendesha mama yake Lloyd lilipata ajali iliyopelekea kuumiza kichwa chake na gari kuharibika vibaya.

“Kwa sasa amelazwa hospitali na anaendelea vizuri ingawa pia alipatwa na mpasuko sehemu ya kifuani” ameeleza msomaji huyo alipokuwa akiutaarifu mtandao huo.

Banks ni miongoni mwa marapa wakali watatu wanaounda kundi la G-Unit linaloongozwa na 50 Cent na hivi karibuni wote walikuwa ndani ya Bongo.

Sasa hatujui kama jamaa aliamua kukatisha ziara yake akamuone mgonjwa ama vipi. Si unajua tena, nani kama mama.

No comments: