Sunday, October 16, 2011

Picha za maonyesho mpanda

Waziri Mkuu Mizengo Pinda akiangalia moderm ya intaenti ya kampuni ya Vodacom wakati Meneja Mawasiliano wa kampuni hiyo Salum Mwalim akimpatia maelezo ya moderm hizo,wakati Waziri Mkuu alipotembelea banda la Vodacom katika maonesho ya bidhaa na huduma pembezoni mwa mkutano wa wadau wa uwekezaji eneo la ziwa Tanganyika unaofanyika Mjini Mpanda. Mkutano huo utafunguliwa kesho 17 Oktoba, 2011 na Rais Dk. Jakaya Kikwete.
Meneja Mawasiliano wa kampuni ya Vodacom Salum Mwalim akimsikiliza kwa umakini kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa SACP Isunto Mantage wakati wawili hao walipokutana katika banda la Vodacom katika maonesho ya wadau watakaoshiriki mkutano wa uwekezaji katika ukanda wa ziwa Tanganyika mjini Mpanda. Mkutano huo unafanyika kesho 17 Oktoba, 2011 Mjini Mpanda, na utafunguliwa na Rais Jakaya Kikwete. Kampuni ya Vodacom imefadhili chakula cha mchana na cha usiku kwa wajumbe zaidi ya mia nne watakaohudhuria mkutano huo.

No comments: