Monday, May 25, 2015

KAMANDA WA UCCM ATOA MSAADA WA KITI CHA WALEMAVU

Mama mzazi wa mtoto Felista Shirima akieleza kwa uchungu namna ambavyo mtoto wake alivyopata ulemavu wa kudumu.
Babu wa mtoto Felista,Anold Shirima akiwasilisha ombi kwa jamii la kupata wakili kwa ajili ya usikilizwaji upya wa kesi dhidi ya watu waliosababisha ajali ya mtoto huyo.
Naibu Kamanda wa jumuiya ya vijana wa CCM(UVCCM) Innocent Melleck akizungumza mara baada ya kutembelea familia ya mtoto Felista wa kijiji cha Rauya Marangu wilaya ya Moshi vijijini.
Baadhi ya atoto na ndugu wengine waliofika nyumbani kwa mtoto huyo.
Melleck alikabidhi kiti cha walemavu cha magurudumu kwa mtoto Felista kwa ajili ya kusaidia wakati wa kwenda shuleni.
Mellecky pia alikabidhi Pempers kwa ajili ya mtoto huyo.
Familia na wanandugu wngine wa mtoto Felista wakiwa katika picha ya pamoja na Naibu Kamanda wa UVCCM wilaya ya Moshi vijijini ,Innocent Melleck mara baada ya kukabidhi msaada wa baiskeli .
Mama mzazi wa mtoto Felsita akitabasamu akiwa amembeba mtoto wake mara baada ya kupokea msaada wa baiskeli,Pempers na Chakula kwa ajili ya mtoto wake,hata hivyo mamahuyo bado anahitaji msaadawa kiasi sha sh Mil,1.5 kwa ajili ya malipo ya matibabu ya mtoto huyo anayodaiwa katika hosptali ya rufaa ya KCMC.


Na Dixon Busagaga wa Globu ya jamii ,kanda ya kaskazini.

No comments: