Monday, October 5, 2015

MAMA SAMIA AFUNIKA TABORA, MAELFU WAFURIKA MIKUTANO YAKE YA KAMPENI

 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akihutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kampeni uliofayika leo kwenye viwanja vya shule ya Sekondari Uyui katika jimbo la Tabora mjini.
 Maelfu ya wananchi wakimshangilia mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari ya Uyui, jimbo la Tabora mjini mkoani Tabora

 Aliyekuwa mgombea Ubunge jimbo la Nkenge lakini akashindwa katika kura za maoni, Mama Asupta Mshama, akihutubia maelfu ya wananchi katika viwanja vya Shule ya Sekondari Uyui, Jimbo la Tabora mjini mkoani Tabora
Mbunge wa jimbo la Tabora Mjini Emmanuel Mwakasaka akiomba kura katika mkutano wa kampeni wa Mama Samia, uliofanyika kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Uyui, katika jimbo hilo mkoani Tabora leo
 Wasanii wa Bongo Movie, wakichangamsha wananchi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari ya Uyui jimbo la Tabora mjini mkoani Tabora leo
 Kiongozi wa wanakampeni wa Mama Ongea na Mwanao, wanaoundwa na kundi la Wasanii wa Bongo Movie, Steven Mengere maarufu kwa jina la Stev Nyerere, akimuombea kura Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli katika mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Uyui, katikajimbo la Tabora mjini mkoani Tabora. Kulia ni Msanii mwenzake wa Bongo Movie Wema Sepetu
 Msanii maarfu kwa jina la Sina Nyonga, akionyesha umahiri wake wa kucheza sarakasi, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofayika leo kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Uyui jimbo la Tabora mjini
 Mwanamuziki wa Bongo Fleva, Stara Thomas akimuombea kura Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari ya Uyui jimbo la Tabora mjini mkoani Tabora.
 Baadhi ya wasanii wakimuaga Mama Samia baada ya kumuombea kura Dk. Magufuli, katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo kwenye Viwanja vya Shule ya Sekondari Uyui mkoani Tabora.
Vijana ambao ni Mashabiki wa CCM wakionyesha furaha zao wakati wa mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari Uyui jimbo la Tabora mjini mkoani Tabora
 Mkuu wa wilaya ya Nzega anayekaimu pia wilaya ya Igunga, Jacqueline Liana akiwa kwenye mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo la Manonga, Igunga mkoani Tabora.
 Mgombea Ubunge jimbo la Igunga, Dalally Kafumu, akijadili jambo la Mgombea Ubunge jimbo la Manonga Seif Gulamali, katika mkutano wa Kamapeni uliofanyika leo katika jimbo la Manonga, wilayani Igunga mkoani Tabora
 Wananchi wakimshangilia mgombea mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Manonga, wilayani Igunga mkoani Tabora
 Mgombea Ubunge jimbo la Manonga, wilayani Igunga mkoani Tabora, Seif Gulamali akisalimia wananchi baada ya kunadiwa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo hilo
 Wagombea Udiwani katika jimbo la Manonga wakisalimia wananchi wakati wa mkutano wa Kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo hilo mkoani Tabora
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akimkabidhi kitabu cha  ilani ya uchaguzi ya CCM, Mgombea Ubunge jimbo la Manonga, Seif Gulamali wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo hilo
 Mgombea Ubunge jimbo la Igunga, Dalally Kafumu akionyesha kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya CCM, baada ya kukabidhiwa na Mama Samia katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo la Manonga wilayani Igunga mkoani Tabora
 Mjumbe wa Kamati ya Kampeni za CCM, Anela Kiziga ambaye ni Mbunge wa Afrika Mashariki, akiteta jambo la Mgombea bunge jimbo la Igunga, Dalaly Kafumu katika mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo la manonga wilayani Igunga mkoani tabora
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akiwasili kuhutubia mkutano wa kampeni katika jimbo la Nzega Vijijini, uliofanyika leo Ndala mkoani Tabora
  Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan akisalimia baadhi ya viongozi wa CCM, baada ya kuwasili kuhutubia mkutano wa kampeni katika jimbo la Nzega Vijijini, uliofanyika leo Ndala mkoani Tabora
 Mbunge wa jimbo la Nzega Vijijini, Dk. Hamis Kigwangala akiomba kura katika mkutano wa Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia uliofanyika leo katika jimbo hilo mkoani Tabora
 Aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Vijana wa Chadema (BAVICHA) Wilaya ya Igunga, Anuar Kashaga, akiichana Chadema, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mama Samia ukiofanyika leo katika jimbo la Nzega Vijijini mkoani Tabora
 Wananchi wakiwa wamefurika katika mkutano wa Kampeni uliofanywa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama samia Suluhu Hassan katika jimbo la Nzega Vijijini mkoani Tabora
Baadhi ya vijana wakiwa kwenye mapaa na nyumba inayojengwa, wakati wa mkutano wa kampeni wa Mama Saamia uliofanyika leo katika jimbo la Nzega Vijijini mkoani Tabora
 Umati wa wananchi ulimsikiliza Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika Ndala katika jimbo la Nzega Vijijini mkoani Tabora leo
 Mgombea Ubunge jimbo la Nzega Vijijini, Dk. Hamais Kigwangala akisalilimia wananchi baada y kunadiwa na Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia Suluhu Hassan katika mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo hilo leo
 Mgombea Ubunge jimbo la Nzega, Hussein Bashe, akihutubia mkutano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika katika jimbo la Nzega Vijijini mkoani Tabora leo
 Baadhi ya wananchi wakiwa wamesimama kwenye meza za biashara zao, wakati wa mkuano wa kampeni wa Mama Samia uliofanyika leo kwenye viwanja vya Soko la Sikonge, jimbo la Sikongea mkoani Tabora
 Mgombea Ubunge jimbo la Sikonge Mussa Ntimizi akiomba kura katika mkutano wa kampeni uliofanyika leo katika jimbo hilo
 Mgombea Mwenza wa Urais kwa tiketi ya CCM, Mama Samia suluhu Hassan akijadili jambo na Mgombea Ubunge jimbo la  Sikonge mkoani Tabora, Mussa Ntimizi wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika katika jimbo hilo mkoani Tabora leo
 Shabiki wa CCM akiwa na mabango ya Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM, Dk. John Magufuli na Mgombea Mwenza Mama Suluhu Hassan wakati wa mkutano wa kampeni uliofanyika leo jimbo la Sikonge mkoani Tabora. PICHA ZOTE NA BASHIR NKOROMO

No comments: