Friday, January 16, 2009

Janga la mafuta limemchelewesha mwanangu shule

Miongoni mwa Watanzania waliathirika na ishu ya mafuta ambayo yaliadimika ghafla tangu mwanzoni mwa wiki hii ni mwana Hip Hop Selemani Msindi ‘Afande Sele’ kutoka pande za Morogoro.

Akipiga stori na safu hii juzi, msanii huyo ambaye bado anatambulika kama Mfalme wa Hip Hop, alisema kwamba athari kubwa zaidi aliyoipata ni kushindwa kumuwahisha shuleni Morogoro mwanaye Tunda baada ya kuwa Dar es Salaam kimatembezi kwa siku kadhaa.

“Yaani kaka huwezi kuamini, nimeanza kuhangaikia mafuta tangu jana (Jumanne) asubuhi, ili nimuwahishe Tunda shule Morogoro nikafanikiwa kuyapata saa 5 usiku kwenye kituo cha Big Bon, Kariakoo, hapa unavyoniona ndiyo tunasafiri kuelekea Moro na familia yangu.” alisema Afande.
************

1 comment:

Anonymous said...

mafuta lita tano yatakufikisha moro afande au ukifika mbezi utaongeza lita tano nyingine.