Saturday, March 28, 2009

ZIZZOU YADHAMINI MR. HANDSOME




Baadhi ya washiriki wa shindano la kumtafuta kijana mtanashati wa jiji la Dar es salaam (Mr. Dar handsome) wakiwa katika Salon na duka la Zizzou mchana wa leo katika maandalizi yao ya mwisho kwa upande wa mavazi na kujiweka soap soap. Shindano linafanyika usiku huu, New Africa Hotel na Zizzou Fashions ni mdhamini wa shindano hilo.

Friday, March 27, 2009

IJUMAA SHOWBIZ!

Ali Kiba
Dully Sykes
Dar es Salaam Hands Up
Shindano lako la kijanja zaidi, ‘Dar es Salaam Hands Up’ (Dar es Salaam Mikono Juu) limeingia kunako hatua nyingine, baada ya wiki iliyopita kuwapata wakali wa Bongo Flava watakaoiwakilisha vyema Wilaya ya Kinondoni, leo tunadondoka na wasanii kutoka pande za Ilala waliyotajwa na wasomaji kuiwakilisha wilaya yao.

Wasanii hao kutoka Wilayani Ilala ni Dully Sykes, Blue, Ali Kibba, Chidi Benz (La Familia), Soggy Dog, Suma G, Zay B na Akili The Brain. Kabla sijaendelea mbele zaidi nakukumbusha kwamba, shindano hili linazihusu Wilaya tatu za Dar es Salaam, Kinondoni, Ilala na Temeke ambapo wewe msomaji na mpenzi wa burudani hii utatuambia ni ipi ina wasanii wakali.

Baada ya kuwapata wasanii hao kutoka Ilala, sasa tunaelekeza macho yetu pande za Temeke ambapo wewe msomaji na mpenzi wa mpambano huu unatakiwa utuambie ni msanii gani anastahili kuiwakilisha wilaya hiyo.

Hivi sasa unatakiwa ututumie ujumbe mfupi ukimtaja msanii wa Temeke ambaye unadhani anastahili kuiwakilisha wilaya hiyo kunako shindano hili, si msanii ambaye unamuona hapa pichani. Baada ya kufanya hivyo tuma kwenda simu namba 0787-110 173. Mwisho wa kupokea kura zenu ni siku ya Jumanne mchana.
*************************************
Blue
Bushoke: Sasa ni zamu ya Bukoba
Zikiwa zimesalia siku kadhaa kabla ya kuifikia Sikukuu kubwa ya Pasaka, msanii Rutta Maximilian Bushoke anatarajia kujirusha na wakazi wa Bukoba, Mkoani Kagera katika kuadhimisha siku hiyo.

Ndani ya ShowBiz msanii huyo ambaye bado ni memba wa kundi la Makole Hexagon lenye maskani yake pande za Dodoma, alisema kwamba baada ya kuzunguka sehemu mbalimbali nchini akiitambulisha albamu yake mpya, ‘Dunia Njia’ sasa ni zamu ya Bukoba.

“Nikiwa na baadhi ya wasanii wengine wa Bongo Flava, kama Ngwea, Blue, Maunda Zorro na wengine kibao tutapiga shoo ya kwanza ndani ya ukumbi wa Linas Club, siku itakayofuata tutajitupa ndani ya Uwanja wa Kaitaba na kuendelea na uzinduzi huo,” alisema Bushoke.

Aidha, mchizi aliweka wazi kwamba, viingilio kunako shoo hiyo vitakuwa ni shilingi elfu kumi (VIP) na elfu tano kawaida, huku uwanjani ikiwa ni shilingi elfu moja kwa kila mtu.
******* **************
Miss EA 2008 kuanzia A-Town
Shindano la kumtafuta mrembo wa Afrika Mashariki (Miss East Africa) ambalo mwaka jana lilimalizika kwa binti kutoka Burundi, Claudia Noyimana kuibuka na ushindi, mwaka huu linaanzia pande za Arusha ambapo litawakutanisha zaidi ya warembo 20.

Akipiga stori na ShowBiz, mratibu wa mpambano huo, Nicodemus Ngogo wa Kampuni ya Tanzania Full Moon Entertainment alisema kwamba tayari zoezi la kuchukua fomu kwa washiriki limeshaanza, linaendelea hadi Aprili 15, mwaka huu kisha warembo ishirini na tano watakaopatikana wataingia kambini kabla ya kukutana kunako jukwaa moja kwa ajili ya kumpata mshindi kutoka pande hizo za Kaskazini.

“Fomu zinaendelea kutolewa katika sehemu mbalimbali Arusha na Dar es Salaam, baada ya hapo warembo wataingia kambini kwa muda wa wiki mbili kabla ya kupambana jukwani ambapo mshindi ataondoka na gari jipya aina ya Toyo Nadia, huku mshindi wa pili na wa tatu wakijipatia pesa taslim ambazo tutazitaja hivi karibuni,” alisema Ngogo. Naye Mwenyekiti wa Kampuni hiyo, Omari Mawamba alisema kila kitu kuhusu shindano hilo kinaendelea vizuri.
**************************************************

Thursday, March 26, 2009

KUTANA NA MWANDISHI CHIPUKIZI!!!!


Kwenu wapenzi wa fasihi,
Kama ilivyo ada, hapa Mkahawani Soma kila Ijumaa ya mwisho wa mwezi ni siku ya kukutana na mwandishi. Ijumaa hii ya tarehe 27/03/2009 tutakutana ana kwa ana na mwandishi chipukizi Sandra Mushi mwandishi wa The Rhythm of my Rhyme amabacho kinapatikana hapa kwenye duka la vitabu Soma pamoja na hadithi fupi nyingi za kuvutia ambazo amechapishwa kwenye blog yake
www.sandrasden.com na www.sarahsoulfood.wordpress.com hadithi moja imechapishwa kwenye toleo la kwanza la jarida la fasihi Soma.

Tutapata fursa ya kuhojiana naye, kujadili mashairi na hadithi zake, na pia tutasoma baadhi ya hadithi zake na kughani baadhi ya mashairi yake.

************************************************

Dear literati,
Welcome again at Soma Book Café on Friday Evening 27th March/2009 whereby we will meet face to face with a Book Writer Sandra Mushi the author of Rhythm of my Rhyme a newly released anthology that has gained popularity among people of varied social backgrounds. The book is available at Soma Bookshop. Sandra has also authored several short stories available in her blog www.authorsden.com and www.sarahsoulfood.wordpress.com and one of them is serialized on the first issue of Soma literary magazine.

We will chart with Sandra and talk about her writings, plus we shall recite some of her poems and read from some of her stories. You will also be able to get her to autograph your copy of her book.

Welcome and Karibuni Wote!

JE, UMEWAHI KUFANYA ENEMA?- 2

WIKI ILIYOPITA TULIANZA MAKALA HAYA KWA KUANGALIA SUALA LA UFANYAJI WA ENEMA KWA AJILI YA KUSAFISHA TUMBO, ZOEZI AMBALO HUSAIDIA KUONDOA SUMU MWILINI NA HIVYO KUEPUSHA MWILI NA MARADHI, ENDELEA...
UTAJIJUAJE KAMA UTUMBO WAKO NI MCHAFU?

Ni rahisi sana kujitambua kwamba utumbo wako ni mchafu, lakini kwa bahati mbaya watu wengi huwa hawazitambui dalili hizo na wanaozitambua huzipuuzia. Dalili ya kwanza ni harufu mbaya kutoka mdomoni, licha ya kupiga mswaki kila siku. Harufu mbaya unayoisikia mdomoni haitoki mdomoni, bali hutoka tumboni.

Dalili nyingine ni harufu mbaya ‘unapopumua’, wenye matumbo masafi huwezi kusikia pumzi zao zikitoa harufu mbaya. Dalili nyingine ni kukosa kwa choo kwa siku kadhaa. Katika hali ya kawaida, binadamu anatakiwa kupata choo angalau mara moja kwa siku kama siyo mara tatu. Unapokosa choo kwa siku nzima ili hali unakula mara tatu au mbili kwa siku, tena ‘plate’ nzima, ujue una matatizo.

Lakini dalili nyingine na ambayo imefanyiwa utafiti wa kisayansi, inapatikana usoni mwa kila mtu! Uso wa binadamu unaelezea viungo vyote vilivyomo tumboni kama mchoro wa makala haya unavyoonesha. Kila kiungo kilichomo tumboni, unaweza kujua hali yake kwa kuangalia kiungo kinachofanana nacho usoni.

Kuanzia sasa, anza kujiangalia pamoja na afya yako kwa mtizamo mwingine. Jiangalie ndani ya mwili wako kupitia sura yako, utaweza kujijua ulivyo tumboni mwako kwa kuangalia uso wako tu, kwani kila kitu kinachoendelea tumboni, kinaonekana usoni mwako:

Katika mchoro wa kwanza, viungo vyote vya tumboni (kama mchoro wa pili unavyoonesha mfumo wa tumbo) vimeoneshwa usoni. Napenda kuzungumzia zaidi sehemu ya utumbo mkubwa (Large Intestine) ambao ndiyo mada yetu ya leo na ambao ndiyo huweza kusafishwa kwa kutumia Enema.

Mtu ambaye utumbo wake mkubwa umejaa uchafu, utamjua kwa kumuangalia chini ya macho (kama mchoro unavyoonesha), chini ya macho ya watu hawa huwa yamevimba, na kuvimba huko huwa kunamaanisha utumbo wake umejaa choo au ana matatizo ya figo.

Kama tulivyosema hapo awali, kujaa choo katika utumbo mkubwa ndiyo mwanzo wa matatizo mengine ya kiafya, mifumo mingine ya mwili hushindwa kufanya kazi zake vizuri na hivyo kusababisha matatizo kama shinikizo la damu, saratani, kisukari, matatizo ya figo na kibofu cha mkojo, magonjwa ya viungo na maradhi mengine hata usiyoyajua.

Baada ya kuanza na utangulizi huu, nafikiri sasa umeelewa Enema ina umuhimu gani katika afya zetu. Kama kweli tunataka kuishi maisha yaliyo huru dhidi ya maradhi, hatuna budi kuifanya enema. Wiki ijayo tutaelezea ufanyaji wa enema hatua kwa hatua, kwani ni rahisi na kila mtu anapaswa kufanya japo mara moja kwa mwaka ili kuondoa na kujikinga na maradhi.
Itaendelea wiki ijayo..

Tuesday, March 24, 2009

TRUE LOVE!

The girl in the picture is Katie Kirkpatrick, she is 21. Next to her, her fiancé, Nick, 23.
The picture was taken shortly before their wedding ceremony, held on January 11, 2005 in the US .
Katie has terminal cancer and spend hours a day receiving medication. In the picture, Nick is waiting for her on one of the many sessions of quimo to end.
In spite of all the pain, organ failures, and morphine shots, Katie is going along with her wedding and took care
of every detail. The dress had to be adjusted a few times due to her constant weight loss


cid:4.3701829053@web52511.mail.re2.yahoo.com
Katie, in her wheelchair with the oxygen tube , listening a song from her husband and friends
At the reception, katie had to take a few rests.The pain do not let her to be standing up for long periods

Katie died five days after her wedding day. Watching a women so ill and weak getting married and with a smile on her face makes us think..... Happiness is reachable, no matter how long it last. We should stop making our lives complicated.

THE MESSAGE TO LEARN
* Life is short
*Break the rules
*Forgive quickly
*Kiss passionately, love truly
*Laugh constantly
*And never stop smiling
*No matter how strange life is
*Life is not always the party we expected to be, but as long as we are here, we should smile and be grateful.

Monday, March 23, 2009

WIKIENDA SHOWBIZ!

Bushoke kujiachia Bukoba Pasaka
Akiwa bado anaendelea kupiga kitabu ndani ya Chuo cha Sanaa Bagamoyo, Mkoani Pwani, msanii Ruta Maxmiliani Bushoke ‘Bushoke’ anatarajia kuendelea na ziara ya utambulisho wa albamu yake, ‘Dunia njia’ pande za Bukoba, siku ya Sikukuu ya Pasaka.

Akipiga stori na safu hii, Bushoke alisema kwamba akiwa Bukoba, Mkoani Kagera ataangusha shoo mbili mfululizo akianzia ndani ya Ukumbi wa Linas Pub siku ya Pasaka ambapo kiingilio kitakuwa ni shilingi 10, 000 (VIP) na 5, 000 kawaida, ikifuatiwa na ndani ya Uwanja wa Kaitaba siku itakayofuata kiingilio kikiwa ni buku moja kwa kila kichwa.

“Katika msafara huo nitakuwa na baadhi ya wasanii ambao nilizunguka nao mwanzo katika uzinduzi wa albamu hiyo, ambao ni Ngwea, Blue, Maunda Zorro na wengine kibao ambao nitawataja hivi karibuni. Watu wa Bukoba na sehemu za jirani wajitokeze kwa wiingi siku hiyo ili tule sikukuu pamoja,” alisema Bushoke.
**********

Hemedi apata dili Mr. HB
Baada ya ‘kuhaso’ huku na kule akitafuta kutoka, msanii Hemedi Suleiman aliyepitia kunako shindano la ‘Tusker Project Fame’ na kuambulia za uso, sasa ameanza kula matunda ya jasho lake nikimaanisha kuwa, ngoma yake mpya ‘Unachotaka ni mapenzi’ imempa dili la kupiga shoo kunako shindano la kumtafuta Mr. Handsome litakalofanyika Machi 28, mwaka huu, Imelda Mtema anajiachia nayo.

Mratibu wa mpambano huo, Methuselah Magese alisema na safu hii kwamba, Hemedi ni miongoni mwa wasanii chache waliopata bahati ya kusimama katika jukwaa la mpambano huo ambao utapigwa katika Hoteli ya New Africa, Dar es Salaam.

“Katika shindano hilo ambalo litawakutanisha vijana watanashati zaidi ya kumi majaji watakuwa ni Nasreen Kareem, Big Brother 2007, Richard Bezuedenhout na Steven Kanumba,” alisema Magese.
***********

Kikosi kutambulisha 3 na studio yao mpya
Kutoka pande za Kinondoni, Dar es Salaam, kundi la muziki wa Hip Hop lenye jina la Kikosi cha Mizinga linaloongozwa na msanii Kalama Masoud ‘Kalapina’ linatarajia kudondoka ndani ya Ukumbi wa Msasani Club na kutambulisha ngoma zao mpya pamoja na studio yao waliyoipa Kikosi Records, Edna Katabalo anashuka nayo.

Akipiga stori na safu hii, Kalapina alisema kwamba, tukio hilo kubwa litafanyika ndani ya Ukumbi wa Msasani Club, siku ya Pasaka na nyimbo watakazotambulisha ni Pamoja na Pata potea na Hip Hop Agaist Albino.

“Ngoma zote tutakazotambulisha siku hiyo zimetengenezwa ndani ya studio yetu, Kikosi Records, mashabiki wajitokeze kwa wingi ili tuungane katika vita dhidi ya mauaji ya albino ambayo tumeianzisha kupitia sanaa yetu.
**********

Sunday, March 22, 2009

IJUMAA SHOWBIZ!


Dar es Salaam Hands up
Hatimaye shindano jipya kabisa na la kijanja ‘Dar es Salaam Hands Up’ (Dar es Salaam Mikono Juu), tayari limeanza na hawa ndio wakali wa muziki wa Bongo Flava waliotajwa kuiwakilisha Wilaya ya Kinondoni kunako mpambano huo kama tulivyowaomba wasomaji wiki iliyopita.

Wasanii hao kutoka pande za Kinondoni ni Jaffarai, Ray C, Prof. Jay, Fid Q, Kalapina (Kikosi cha Mzinga), A.Y, Mr. Nice, Ngwea, Witness na K-Sher. Nakukumbusha tena, shindano hili linazihusu Wilaya tatu za Dar es Salaam, Kinondoni, Ilala na Temeke ambapo wewe msomaji na mpenzi wa burudani hii utatuambia ni ipi ina wasanii wakali. Baada ya kuwapata wakali kumi kutoka Kinondoni, sasa tunaigeukia Wilaya ya Ilala.

Unachotakiwa kufanya kwa sasa kabla hatujaingia kwenye zoezi kubwa la kuzipigia kura wilaya ni kututajia jina la masanii ambaye unadhani anafanya vyema ndani ya Wilaya ya Ilala kwa kuandika ujumbe mfupi (SMS) ukilitaja jina lake kisha tuma kwenda simu namba 0787-110 173. Kumbuka kwamba kila wilaya itawakilishwa na wasanii kumi.
***********

Miss Utalii azama mapangoni na madenti

Miss Utalii 2006-2007, Consolata Rushau ambaye pia ni mwalimu wa shule moja ya msingi Mkoani Tanga, ameonesha yuko karibu zaidi na fani hiyo kwa kuwapeleka wanafunzi wake kunako makumbusho ya mapango ya Amboni yaliyopo mkoani humo kila anapopata nafasi, Imelda Mtema alipiga naye stori.

Akisema na ShowBiz alipotembelea ndani ya ofisi zetu zilizopo Sinza, Bamaga, Dar es Salaam hivi karibuni, mrembo huyo alitamka kwamba, japo amebahatika kuwa mwalimu, mambo ya utalii yako kwenye damu yake na ndio maana hupenda kuwapeleka wanafunzi wake ili wafahamu zaidi mambo ya kiutalii.

“Urembo ni sehemu ya maisha yangu, nafikiria kuwa mwanamitindo maarufu, japo kuna fani nyingine nazipenda kama uigizaji wa filamu na nyingine. Bado sijakata tamaa wala sijaridhika na taji nililonalo, naendelea kutafuta nafasi nzuri zaidi katika tasnia ya urembo ili nifikie levo za kina Naomi Campbell,” alisema.

*******
Misosi na Neno la Mungu
Ukiisikiliza ngoma yake mpya, ‘Mungu yuko bize’ unaweza kudhani kwamba, mchizi sasa anaelekea kwenye wokovu ukizingatia kuwa siku hizi pia hupendelea kutoka ‘kipapaa’, yaani kiutu uzima, mashati ya mikono mirefu na tai shingoni kitu ambacho yeye binafsi hajaweka wazi.

Namzungumzia kijana kutoka pande za Tanga, Joseph Rushahu ‘Bwana Misosi’ ambaye baada ya kuisikia kazi hiyo mpya tuliamua kumtafuta ili kujua nini hasa kimemsukuma akaamua kutoka na ngoma hiyo iliyomshirikisha mwana TMK Family, Said Juma ‘Chegge’.

“Mungu yuko bize’ ni sanaa tu, si vinginevyo ila ni kazi ambayo iko pande zote na kwa madhehebu yote haijambagua mtu. Kuna baadhi ya binadamu huwa wanajifanya wako bize zaidi wakati Mungu yuko ‘bize’ zaidi. Kuhusu mavazi, Misosi nimeshakuwa mtu mzima, ndiyo sababu iliyonifanya nikanyoa rasta zangu,” alisema Misosi.
********