
Saturday, June 12, 2010
Friday, June 11, 2010
IJUMAA SHOWBIZ!

Binti aliyesimama vyema ndani ya sanaa ya muziki wa kizazi kipya kutoka pande za Kenya, Wahu ambaye juzi kati alidondoka Bongo na kutoa sapoti kwenye uzinduzi wa albamu ya Temba na Chegge, ametajwa kuchukua nafasi ya mwanadada Amani ambaye hivi sasa anaonekana ‘kudrop’ kimtindo.
Baadhi ya wadau wa burudani waliohudhuria kwenye uzinduzi huo uliyofanyika ndani ya Club Sun Cirro,Ubungo Dar mwishoni mwa wiki iliyopita walisema na ShowBiz kwamba hivi sasa Wahu anaonekana yuko juu kuliko wanawake wengine waliopo kwenye game huko nyumbani kwao Kenya.
“Siku hizi siwasikii kwa sana wasanii kama Amani, Nyota Ndogo na wengine waliowahi kuja Bongo na kufunika zaidi ya Wahu ambaye tangu ali poibukia kwenye game hiyo na kufanya vyema na ngoma yake, ‘Sweet Love’ hajawahi kuzimika zaidi ya kusonga mbele.
Akipiga stori na safu hii muda mchache baada ya kushuka stejini, Wahu alisema kwamba anajisikia fahari sana kufanya kazi na wasanii wa Bongo na kualikwa pande hizi mara kadhaa kwa ajili ya shoo. Msanii huyo amewahi kufanya kazi na wasanii kadhaa wa Tanzania wakiwemo Chegge na Temba.
xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Kundi la muziki wa asili kutoka Botswana, Matsuwe Tradition Dance maarufu kama Makhirikhiri bado lipo Bongo na kinachofuata hivi sasa ni ziara mkoani Mbeya ambapo litaangusha shoo ndani ya Uwanja wa mpira wa Sokoine Juni 12, mwaka huu kabla ya kumalizia Iringa katika Uwanja wa Samora.
Sisi kama ShowBiz leo tunamcheki kiongozi wa kundi hilo, Moses Malapela ambaye ana a.k.a ya Shumba Ratshega. Wengi hawajui Shumba katoka wapi mpaka kufikia hapa alipo leo kama kiongozi wa kundi la Makhirikhiri mwenye sauti ya kipekee katika ngoma za muziki huo wa asili.
Mchizi alizaliwa 1981 katika kijiji cha Bobonong, nchini Botswana ni miongoni mwa wasanii wa muziki huo waliopitia pilikapilika za hapa na pale. Alianza kama mcheza shoo ndani ya Kundi la Re Tlaa Re Ke Dipitse Cultural Group lililokuwa hapo hapo kijijini kwao.
Baada ya hapo alijimuvuzisha hadi kwenye kundi lingine lililokuwa na jina la Motswedi Cultural Group. Jina la Shumba alilipata kupitia kabila yao, Kalanga likiwa na maana ya Simba huku lile la Ratshega kwa mashabiki wake alipokuwa akipiga shoo.
Alitoa albamu yake ya kwanza kama muimbaji na mchezaji mwaka 2006 ikiwa na jina la Masiela. Albamu hiyo ambayo haikumtambulisha vyema ilifuatiwa na Makhirikhiri 2007 ambayo ilifanya vizuri na kuuzwa katika nchi kibao zikiwemo Botswana yenyewe, Afrika Kusini, Namibia, Zambia na Zimbabwe.
Mwaka huo huo wa 2007, kupitia Tuzo zenye jina la Mascom-Bomu Awards, Makhirikhiri aliibuka na ushindi kama albamu bora ya asili. Mwaka 2008 Shumba aliitambulisha albamu mpya yenye jina la Ntopolela Bichana kupitia wimbo wa Dikhwaere. Mwaka jana wa 2009 akatambulisha albamu nyingine yenye jina la Kukantsu.
Kupitia muziki wake, Shumba ameweza kujiwekea heshima ndani na nje ya nchi yake Botswana, mfano mzuri ni pale alipofanya shoo mbele ya rais wao mwaka 2008 kwenye sherehe za uhuru na kuwaburudisha mawaziri wote wa nchi hiyo kwenye hafla ya chakula cha usiku.
Kupitia kundi lake, Makhirikhiri, Shumba amewahi kufanya shoo Afrika Kusini, China, Namibia, Zambia na Angola kabla ya kuja Tanzania. Kutokana na heshima aliyoijengea nchi yake kabla hajaja Tanzania, Rais wao, Lt General Seretse Khama Ian Khama alimkabidhi bendera kwa ajili ya kuitangza zaidi Botswana.
**********************************

Kutoka pande za Kijitonyama, Dar mchizi aliyewahi kufanya vyema kupitia ngoma yenye jina la ‘Napenda nini’, Jaffari Ally Mshamu a.k.a Jaffarai amesema na ShowBiz kwamba ‘Demu wangu’, ngoma yake inayofanya vyema hivi sasa tayari imetupiwa kwenye kamera za video na muda wowote inaanza kuuza kunako vituo kadhaa vya televisheni.
Akipiga stori zaidi, Jaffarai alisema kwamba video ya ngoma hiyo imefanyika sehemu kadhaa ndani ya Dar es Salaam chini ya mtayarishaji John Kallage huku ikiwauzisha sura mastaa kibao wa Bongo flava na wadau wa muziki huo ambao ni kipenzi cha msanii huyo.
“Bado naamini kuwa ili msanii afanye kazi nzuri hata kama ni mkongwe lazima aumize kichwa kwa kuandika kazi nzuri, ndiyo maana mimi niko ‘bize’ kuhakikisha kila ngoma ninayotoa inakuwa juu kama hii “Demu wangu’ niliyomshirikisha TID ambaye hakufanya masihara kwenye korasi,” alisema Jaffarai.
xxxxxxxxxxxxxxx

Bendi maarufu ya muziki wa dansi, African Stars a.k.a Twanga Pepeta inatarajia kuadhimisha miaka kumi tangu kuanzishwa kwake kwa sherehe ya kipekee itakayofanyika ndani ya Viwanja vya Leaders Club Juni 27, mwaka huu.
Akipiga stori na ShowBiz, Mkurugenzi wa ASET, Asha Baraka alisema kwamba ishu hiyo ambayo itakwenda sambamba na kusheherekea albamu yao ya kumi, ‘Mwana Dar es Salaam’ itaanza kwa maandamano kutoka kwenye ofisi zao zilizopo Kinondoni mpaka kwenye viwanja hivyo.
“Baada ya kufika uwanjani kutakuwa na michezo mbalimbali kama mpira wa miguu, mpira wa wavu kwa wanawake, mbio za kuku, burudani ya muziki kutoka kwa wasanii wa ndani na nje ya Bongo na mambo mengine mengi ambayo yataifanya siku hiyo ionekane ya kipekee,” alisema Asha Baraka.
Mengi zaidi kuhusu shughuli hiyo, endelea kufuatilia kwenye magazeti yanayochapishwa na Kampuni ya Global Publishers.
xxxxxxxx
Tuesday, June 8, 2010
Unajua kwanini tunaugua mara kwa mara? - 2

Unapoacha kunywa maji kiwango kinachotakiwa kwa siku, mwili wako utatoa ishara yake kupitia mkojo. Utakapoenda haja ndogo, rangi ya mkojo wako itakuwa ya njano na wenye harufu mbaya. Tabia ya kutokunywa maji ikiendelea kwa muda mrefu, siyo tu utakuwa unakojoa mkojo wa njano, bali mwekundu ukiambatana na damu.
Siyo hilo tu, dalili nyingine utakayoiona kutokana na kutokunywa maji, ni kukosa choo kwa siku kadhaa na hata unapokipata, kinakuwa kidogo na kigumu. Kwa kawaida binadamu anatakiwa kupata chooo kikubwa angalau mara moja kila siku, kama siyo mara 2 au tatu, kutegemeana na idadi na aina yam lo anaokula kwa siku.
Madhara ya kuwa na tabia ya kutokupenda kunywa maji kama inavyotakiwa, hayaishii kwenye kukojoa mkojo wa njano au damu na kukosa choo, bali huende mbele zaidi. Matatizo mengine yanayoweza kujitokeza kwenye mfumo wa haja ndogo, ni pamoja na kuziba kwa kibofu cha mkojo na kushindwa kukojoa kabisa.
Halikadhalika, madhara ya kutokunywa maji mengi hayaishii kwenye kukosa choo au kupata choo kigumu, bali hali hiyo ikiendelea husababisha madhara mengine mwilini. Uchafu unapokaa tumboni kwa muda mrefu, hugeuka na kuwa sumu ambayo husambaa katika mfumo wa damu na kudhoofisha kinga ya mwili.
Mtu akisha kuwa katika hali hiyo, anakuwa amejiweka katika hatari ya kupatwa na magonjwa nyemelezi ambayo hutokea wakati wowote. Mwili unapokuwa umejaa sumu, unakuwa sawa na yumba ambayo haijafagiwa siku nyingi ambayo huwezi kushangaa kuona mende, panya, nyenyele, n.k. Mtu mwenye mwili wa aina hii, kuumwa mara kwa mara itakuwa ni jambo la kawaida kwake.
Ulaji chakula
Kwa kawaida, binadamu tunaruhusiwa kula vyakula vyote, lakini kila chakula kina kiasi chake. Mwili una kanuni yake ambapo kuna aina ya vyakula inahitaji kwa wingi kila siku na kuna aina nyingine inahitaji kidogo sana. Eneo hili ndilo linalowashinda watu wengi na kujikuta wanakula vyakula bila mpangilio na mwisho wa siku hukatazwa kuvila kabisa baadhi ya vyakula.
Kula bila kufuata kanuni ya ulaji husababisha mwili kukosa uwezo wake wa asili wa kujilindi. Mungu ameonesha uwezo wake mkubwa katika uumbaji. Aliuumba mwili kisha akauwekea ulinzi wake wa asili dhidi ya wavamizi wa kila aina.
Ndani ya miili yetu kuna kinga za asili ambazo zinapambana na ‘wavamizi’ kila siku bila sisi wenywe kujijua. Binadamu wote hatuko salama dhidi ya maradhi kutokana na mazingira tunayoisha ya kuvuta hewa chafu, kula vyakula visivyo salama, kunywa maji yasiyo salama, hivyo tunahitaji ulinzi wa kutosha, vinginevyo kila siku tutakuwa kitandani wagonjwa.
Ili walinzi wako wa asili waweze kufanya kazi ya kukulinda vizuri, wanahitaji kuwezeshwa.
Itaendelea wiki ijayo...
BRAZIL YAACHA GUMZO BONGO
Monday, June 7, 2010
WIKIENDA SHOWBIZ!
Mkono Mmoja Yawakutanisha Wahu, Michael Ross Bongo
Usiku wa Mkono mmoja ambao ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Club Sun Ciro huku vichwa kutoka TMK Wanaume, Chegge na Temba vikitambulisha albamu yao, Vita uwanjani, uliwakutanisha pia mastaa wawili kutoka Afrika Mashariki, Wahu wa Kenya na Michael Ross kutoka Uganda.
Shoo hiyo ambayo ilianza majira ya saa sita za usiku ilimpa shavu la ukweli Michael Ross ambaye alipanda stejini kupitia juu ya paa la ukumbi huo kabla hajashuka chini na kuanza kuonesha uwezo wake jukwaani huku akiamsha shangwe kutoka kwa mashabiki waliofurika siku hiyo.
Aliyefuatia alikuwa ni Wahu ambaye pia aliufanya usiku huo kuwa wa burudani kabla vijana wa TMk kupanda na kumaliza kazi kwa staili mpya kabisa iliyotawaliwa na shoo ya kiduku kabla hawajamaliza kwa ngoma ya Mkono mmoja iliyomshirikisha Wahu. Msanii Goodzila alitoa sapoti ya nguvu huku shoo nzima ikisimamiwa na B-12 wa kipindi cha XXL cha Clouds FM.



Makhirikhiri Wamaliza kazi kwa kufunika Dar
Kama walivyoahidi wasanii wa kundi la muziki wa asili kutoka Botswana, Makhirikhiri walipodondoka ndani ya ofisi za gazeti hili katikati ya wiki iliyopita, ndivyo walivyofanya juzi ndani ya Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam ambapo waliangusha shoo ya kihistoria.
Wakiongozwa na Shumba Ratshega, Makhirikhiri waligonga staili zao zote ambazo zimetokea kuwavutia mashabiki wengi wa muziki wao tangu walipoanza kulifahamu kundi hilo lililojipatia umaarufu wa ghafla Bongo na kusababisha shangwe zilipuke kwa sana ukumbini.
Baada ya kufanya maajabu Diamond, jamaa walihamishia majeshi ndani ya Uwanja wa Uhuru jana Jumapili na kuacha historia kwa wakazi wa Dar. Makhirikhiri ambao wanaendelea na ziara yao Mkoani Mbeya walipigwa tafu na Wanne Star na mwanadada Mwantum Chambali kutoka kundi la Mshikamano ambaye anatisha kwenye mchezo wa kujinyonganyonga maarufu kama Yoga.
Russel Simmons Hiki ndiyo kifaa chake, baada ya kuwapitia wengine 9
Kutoka pande za mbele a.k.a Marekani leo ndani ya Ebwana Dah! tunacheki listi ya uhusiano wa kimapenzi ya mmoja kati ya waasisi wa muziki wa Hip Hop, Russell Simmons ambaye hivi sasa ameamua kujikita zaidi kwenye biashara ya mavazi, huku akimiliki logo kadhaa ikiwemo ‘Phat Farm’. Ni maombi ya wasomaji wengi wa safu hii hapa Bongo, hasa baada ya kuenea kwa picha za tajiri huyo na mwanamitindo wetu, Flaviana Matata kwenye mtandao.
Kama bado haujafahamu, Russell amewahi kujiachia on bed na mastaa wa kike tisa kabla ya kudondokea kwa Noemie Lenoir (picha kubwa) mwaka jana wa 2010. Lakini pamoja na hao mchizi kutoka ndani ya kundi la Out Cast, ‘brazameni’ Andre Benjamin pia ametajwa kwenye listi ya watu waliowahi kujiachia faragha na Russell kitu ambacho kinaweza kumshangaza kila msomaji ukizingatia kwamba hawa jamaa wote ni wanaume.
Tukirudi kunako listi ya warembo hao, Russell alianza kutoka na Eva Pigford ambaye nyota yake ni Nge akifuatiwa na Karin Taylor, kisha Karrine Steffans, Veronica Webb, Kara Young (1994 - 98), Kimora Lee Simmons ambaye ndiye alikuwa mkewe baada ya kufunga ndoa 1998 kabla ya kupigana chini 2006, kisha kurudiana tena na kuachana moja kwa moja 2009.
Kabla hajaachana na Kimora, Russell alicheza game ya nje ya ndoa kwa kujiachia na mwanadada Porschla Coleman kuanzia 2007 - 08. Baada ya kuachana na Kimora mchizi alitua kwa Julie Henderson 2009 kisha Noemie Lenoir 2009.
Russell alizaliwa pande za Queens, New York, Oktoba 4, 1957, jina lake kamili ni Russell Wendel Simmons. Akiwa na umri wa miaka 52 sasa na urefu wa nchi 5 na futi 8, mchizi alihitimu elimu ya juu katika vyuo vya City College of New York na Harlem vilivyopo huko New York.
Usiku wa Mkono mmoja ambao ulifanyika mwishoni mwa wiki iliyopita ndani ya Club Sun Ciro huku vichwa kutoka TMK Wanaume, Chegge na Temba vikitambulisha albamu yao, Vita uwanjani, uliwakutanisha pia mastaa wawili kutoka Afrika Mashariki, Wahu wa Kenya na Michael Ross kutoka Uganda.
Shoo hiyo ambayo ilianza majira ya saa sita za usiku ilimpa shavu la ukweli Michael Ross ambaye alipanda stejini kupitia juu ya paa la ukumbi huo kabla hajashuka chini na kuanza kuonesha uwezo wake jukwaani huku akiamsha shangwe kutoka kwa mashabiki waliofurika siku hiyo.
Aliyefuatia alikuwa ni Wahu ambaye pia aliufanya usiku huo kuwa wa burudani kabla vijana wa TMk kupanda na kumaliza kazi kwa staili mpya kabisa iliyotawaliwa na shoo ya kiduku kabla hawajamaliza kwa ngoma ya Mkono mmoja iliyomshirikisha Wahu. Msanii Goodzila alitoa sapoti ya nguvu huku shoo nzima ikisimamiwa na B-12 wa kipindi cha XXL cha Clouds FM.
****************************************




Kama walivyoahidi wasanii wa kundi la muziki wa asili kutoka Botswana, Makhirikhiri walipodondoka ndani ya ofisi za gazeti hili katikati ya wiki iliyopita, ndivyo walivyofanya juzi ndani ya Ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam ambapo waliangusha shoo ya kihistoria.
Wakiongozwa na Shumba Ratshega, Makhirikhiri waligonga staili zao zote ambazo zimetokea kuwavutia mashabiki wengi wa muziki wao tangu walipoanza kulifahamu kundi hilo lililojipatia umaarufu wa ghafla Bongo na kusababisha shangwe zilipuke kwa sana ukumbini.
Baada ya kufanya maajabu Diamond, jamaa walihamishia majeshi ndani ya Uwanja wa Uhuru jana Jumapili na kuacha historia kwa wakazi wa Dar. Makhirikhiri ambao wanaendelea na ziara yao Mkoani Mbeya walipigwa tafu na Wanne Star na mwanadada Mwantum Chambali kutoka kundi la Mshikamano ambaye anatisha kwenye mchezo wa kujinyonganyonga maarufu kama Yoga.
************************************

Kutoka pande za mbele a.k.a Marekani leo ndani ya Ebwana Dah! tunacheki listi ya uhusiano wa kimapenzi ya mmoja kati ya waasisi wa muziki wa Hip Hop, Russell Simmons ambaye hivi sasa ameamua kujikita zaidi kwenye biashara ya mavazi, huku akimiliki logo kadhaa ikiwemo ‘Phat Farm’. Ni maombi ya wasomaji wengi wa safu hii hapa Bongo, hasa baada ya kuenea kwa picha za tajiri huyo na mwanamitindo wetu, Flaviana Matata kwenye mtandao.
Kama bado haujafahamu, Russell amewahi kujiachia on bed na mastaa wa kike tisa kabla ya kudondokea kwa Noemie Lenoir (picha kubwa) mwaka jana wa 2010. Lakini pamoja na hao mchizi kutoka ndani ya kundi la Out Cast, ‘brazameni’ Andre Benjamin pia ametajwa kwenye listi ya watu waliowahi kujiachia faragha na Russell kitu ambacho kinaweza kumshangaza kila msomaji ukizingatia kwamba hawa jamaa wote ni wanaume.
Tukirudi kunako listi ya warembo hao, Russell alianza kutoka na Eva Pigford ambaye nyota yake ni Nge akifuatiwa na Karin Taylor, kisha Karrine Steffans, Veronica Webb, Kara Young (1994 - 98), Kimora Lee Simmons ambaye ndiye alikuwa mkewe baada ya kufunga ndoa 1998 kabla ya kupigana chini 2006, kisha kurudiana tena na kuachana moja kwa moja 2009.
Kabla hajaachana na Kimora, Russell alicheza game ya nje ya ndoa kwa kujiachia na mwanadada Porschla Coleman kuanzia 2007 - 08. Baada ya kuachana na Kimora mchizi alitua kwa Julie Henderson 2009 kisha Noemie Lenoir 2009.
Russell alizaliwa pande za Queens, New York, Oktoba 4, 1957, jina lake kamili ni Russell Wendel Simmons. Akiwa na umri wa miaka 52 sasa na urefu wa nchi 5 na futi 8, mchizi alihitimu elimu ya juu katika vyuo vya City College of New York na Harlem vilivyopo huko New York.
Compiled by mc george/ijumaa wikienda
Subscribe to:
Posts (Atom)