Sunday, August 12, 2007

NGONO KWENDA MBELE!!


RICHARD BUKOS NA CHRISTOPHER LISSA
kamera ya Ijumaa Wikienda ikiwa kazini, wikiendi iliyopita iliwanasa njemba moja na mrembo aliyefahamika kwa jina la Prisca Michael wakifanya vitendo vya ngono uchochoroni.

Fumanizi hilo lilitokea usiku wa manane wa kuamkia Jumamosi, katika moja ya vichochoro vilivyopo karibu na Klabu ya High Way Night Park ‘Kwa Macheni’, Magomeni jijini Dar es Salaam.

Timu ya Wikienda ambayo ilikuwepo maeneo hayo, ikikusanya matukio yanayojiri usiku huo ili kuijuza jamii, ilifuatilia kwa karibu ‘mkandamizo’ huo bila kupoteza pointi hata moja.

Kabla ya fumanizi, aliyekuwa wa kwanza kuonwa na waandishi wetu ni Prisca ambaye alikuwa akizunguka zunguka katika maeneo jirani na klabu hiyo kana kwamba alikuwa akitafuta kitu.

Majira ya saa saba na dakika kadhaa za usiku, ilitokea njemba hiyo ambayo haikufahamika jina mara moja na kuanza kuongea na Prisca, maongezi ambayo timu yetu haikufanikiwa kuyanasa.

Hata hivyo, maongezi kati ya wawili hao hayakuchukua muda mrefu, kwani kitambo kidogo, walishuhudiwa wakiongozana kuelekea gizani. Timu yetu, baada ya kuvutiwa na mkanda huo, ilijigawa na kuanza kufuatilia nyendo za Prisca na mwenzake ili kujua mwisho wao.

Aidha, waandishi wetu wakiwa wameandaa kamera tayari kwa kazi mbele yao, waliweza kuwaona wawili hao wakiwa wamejibanza uchochoroni huku wamekumbatiana. Bila kufanya ajizi, kamera yetu ikiwa mbali kidogo kutoka walipokuwa Prisca na mwenzake, ilifanikiwa kupata picha nne zilizopigwa bila kushtukiwa.

Baada ya kukamilisha zoezi la upigaji picha, timu ya gazeti hili iliwasogelea wawili hao kwa lengo la kuwauliza sababu ya kufanya vitendo hivyo uchochoroni, lakini njemba hiyo ilitimua mbio baada ya kujua kwamba watu waliokuwa mbele yake ni waandishi wa habari.

Hata hivyo, ilifanikiwa kumpata Prisca ambaye kabla ya yote alianza kulaumu kwa kukimbiziwa mteja wake. “Nyie wadaku vipi? Mbona mnaingilia anga za watu? Mnaona mpaka mteja wangu amekimbia, bahati yenu ameshanipa changu, vinginevyo tungekabana mashati,” alifoka Prisca.
Mrembo huyo ambaye alikuwa amekolea kilevi aliongeza: “Msione watu wanapeana raha, nyie mnawashwa, haya semeni kama mnataka ‘mchezo’ niwasaidie.”

Alipoulizwa kwa nini alikuwa akifanya mapenzi uchochoroni, mrembo huyo alijibu kwamba hakuna mtu anayeweza kumpangia. “Mapenzi popote, kama aibu mnazo nyie, mimi naangalia biashara, nakubaliana na mtu wangu, tunazama sehemu yoyote anayotaka, kama hana hela ya gesti je, nyie vipi?” Alihoji mrembo huyo.

Hata hivyo, baada ya kutuliza munkari, mrembo huyo alisema, hafanyi biashara ya kuuza mwili kwa shida kwa sababu anatoka kwenye familia inayojiweza kifedha. Alisema, anafanya ukahaba kama ‘hobi’ na kuongeza kuwa wazazi wake wameshajitahidi kumfanya aache lakini imeshindikana.

“Nyumbani kwetu ni Kimara, mimi naitwa Prisca Michael, baba yangu ni mtu mwenye uwezo tu, kwahiyo msinione hapa mkadhani labda shida ndiyo zimenifanya niwe changudoa,” aliongeza mrembo. Baadaye, waandishi wetu walimpiga picha mrembo huyo akiwa amepozi, baada kuomba afanyiwe hivyo kwakuwa endapo ataonekana gazetini, basi wateja wataongezeka.

Huu ni uchafu ambao haupaswi kufumbiwa macho, Ukimwi unazidi kushika kasi, lakini miongoni mwa tabia hatarishi za ugonjwa huo ni biashara ya ngono. Jamii bado inahitaji kuelimishwa zaidi ili yapatikane mapinduzi ya fikra, vitendo vinavyofanyika usiku vinatisha, hatuwezi kuzuia Ukimwi kama tunafumbia macho uchafu utokeao usiku. Mhariri



Mariam Mashauri aeleza yaliyomkuta gerezani

Wanza Temu na Imelda Mtema

Aliyekuwa Mshiriki wa Shindano la Muziki la Bongo Star Search (BSS) mwaka 2006-07, Mariam Mashauri, ameeleza yaliyomkuta gerezani sambamba na kusimulia picha halisi ya maisha ya mfungwa wa kike.

Kwa mujibu wa mahojiano kati ya waandishi wetu na mwanamuziki huyo, Ijumaa iliyopita jijini Dar es Salaam, Mariam pia alimshukuru Mungu kwa kuachiwa huru ikiwa ni miezi mitatu tangu alipohukumiwa kifungo cha miaka mitano jela.

Mariam ambaye alikuwa katika Gereza la Segerea jijini Dar es Salaam, aliongea mambo kadhaa kuhusiana na maisha ya ufungwa, katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Mikocheni B, ikiwa ni saa kadhaa baada ya kuachiwa huru.

Mahojiano hayo yalikuwa kama ifuatavyo;
Wikienda: Habari yako Dada Mariamu na hongera kwa kuachiwa huru.
Mariamu: Ahsante sana, namshukuru Mungu yeye ndiye muweza wa yote.

Wikenda: Sisi ni waandishi wa habari kutoka Gazeti la Ijumaa Wikienda, kwanza tunakupa pole kwa matatizo yaliyokupata, lakini ni vizuri kama utatueleza unajisikiaje kuwa huru na imekuwaje leo umeachiwa?

Mariamu: Ahsanteni, nimeachiwa kwa sababu baada ya kuhukumiwa, nilikata rufaa kwa sababu sikutendewa haki kwenye hukumu ya kwanza, kwahiyo nimeshinda, mimi ni Mtanzania na cheti cha kuachiwa hiki hapa (anawaonesha waandishi).

Wikienda: Unadhani nini chanzo cha kuenea habari kwamba wewe siyo Mtanzania na kusababisha ukafungwa?

Mariamu: Watu siyo wazuri, wapo wasiopenda maendeleo yangu, wanasema lafudhi yangu, lakini hiyo ni kuongea tu wala haina maana kuwa mimi ni mgeni wa nchi hii, chanzo cha hayo yote ni rafiki yangu mmoja, yeye ndiye aliyenichongea hadi nikapata matatizo yote, ukweli ni kwamba mimi ni Mtanzania, baba yangu ni Msambaa wa Tanga ila mama ni Mzambia.

Wikienda: Kwa maana hiyo unamjua adui yako, sasa unatarajia kuchukua hatua gani dhidi yake?

Mariamu: Nimeshamsamehe, sitochukua hatua yoyote, haki ipo mbele ya Mungu peke yake.

Wikienda: Zipo taarifa ambazo zimezagaa kila kona kuhusu jela kwamba kuna vitendo viovu, ushoga kwa wanaume, usagaji kwa wanawake, uvutaji wa bangi na wafungwa wa kike kulazimishwa ngono na askari magereza wa kiume, je, wewe yalikukuta hayo?

Mariamu: Namshukuru Mungu sana, mimi sikuwahi kukutana na vitendo hivyo, huwa nasikia hata nilipokuwepo gerezani nilisikia watu wakisema mambo hayo, lakini haikutokea kwangu, Mungu ni mkubwa, alinikinga kwa yote.

Naweza kusema jela imenisaidia kwa kiasi fulani, imenifunza mambo mengi, kule kulikuwa na ngoma ya gereza, kwahiyo nilikuwa nacheza sana, pia nimejifunza kushona masweta na mambo mengine.

Wikienda: Kuna vitu gani ambavyo vilikuwa vikikukwaza katika kipindi chote cha miezi mitatu uliyokuwepo gerezani?

Mariamu: Washiriki wenzangu katika Shindano la Bongo Star Search hawakuja kuniona hata siku moja, kwa kweli ilinisikitisha sana kuona hata majaji wetu hawakunijali angalau kuja kunipiga jicho hata mara moja, hata hivyo, sina kinyongo, nimewasamehe wote.

Wikienda: Ukiambiwa utaje vitu ambavyo utavikumbuka sana gerezani, utaorodhesha nini na nini?

Mariamu: Mimi nilikuwa nikitunga nyimbo na kuimba, mpaka sasa nina albamu yangu ambayo imekamilika kwa nyimbo tano, pia wafungwa wenzangu, niliwazoea sana, mimi nilikuwa mpole kwahiyo nilielewana na kila mtu, wakawa wakarimu kwangu, niliwafundisha kumjua Mungu na kutubu dhambi na leo nilipowaaga, wengi wamelia machozi.

Wikienda: Vipi 'msosi' wa gerezani, ulikuwa unapanda au ulikuwa ni adhabu kwako?

Mariamu: Nilikuwa nakula chakula bila kudengua, nilijua kila kitu ni mapito tu.

Wikienda: Tunafurahi upo huru tena, tunakupongeza, lakini tunataraji kukuona ukiwasha moto mkali kwenye fani yako ya muziki.

Mariamu: Ahsante, kazi ipo.

1 comment:

Anonymous said...

sijaona uhisiano wa kichwa cha habari na maelezo yaliopo hapo. kimsingi kichwa hiki kilikuwa kinaonyesha msanii kudai hali mbaya jela ila habari yenyewe haiko hivyo. Ni vyema waandishiiam kurudi uraiani tena wa habari wakawa wana kiasi kwenye maandishi. Hongera dada mar