Sunday, August 12, 2007

WADAU WA UREMBO BONGO: MNAMKUMBUKA MREMBO HUYU?


Leo Abby Cool & MC Geroge Over The Weekend imeamua kukufanyia bonge la surprise, imetega na mitego imemnasa na kumuibua Miss Tanzania namba 2 mwaka 1999 - 2000, Ayan Hassan(pichani juu) kisha kupiga naye stori.

Akiongea kupitia mtandao wa internet, mnyange Ayan alisema kwamba, muda mrefu aliotoweka nchini yupo kwenye ardhi ya Malkia Elizabeth, UK, akilisongesha gurudumu la maisha na amekuwepo nchini humo kwa miaka mitano sasa.

Aidha mlimbwende huyo aliyepata kutingisha kunako sanaa ya urembo alisema kuwa, akiwa nchini humo tayari ameshamaliza masomo yake ngazi ya diploma, yaliyomgharimu miaka mitatu katika chuo cha Hammersmith and West London cha London, England na sasa hivi anajipanga kwenda kutembea USA.

Pia nina mpango wa kurudi nyumbani na ninamatumaini ya kufungua biashara yangu mwenyewe, japo sijaamua nifanye bishara ya aina gani. Kuhusu masuala ya urembo kwasasa nimeyaweka kando, sina mpango wa kuendelea na mambo ya urembo kwa sasa, labda baadaye.

"Ningependa kuwashauri washiriki wa urembo wajitahidi kujihadhari na gonjwa la ukimwi. Ningewaomba kwakuwa wao ni jicho la umma wawe mstari wa mbele katika kuielimisha jamii kuhusu HIV hasa vijana."Rais Kikwete (Jakaya) kashatoa mfano naomba tumuunge mkono", alisema Ayan Hassan.

No comments: