Monday, November 26, 2007

Wakali wa Taarab uso kwa uso Diamond Jubelee wiki hii

Ule mpambano wa Taarab uliokuwa ukisubiriwa kwa hamu kubwa na wapenzi wa sanaa hiyo sasa umewadia, tunahesabu siku tatu tu iwadie Novemba 30, mwaka huu wapambanaji wakutane dani ya ukumbi wa Diamond Jubilee.

Kampuni za QSSP Group kupitia Kituo chake cha Televisheni cha C2C na LIRO Promotion ndiyo waandaaji wa shughuli hiyo nzito ambao waliyataja makundi yaliyofanikiwa kupenya na kuingia kunako fainali hizo ambayo ni Jahazi Modern Taarab (Wana wa Nakshi nakshi), Dar Modern Taarab (Watoto wa Kandoro, Wajukuu wa Makamba) East African Melody (Watoto wa mjini).

Meneja wa C2C, Bahati Singh alisema kwamba baada ya kutolewa kwa kundi la Zanzibar Stars kupitia mchuo uliokuwa unafanyika katika kituo hicho cha televisheni, mashabiki wanatakiwa waendelee kuyapigia kura makundi hayo matatu ili kuliwezesha moja kuibuka na ushindi siku hiyo ya fainali.

'Mashabiki wanatakiwa kupiga kura zao ili apatikane mshindi mmoja. Ili kuliwezesha kundi la East African Melody unaandika neno 'EAM' kupitia simu yako ya mkononi kisha unatuma kwenda namba 15551, Dar Modern Taarab unaandika 'DMT' kwenda namba 15551 na Jahazi Modern Taarab unaandika 'JMT' kwenda 15551', alisema Singh.

Mpambano huo unakujia chini ya wadhamini kibao, ikiwemo Kampuni ya Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Uwazi, Amani, The Bongo Sun, Championi, Risasi, Ijumaa na Ijumaa Wikienda.

No comments: