Friday, August 20, 2010

IJUMAA SHOWBIZ!

Lloyd Banks Aipaisha Bongo
Mkali wa Muziki wa Hip Hop kutoka kruu ya G-Unit inayowakilisha kutoka pande za New York, Marekani, Lloyd Banks amelipa fadhila za shangwe alizopewa na mashabiki alipokuja kufanya shoo Bongo akiwa na 50 Cent mwaka 2008, baada ya kushusha ngoma mpya ambayo ndani yake ina mashairi yanayozungumzia Bongo.

Ngoma hiyo inayokwenda kwa jina la Any Girl, aliyomshirikisha staa kutoka lebo ya Murder Inc aitwaye Lloyd Polite Jr, imelipa shavu la kutosha Bongo.
““Nimefanya shoo nyingi Ulaya na Amerika lakini kwa Afrika siku zote nimekuwa siisahau Tanzania ndiyo maana nimeamua kuzungumza kitu kuhusu nchini hii, kwangu mim ni nchi nzuri na nimeipenda sana,” alisema katika mtandao mmoja wa burudani nchini Marekani.

Baadhi ya mistari inayosikika katika mashairi ya pini hilo ni kama hivi; ‘ Baby, I’m a millionair, got a show hoppin outta’ the leer in Tanzania.’

Promota: Sikumuomba penzi Ray C ila...
Baada ya kutupiwa lawama za kumtaka kimapenzi nyota wa muziki kutoka Bongo, Rehema Chalamila ‘Ray C’, promota maarufu wa muziki pande za ‘Nai’ (Nairobi) anayejulikana kwa jina moja la Saadat, ameibuka na kutupilia mbali madai hayo kuwa hakuwahi kufanya hivyo.

Kwa mujibu wa habari kutoka mtandao wa kenyaonline, promota huyo alitanabaisha kuwa ingekuwa ni vigumu kwake kumualika nyota huyo wa Kitanzania kupiga shoo mara nyingi kama angekuwa amemtaka kimapezi pindi alipokutana naye hapa Bongo.

“Kama nilimtaka kimapenzi na akanichomolea kwanini nimemleta Kenya baada ya mwezi mmoja na nusu tangu nikutane naye Tanzania? Je, kama nilikuwa namtaka ningewalipia tiketi ya ndege yeye na boyfriend wake Lord ili waje Kenya? Je, hivyo ndivyo angefanya mtu ambaye anamtaka mwanamke kimapenzi?” Alihoji promota huyo na kukaririwa na mtandao huo unaojihusisha na mambo ya mastaa nchini humo.

Nasaka mahela kwenye filamu na muziki- H . BABA
Siku chache kabla ya kudondosha sinema yake mpya kitaani iliyopewa jina la Promota, mkali wa miondoko ya TAKEU Bongo, Hamis Ramadhani a.k.a H. Baba amekanusha stori pepe zilizozagaa mtaani kuwa ameuweka kando muziki.

Akizungumza na ShowBiz hivi karibuni jijini Dar, mkali huyo mwenye vipaji lukuki aliweka kweupe kuwa, ishu ya yeye kugonga muvi isitafsiriwe kama katoa mkono wa kwaheri kwenye muziki kwani anasaka mahela kote kote.

Huyu hapa anafafanua: “Siyo kweli kuwa nimeacha muziki, mimi ni msanii hivyo nina nafasi ya kufanya aina yoyote ya sanaa hapa duniani, iwe muziki, filamu, maigizo, sarakasi na mazingaombwe, hizo zote ni kazi zangu na ndiyo maisha yangu, siwezi kuacha muziki hata siku moja.” Mzigo huu umeshushwa na Hemed Kisanda.

Chipukizi wa filamu wamtolea chozi JB
Baadhi ya wasanii chipukizi wa filamu Bongo wamemtolea chozi staa anayetesa kwenye field hiyo, Jacob Steven ‘JB’ wakimtaka awashirikishe kwenye sinema zake ili watoke kisanii, muziki mzima unaletwa na Jelard Lucas.

Akizoza na kona hii juzi Jumatano, jijini Dar es Salaam, alipokutana uso kwa macho na paparazi wetu, JB alisema mara kwa mara amekuwa akiombwa na wasanii chipukizi awashirikishe kwenye filamu zake.

“Labda niweke wazi kwamba, sasa nataka kuwasaidia kwa dhati kabisa, kama wewe ni chipukizi na unajua una kipaji, tuwasiliane,” alisema JB na kuongeza: “Unajua leo tupo, kesho hatupo kwahiyo lazima tufungue milango ya kuwasaidia wale wenye vipaji ili tukiwa hatupo waweze kuchukua nafasi zetu. Mimi nimeamua kwa dhati kabisa, kuwasaidia kupitia Kampuni yangu ya Jerusalem Film Compony.”

ShowBiz inampa tano JB kwa uamuzi wake huo ambao kiukweli utainua vipaji vya wasanii wetu. Poa sana mwana!!!

Wednesday, August 18, 2010

Ngoma Africa Band wazidi kupeta

FFU wa Ngoma Africa Band wameendelea kutikisa baada ya kutoa shoo kali katika jukwaa la World Music Festival, mjini Loshasen, Ujerumani hivi karibuni.

Kufunga kuna faida gani kiafya?


Umekuwepo mjadala wa kisayansi wa muda mrefu kuhusu kufunga kama kuna manufaa kwa afya ya mtu ama la. Kufunga ni sehemu muhimu ya imani nyingi za kidini, kuanzia Waislamu, Wakristo hadi Wayahudi. Wengi wana mashaka kama faida ya kiroho inayopatika kutokana na funga huwa na uhusiano na afya ya mwili.

Jumuiya nyingi za wataalamu wa tiba mbadala, wanaamini kwamba funga inaweza kufanya maajabu makubwa katika mwili wa binadamu. Katika makala haya, tutajaribu kuangalia hoja zinazotolewa na wataalamu hao wa tiba mbadala katika jitihada za kuihabarisha jamii umuhimu wa funga kiafya.

Kitaalamu, funga huanza kufanya kazi ndani ya saa 10 za kwanza hadi saa 24. Kwa sababu ili athari za funga zianze kuonekana ni mpaka akiba ya wanga iliyomo mwilini inapoanza kutumika kama chanzo cha nishati. Mtu huanza kusikia njaa, pale akiba ya protini inapokwisha mwilini kama nishati.

Kwa kawaida, mwili huwa na uwezo wa kijisafisha wenyewe kwa kutoa sumu mwilini (Detoxification) na hii ndiyo hoja kubwa inayotumiwa na wataalamu wa tiba mbadala wanaoamini funga ni tiba na kinga ya maradhi mengi. Detoxification ni mchakato wa mwili kuua na kutoa sumu mwilini kupitia haja kubwa, ini, figo, mapafu na kwa njia ya ngozi (jasho, n.k).

Faida nyingine ya funga inayoelezewa ni ule mchakato wa uponyaji unaofanyika mwilini wakati mtu anapokuwa amefunga. Inaelezwa kuwa wakati wa funga, ile nishati inayoelekezwa kwenye mfumo wa usagaji chakula, huelekezwa kwenye mfumo wa ‘metabolizi’ na mfumo wa kinga ya mwili. Katika kipindi hicho, magonjwa na mauvimbe ya ajabu ajabu huweza kudhibitiwa na hatimaye kutoweka kabisa.

Vile vile ukarabati wa seli zilizoathirika huko nyuma, huweza kutengenezwa upya na kuwa imara zaidi. Mwisho, faida kubwa iliyothibitishwa kisayansi itokanayo na funga, ni kwamba mtu anayefunga, mwili wake huimarika na miaka yake ya kuishi huongezeka! Faida hii inatokana na ukweli kwamba wakati wa funga uzalishaji wa protini mwilini huwa mkubwa, kasi ya ‘metaboliz’ hushuka, mfumo wa kinga ya mwili huimarika zaidi.

Kuongezeka kwa uzalishaji wa homoni za mwili ndiko kunakochangia faida hizi za muda mrefu. Pamoja na kuongezeka kwa uzalishaji wa homoni za ukuwaji wa mwili, homoni za kuzuia uzeekaji wa mwili nazo huzalishwa kwa wingi wakati wa funga, hivyo kumfanya mtu anayefunga mara kwa mara kuonekana kijana kila siku.

Kwa kuhitimisha, inaonekana kuna sababu nyingi za msingi za kuamini kuwa funga ina faida nyingi kwa afya ya binadamu. Hata hivyo, bado kuna baadhi ya madaktari wengine hukataza watu kufunga kwa muda mrefu bila kupata ushauri wao kwa madai kuwa kufunga kuna madhara katika afya, na hii imetokana na ukweli kwamba jamii imekuwa ikiamini kwamba ili mtu uishi unahitaji kula, iweje leo mtu usipokula utaishi sana? Lakini wanasahu kuwa Mungu aliyetuamrisha kufunga anajua zaidi yetu!



Monday, August 16, 2010

WIKIENDA SHOWBIZ!

Lil Kim Hawa wote kadondoka nao kitandani!
Last week haikusomeka kwa sababu ya kuitendea haki shoo ya Fiesta lakini Blue Monday hii, Ebwana Dah! inakujia tena. Leo anaangazwa mtoto wa kike chakaramu ambaye Jumamosi ya Agosti 7, 2010 alisababisha mzozo alipofanya makamuzi ya kiwango cha juu kwenye Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar.

Mtajwa ni Kimberly Denise Jones ‘Lil’ Kim’ ambaye katika kulinogesha Tamasha la Fiesta 2010, alifanya ‘upacha’ jukwaani na Mfalme wa Temeke, Juma Kassim Kiroboto ‘Sir Nature’ na kutoa shoo ambayo imeacha simulizi kwa Watanzania.

Kinachohusu hapa ni nani kafaidi penzi la staa huyo. Kwa mujibu wa site ya kiwanja ambayo inadili na issues za uhusiano wa mastaa wa kiwanja, kidume Andre Benjamin ndiye anayetajwa kuwa wa kwanza kutoka na Lil’ Kim ingawa haitajwi ni mwaka gani.
Baba Beyonce, Sean Carter ‘Jay Z’ anatajwa wa pili, halafu anaungwa marehemu Christopher Wallace ‘Notorious BIG’, anakuja Damian Hardy na wote hao haielezwi ni lini walianza kumchangamkia Lil’ Kim wala kivipi waliachana.

Mwaka 1997, Lil’ Kim hakuona soo kuachia penzi kwa swahiba wa BIG, Sean Combs ‘P. Diddy’, baada ya hapo alimegana kisela na mdogo wake Brandy Norwood, Ray-J.
Mwaka 2003 alijitoa kwa Damian ‘World’ Hardy, kisha akaamua kwenda sawa kwenye penzi la kisagaji na mkali mwenzake wa Hip Hop, Missy Elliot, alipohisi anahitaji mwanaume na si mwanamke mwenzake, mwaka 2004, alitua mikononi mwa Scott Storch.

Mwaka 2007, alitua kwa Jamie Foxx na penzi lao linasomeka mpaka sasa, ingawa mwaka 2008, alisaliti ‘kiduchu’ na kwenda kuchangamsha damu na Tracy Morgan.
Lil’ Kim ana umri wa miaka 35. Alizaliwa Julai 11, 1975, New York, Marekani. Mbali na kurap, pia anaandika nyimbo na kuigiza. A.k.a yake nyingine ni Queen Bee.
**************************************
Jully Tax: Bongo Movie yaipiga mwereka Nigeria
Director wa filamu mwenye kichwa chenye ‘madini’ ya thamani kubwa, Mfaume Abdul Hassan ‘Jully Tax’ amesema kuwa hivi sasa soko la filamu Afrika linatekwa na Tanzania na nchi nyingi zinakubali ubora wa Bongo Movies kuliko zile za Nollywood, Nigeria.

Katika straight talk to Abby Cool & MC George over the weekend juzi (Jumamosi), Jully Tax ambaye ndiye aliyegundua vipaji vya mwanamuziki Hamis Ramadhan Baba ‘H-Baba’, alisema kuwa baada ya kufanya filamu nyingi nchini, alipata mualiko nchi mbalimbali na kujionea mapinduzi makubwa ya sanaa ya Tanzania.

“Nilikuwa Bukavu, DRC nikajionea maajabu. Kwanza nilikuwa sijui kama tunakubalika lakini nilipokelewa kama kiongozi wa nchi na kupewa heshima zote na ujumbe mkubwa ambao nilipewa ni kwamba Watanzania hatujiamini,” alisema Jully Tax na kuongeza:

“Wakati nafanyiwa mahojiano kwenye televisheni Bukavu, kuna watazamaji walinipiga simu na kuuliza ni kwanini wao wakitazama picha za kutisha za Tanzania wanazikubali kuliko za Wanigeria, lakini Tanzania mpaka leo wanasema wapo nyuma kwa Wanigeria?

Jully Tax aliye pia prodyuza wa filamu, ameendelea kuthibitisha kiwango chake katika kuandika, kutayarisha na kuongoza ‘muvi’ zenye sura ya mauzauza barani Afrika.

Mtayarishaji huyo, pia ndiye ‘injini’ ya filamu ya Chozi la Urithi, Mtemi, Radi Cobra, Saladini, Mama wa Kambo na Kuku Awikia Tumboni.
****************************************************
‘Promota’ ya H-Baba ipo tayari
STAA wa TAKEU, Hamis Ramadhan Baba ‘H-Baba’ amesema kuwa sasa yupo tayari kuidondosha mtaani muvi yake inayoitwa Promota, baada ya kukamilika kwa mpango mzima wa kuitengeneza. Muvi hiyo imetengenezwa ndani ya mjengo wa Movie Galaxy, Mwanza na kusimamiwa na Tollywood Movies yenye mkono wake nchi nzima.

Akistorisha ‘fesi tu fesi’ na Abby Cool & MC George over the weekend juzi, H-Baba aliweka wazi kuwa ana uhakika muvi hiyo iliyosheheni wakali kibao, itafanya mapinduzi makubwa ukizingatia muongozaji wake ni wa kiwango cha juu.

“Muongozaji ni Jully Tax (Mfaume Abdul Hassan) ambaye uwezo wake unakubalika. Kuna wasanii wakali kama Yusuf Mlelana wengineo, ni filamu ya kiwango cha juu. Nataka kuonesha kiwango changu kwenye usanii. Nimetisha kwenye muziki na sasa nataka kufanya kweli katika filamu,” alisema H-Baba na kuongeza:

“Nimefanya hii muvi kwa uhakika na najua mashabiki wangu wataipenda.”
Imeandikwa na Na Jelard Lucas

***************************************************

DIAMOND, TANZANITE ‘BHITA’ NI ‘BHITA’
Harufu ya bifu zito kati ya wasanii chipukizi wa muziki wa Kizazi Kipya Bongo, Mwingereza Athuman Mwingereza ‘Tanzanite’ na Nassib Abdul ‘Diamond’ sasa imefika puani kufuatia kukutana ‘laivu’ kwa wawili hao.

Diamond anatamba kitaani na kibao chake cha ‘Mbagala’ huku Tanzanite akidaiwa ‘kuangalizia’ wimbo huo kwa sauti na ‘biti’ katika wimbo wake wa ‘Kafara’.

Katika kipindi cha ‘Saturday Night Live’ kilichorushwa angani na runinga ya Channel Ten (EATV) Ijumaa iliyomalizika, wasanii hao walikutana ‘laivu’ na kidogo ‘pasitoshe’ baada ya Diamond kuonesha wazi hasira zake dhidi ya Tanzanite. Mzuka ulipanda zaidi kufuatia ‘Prizenta’ wa kipindi hicho, Jimmy Kabwe kumuuliza Tanzanite ni kwanini alikopi wimbo huo kwa sauti na biti, ambapo alijibu alikuwa akijaribu lakini akashangaa kusikia wimbo huo unarushwa hewani na vituo vya redio Bongo.

Katika majibu yake, Diamond alisema msanii huyo ni mwongo ‘mkubwa’ na kwamba, tayari yeye ameshampeleka msanii huyo kwenye ‘mahakama’ ya COSOTA licha ya kwamba, hajui ni kwanini mpaka sasa chama hicho cha kusimamia kazi za wasanii hakijamchukulia hatua Tanzanite.
****************************************
Wagosi kuvunjika; Mkoloni atoa tamko
Kundi lenye heshima kubwa Bongo, Wagosi wa Kaya limetajwa kuvunjika baada ya mmoja wa wasanii wake, John Simba ‘Dk. John’ kueleza kuwa hakuna alichobakiza ndani ya kundi. Memba mwingine, Fred Maliki ‘Kinega Mkoloni’ ameamua kutoa tamko lake kupitia Abby Cool & MC George over the weekend.

Mkoloni ambaye ni main character wa project ya Antivirus, ali-speak loudly na kona hii wikiendi iliyopita kuwa Wagosi wa Kaya bado lipo mzigoni na tamko la John halina msingi unaoeleweka.

Mwanaharakati huyo wa CHADEMA alisema, Wagosi wa Kaya bado ni hazina kubwa ambayo inaendelea kuingiza ‘faranga’ kila baada ya kipindi fulani kutokana na kazi nzuri walizorekodi mwanzoni mwa miaka ya 2000.

“Mpaka kuna wakati tunaitwa kwa Mdosi kugonga kopi, kuna kazi zetu Ulaya tulizipeleka na fungu huwa linakuja, kwahiyo siwezi kukubali kundi life halafu haki yangu ipotee,” alisema Mkoloni na kuongeza:

“Wagosi wa Kaya hatukuandika mkataba wa kuwa pamoja, kwahiyo yeye akiondoka basi na afanye hivyo kwa maslahi yake lakini kundi litaendelea kuwepo kwa sababu mimi bado nalihitaji na nina maslahi nalo.

“Kundi likifa, tukiitwa na Mdosi kugonga kopi yeye ataenda kama nani? Nadhani alipaswa kukaa na mimi tushauriane. Ni bora angesema yeye amesitisha kufanya kazi kama kundi na Wagosi wa Kaya kuliko kuzungumza kwamba limekufa. Bado lipo, nitaendelea kulisimamisha.”

Mkoloni alitoa tamko hilo, baada ya Dk John kukaririwa akisema kuwa Wagosi wa Kaya lvimekufa kwa sababu Mkoloni amejiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).
“Hiki ni kichekesho, Wagosi wa Kaya si kundi la siasa, tulikuwa tunafanya muziki na nje ya jukwaa kila mmoja ana itikadi yake, iweje leo kujiunga CHADEMA iwe chanzo? Ningeenda CCM je?” Alihoji Mkoloni.

Sunday, August 15, 2010

MSIMU MPYA, MALI MPYA ZIZZOU FASHIONS!


UZI MPYA WA ENGLAD

UZI MPYA WA CHELSEA
UZI MPYA WA MAN U

UZI MPYA WA LIVERPOOL







KWA MAELEZO NA KUJUA BEI ZAO, WASILIANA NA ZIZZOU FASHIONS STORES WAPO KIJITONYAMA VICTORIA OIL COM PETROL STATION NA SINZA AFRICA SANA:
TEL: +255 714 383330.

MSIMU MPYA, MALI MPYA ZIZZOU FASHIONS!















KWA MAELEZO NA KUJUA BEI ZAO, WASILIANA NA ZIZZOU FASHIONS STORES WAPO KIJITONYAMA VICTORIA OIL COM PETROL STATION NA SINZA AFRICA SANA:
TEL: +255 714 383330
.